Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwantum Dau Haji

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MWANTUMU DAU HAJI aliuliza:- Kumekuwa na ucheleweshaji wa mishahara kwa watumishi wa umma:- Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo hilo?

Supplementary Question 1

MHE. MWANTUMU DAU HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Namshukuru Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri aliyoyatoa hivi sasa. Kwa kuwa hakuna ucheleweshwaji wa mishahara, napenda kuuliza maswali yangu mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Serikali inasema nini kuhusu uongezaji wa mishahara kwa watumishi hao?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Serikali inasema nini kuhusu upandishaji wa madaraja mbalimbali kwa watumishi wa umma?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mwantumu Dau Haji, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza ameuliza Serikali inasema nini kuhusu uwekezaji wa mishahara ya wafanyakazi. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba mshahara ni mali halali ya mfanyakazi mwenyewe hivyo kuhusu uwekezaji ni mfanyakazi mwenyewe anaamua mshahara wake nini aufanyie, akitaka kuuwekeza wote yuko huru kufanya hivyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu upandishwaji wa madaraja, Serikali yetu siku zote imekuwa ikiwatendea haki wafanyakazi wetu kwenye upandishaji wa madaraja na kila mwaka wafanyakazi hupandishwa madaraja.