Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- (a) Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu miradi ya maji ya Kali, Rukoma, Ilagala, Kandego, Uvinza na Nguruka ambayo wakandarasi wamesimama kwa ukosefu wa fedha? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. HASNA S.K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Waziri lakini tumekuwa na tatizo kubwa la wakandarasi hawa, kwa mfano, Mradi wa Nguruka Mheshimiwa Rais alifanya ziara tarehe 23 Julai, 2017 akatoa tamko hadi Desemba. 2017 Mradi wa Nguruka uwe umekamilika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pesa zinaletwa na Serikali wakandarasi hawa hawakamilishi miradi hii na mradi wa Nguruka wananchi wanaona pesa zinaingia lakini hawapati maji. Mradi wa Uvinza pesa zinaletwa lakini wakandarasi hawakamilishi ili wananchi wapate maji. Mradi wa Kandaga Mheshimiwa Waziri wewe ni shahidi tarehe 17 Julai, 2018 tulifanya ziara pale ukampa mkandarasi wiki mbili lakini hadi leo hii hakuna maji yanayotoka pale. Swali langu la kwanza, je, Serikali ina kauli gani kwa hawa wakandarasi ambao wanalipwa pesa lakini hawakamilishi miradi kwa wakati? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, tarehe 29 Julai, 2018, Mheshimiwa Waziri Mkuu alifanya ziara kwenye Kijiji cha Mwakizega na wananchi wakamlilia kwamba tunahitaji maji na tamko tukaambiwa tuandae taarifa ya mradi wa maji ili tuweze kuwasilisha Wizarani. Hivi navyoongea Injinia wa Maji Halmashauri ya Uvinza yuko hapa Dodoma ameshawasilisha andiko hilo la mradi ambalo linagharimu kiasi cha shilingi bilioni 1.9. Je, ni lini sasa Wizara itatuletea pesa ili tuanze kutekeleza huu mradi mpya wa Mwakizega? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Hasna, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza kwamba Serikali inachukua hatua gani kwa wakandarasi ambao wanashindwa kukamilisha kazi kwa wakati. Kuna taratibu mbalimbali Serikali inachukua kama mkandarasi anashindwa kukamilisha kazi kwa wakati. Hatua ya kwanza, kama mkandarasi anachelewesha kazi tunampiga faini kutokana na ucheleweshaji na kila siku mkandarasi huyo analipa faini inategemeana na mradi wenyewe na kiasi cha gharama za mradi. Hatua ya pili ambayo kama mkandarasi atashindwa kutelekeza kazi kwa wakati tunaweza kumfutia usajili na mwisho wake hatoweza kufanya kazi yoyote ya ukandarasi kwenye sekta zote za ujenzi pamoja maji na sekta zote hapa nchini. Tutawasimamia wakandarasi wote tuhakikishe kwamba wanafanya kazi kwa wakati na wanazimaliza kwa wakati ili Watanzania ambao wamesubiri maji kwa muda mrefu waweze kupata maji na salama kwa muda unaostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili Mheshimiwa Mbunge amezungumzia kuhusu andiko, andiko tumelipokea na kama kawaida andiko lolote lazima lipitie michakato mbalimbali. Mara litakapokamilika tutaweza kutoa fedha ili mradi huo uweze kutekelezwa. (Makofi)

Name

Frank George Mwakajoka

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tunduma

Primary Question

MHE. HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- (a) Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu miradi ya maji ya Kali, Rukoma, Ilagala, Kandego, Uvinza na Nguruka ambayo wakandarasi wamesimama kwa ukosefu wa fedha? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. FRANK G. MWAKAJOKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uko mradi ambao unataka kutekelezwa kwenye Mji wa Tunduma na SADC na Mheshimiwa Waziri katika Bunge lililopita alisema kwamba ameshampeleka consultant pale. Wananchi wa Tunduma wanataka kujua mpaka sasa mradi umefikia kiwango gani katika maandalizi ya utekelezaji?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge wa Tunduma, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kweli consultant ameenda kwa ajili ya mradi huo lakini taratibu za utekelezaji zinakwenda hatua kwa hatua. Kwanza consultant anakwenda kufanya study analeta hiyo study tutaipitia baadaye kama pesa ipo utafuata mchakato wa kutafuta mkandarasi ili aweze kufanya kazi hiyo.

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Primary Question

MHE. HASNA S. K. MWILIMA aliuliza:- (a) Je, Serikali inatoa kauli gani kuhusu miradi ya maji ya Kali, Rukoma, Ilagala, Kandego, Uvinza na Nguruka ambayo wakandarasi wamesimama kwa ukosefu wa fedha? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. DUNSTAN L. KITANDULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa niulize swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika bajeti ya mwaka huu tumetenga fedha kwa ajili ya kufanya usanifu wa Mradi wa Kupeleka Maji Makao Makuu ya Wilaya ya Mkinga kutoka Mto Zigi kuelekea Horohoro lakini mpaka sasa hakuna dalili yoyote ya jambo hili kufanyika. Ni lini usanifu huu utaanza?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge wa Mkinga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba usanifu huo utaanza mara moja, tunajipanga kuhakikisha kwamba tunatafuta wataalam ili wakafanye kazi hiyo.