Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SILYVESTRY F. KOKA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha bidhaa za nyama nchini pamoja na mazao mengine yatokanayo na mifugo?

Supplementary Question 1

MHE. SILYVESTRY F. KOKA: Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri ninayo maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika nia njema ya Serikali kurejesha baadhi ya maeneo ya shamba la mitamba la Kibaha kwa wananchi, kuna eneo dogo ambalo wananchi wanalikalia linaitwa maarufu Vingunguti. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari mimi na yeye kwenda kukutana na wananchi ili kuona muafaka kati yao na shamba hili la mitamba?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa machinjio ya kisasa yaliyokuwa yanajengwa pale kwenye Ranchi ya Ruvu ina zaidi ya miaka minne haijaendelea na ujenzi na huku mahitaji ya nyama bora ni makubwa kwa Pwani na Dar es Salaam. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza ujenzi wa machinjio haya hata kwa ubia kati ya wananchi na Serikali?

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza anataka kujua kama niko tayari kwenda Kibaha na nataka kumhakikishia niko tayari kwenda Kibaha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, anataka kujua nini msimamo wa Serikali juu ya machinjio ya kisasa ya pale Ruvu. Ni kweli mradi huu umekawia, lakini kupitia mradi wa uendelezaji wa sekta ya kilimo, Serikali ya Korea imeonesha nia ya kutukopesha dola za Kimarekani takribani milioni 50 ambapo hivi sasa utaratibu Serikalini unaendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na moja ya miradi ambayo itakwenda kunufaika na pesa hizi ni pamoja na machinjio ya kisasa ya Ruvu ambayo haitaishia kaktiak kuwa machinjio tu, tutakuwa na Leather Complex ambayo itakwenda kutengeneza na uchakataji wa ngozi. Pia vilevile tutakuwa tayari kutengeneza bidhaa mbalimbali za ngozi kupitia mradi huu wa machinjio ya pale Ruvu. Ahsante.