Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silafu Jumbe Maufi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:- Serikali inafahamu kuwa michezo ni afya na ni ajira pia, lakini mikoa kadhaa hapa nchini ina viwanja visivyokidhi hadhi ya kitaifa na kimataifa na hata kasi ya kuibua vipaji vipya imedorora katika Mikoa ya Rukwa, Tabora, Iringa, Kigoma na kadhalika. Je, Serikali sasa haioni umuhimu wa kushirikiana na wamiliki wa viwanja hivyo kuvikarabati na kuviboresha kufikia hadhi stahiki?

Supplementary Question 1

MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Naibu Waziri katika swali langu la msingi, mimi kama Mheshimiwa Mbunge wa Bunge hili la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania na bahati nzuri kwa rehema zake Mwenyezi Mungu, jana tu tumepitisha sheria ya kuiwezesha Serikali kuingia ubia na mashirika binafsi katika maendeleo ya wananchi wetu wa Tanzania.
Je, kwa nini Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa wao kuingia ubia na sekta hii binafsi yenye viwanja hivi vinavyomikiwa na hawa watu ambao ni viwanja vyao vya halali? Kwani wamevijenga kwa muda mrefu na wanasuasua katika kuviendeleza viwanja hivi ili waweze kuingia ubia waweze kuvikarabati na watoto wetu wapate afya njema na waweze kupata ajira katika maendeleo yao.
Mheshimiwa Spika, naomba Serikali inipatie majibu kwa hilo swali dogo ambalo nimeliuliza kwa wakati huu. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTHONY P. MAVUNDE K.n.y. WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO): Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua kwamba moja kati ya mkakati wa kuendeleza michezo mbalimbali nchini ni pamoja na kuwa na miundombinu rafiki ya kuwafanya washiriki wa mchezo husika kuweza kushiriki kwa ufanisi mkubwa. Ni dhamira ya Serikali kuendeleza viwanja vingi vya michezo hapa nchini.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ushauri uliotolewa na Mheshimiwa Mbunge wa kushirikisha sekta binafsi na wadau mbalimbali, sisi kama Serikali tuko tayari. Lengo letu ni kujenga mazingira rafiki ya kufanya michezo mbalimbali iliyo na miundombinu ambayo itatoa fursa kwa washiriki wake kushiriki kikamilifu.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:- Serikali inafahamu kuwa michezo ni afya na ni ajira pia, lakini mikoa kadhaa hapa nchini ina viwanja visivyokidhi hadhi ya kitaifa na kimataifa na hata kasi ya kuibua vipaji vipya imedorora katika Mikoa ya Rukwa, Tabora, Iringa, Kigoma na kadhalika. Je, Serikali sasa haioni umuhimu wa kushirikiana na wamiliki wa viwanja hivyo kuvikarabati na kuviboresha kufikia hadhi stahiki?

Supplementary Question 2

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Tatizo la ubovu wa viwanja limekuwa kubwa sana hapa nchini. Sasa Serikali haioni kwamba huu ni wakati sahihi sasa wa kuanzisha Wakala wa Kusimamia Viwanja vya Mpira ili iwe inasimamia ubora wa viwanja vyote vya mpira hapa nchini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, KAZI, VIJANA NA AJIRA (MHE. ANTHONY P. MAVUNDE K.n.y. WAZIRI WA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO): Mheshimiwa Spika, chini ya Wizara pamoja na Shirikisho la Michezo Tanzania kwa maana TFF iko Idara maalum ambayo inasimamia ubora na vigezo vya viwanja ambavyo vitatumiwa katika michezo mbalimbali. Utaratibu uliowekwa ni kwamba iko international standard ambayo inavitaka viwanja mbalimba viwe vina sifa zifuatazo:-
Mheshimiwa Spika, kwa mfano, kwa Kiwanja cha Mpira wa Miguu, kwa mujibu wa international standard kinatakiwa kiwe kati ya mita 100 mpaka mita 110 na upana wake uwe ni mita 64 mpaka mita 75. Kwa hiyo, tunayo Idara chini ya TFF na kwenye Wizara ambayo kazi yao ni kushughulikia viwanja ambavyo vitakuwa ni bora.
Mheshimiwa Spika, pia kwa wazo ambalo ameleta Mheshimiwa, naamini kazi kubwa ambayo tutafanya kama Serikali ni kuboresha Idara zetu za ndani ili ziendelee kufanya utaratibu kuhakikisha kwamba tunakuwa tuna viwanja bora zaidi vya watu kuchezea.