Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Augustino Manyanda Masele

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Je, ni lini mgodi utafunguliwa katika eneo la Nyakafuru Wilayani Mbogwe baada ya utafiti kuchukua muda mrefu kwenye eneo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. AUGUSTINO M. MASELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa eneo hili la Nyakafuru limekuwa chini ya utafiti kwa muda mrefu na tayari wachimbaji wadogo wameshalivamia. Je, Serikali iko tayari sasa kuwamilikisha wachimbaji hao wadogo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, eneo pia la Nakanegere Mlimani nalo limekuwa chini ya utafiti kwa muda mrefu. Serikali inasemaje juu ya uwezekano wa kuwapatia wananchi kuchimba kwa leseni za wachimbaji wadogo wadogo?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Augustino Manyanda Masele, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu kuwamilikisha wananchi kwenye eneo hilo, nieleze tu kwamba Mheshimiwa Mbunge anafahamu wananchi wa Nyakafuru ndiyo wao wako pale wanaendelea na shughuli. Kwa kuwa wanaendelea na shughuli pale na kwa maelekezo tuliyopewa kazi yetu ni kuwasaidia wachimbaji wadogo, wale ambao hawako rasmi tuwarasimishe ili waweze kupata vibali halisi waweze kuchimba kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu eneo la Nakanegere, eneo hili lote linamilikiwa na kampuni moja na lenyewe utaratibu wake utakuwa kama ule wa Nyakafuru.

Name

Martha Jachi Umbulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AUGUSTINO M. MASELE aliuliza:- Je, ni lini mgodi utafunguliwa katika eneo la Nyakafuru Wilayani Mbogwe baada ya utafiti kuchukua muda mrefu kwenye eneo hilo?

Supplementary Question 2

MHE. MARTHA J. UMBULLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuniona. Kama lilivyo suala la madini katika Jimbo la Mbogwe, Mkoa wetu wa Manyara maeneo mengi yana madini kulingana na utafiti uliofanyika. Hivi sasa uchimbaji huo unafanywa kiholela na sina hakika kama Serikali ina mkakati wowote ama ina taarifa na suala hilo. Je, Serikali sasa iko tayari kutupa takwimu ama hali halisi ya madini yaliyoko katika Mkoa wetu, Wilaya za Mbulu, Simanjiro na Kiteto?

Name

Doto Mashaka Biteko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukombe

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. DOTO M. BITEKO):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Felister Bura, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Bura atakumbuka kwamba wakati tunawasilisha bajeti yetu pamoja mambo mengine tulitoa machapisho na majarida mbalimbali ambayo ndani yake yalikuwa yanatoa takwimu kwa ujumla kwenye sekta ya madini kwa kila Mkoa, Wilaya na maeneo mbalimbali. Naamini Mheshimiwa Bura akienda kukapitia kale kakijitabu atapata taarifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini hili jambo lingine ambalo ameeleza juu ya wananchi kuchimba kwenye maeneo mbalimbali kwenye Mkoa Manyara. Niseme kwamba Serikali inazo taarifa za wachimbaji wadogo kuvumbua. Mara ugunduzi unapotokea, kazi yetu ya kwanza ni kupeleka usimamizi ili kudhibiti usalama lakini vilevile kudhibiti mapato ya Serikali. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Bura ugunduzi wowote unaotokea katika Mkoa wa Manyara tunafahamu na tayari kuna usimamizi ambao unafanywa na Ofisi zetu za Madini kwenye Kanda pamoja na Mikoa.