Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Wananchi wa Kanda ya Kati ni wakulima wazuri wa zao la alizeti:- Je, Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko kuanzisha Mfuko mahsusi wa uendelezaji wa zao la alizeti?

Supplementary Question 1

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Naibu Waziri kwa kuteuliwa lakini pia nimpongeze kwa majibu mazuri aliyonipatia. Pamoja na majibu hayo mazuri, nina maswali mawili madogo ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, Taifa hili hutumia fedha nyingi sana kuagiza mafuta ya kula ukiachilia mafuta ya petroli, lakini nchi hii ina uwezo wa kuzalisha mafuta ya kutosha ya kula na tukaacha kuagiza mafuta kutoka nje ya nchi. Katika nchi yetu kuna viwanda vingi vinavyokamua mafuta kwa mfano, Kiwanda cha Mount Meru ambacho kina uwezo wa kukamua mafuta tani 400,000 lakini kwa sasa wanapata tani 40,000 tu ukiachilia viwanda vingine.
Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha kwamba Mikoa ya Dodoma, Singida na Manyara wanawekwa kwenye mkakati maalum wa kuzalisha mazao ya mafuta na hata Mkoa wa Kigoma unaozalisha mafuta ya mawese, kwamba sasa mkakati uwekwe kwa kupata mbegu bora kwa ajili ya kuzalisha mazao yanayozalisha mafuta, ni mkakati gani umewekwa na Serikali? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, sisi wananchi wa Dodoma ni wakulima wazuri sana wa zabibu na tunazalisha mara mbili kwa mwaka lakini hatuna soko. Zabibu zinaoza mashambani kwa sababu wakulima wamekosa masoko. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba zabibu zote zinazozalishwa na wakulima zinapata soko? (Makofi)

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi ya kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bura, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza ni kutaka kujua mkakati wa Serikali kwa ajili ya kuweza kuzalisha mazao ya mbegu ya mafuta hapa nchini ili kumaliza tatizo la mafuta hapa nchini ili kuokoa fedha za kigeni. Serikali ya Awamu ya Tano ikiongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 4 Juni, 2018 ilizindua Programu Maalum ya Kuendeleza Kilimo, kwa Kiluguru tunaita ASDP II ambapo lengo lake ni kuongeza uzalishaji na tija kwa ajili ya mazao ya kilimo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sambamba na mpango huo Mheshimiwa Waziri Mkuu alianza utekelezaji huo tukaenda Mkoa wa Kigoma kwa ajili ya kuzindua na kuendeleza kilimo cha mchikichi, ikafuatiwa na kikao cha wadau kilichofanyika tarehe 24/05 pale Morogoro kwa maana ya kampuni yetu ya uzalishaji mbegu ya ASA, Kampuni ya Utafiti wa Mbegu (TARI) pamoja na Kampuni ya Udhibiti wa Mbegu (TOSCI) wamepanga mikakati na tumekubaliana kama Serikali kuanza kufufua zao la mchikichi kwa ajili ya kuzalisha ndani ya miaka minne miche milioni 20 ili kumaliza tatizo hilo sambamba na kuongeza mbegu bora katika zao la alizeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu zabibu, kwanza nimpongeze Mheshmiwa Mbunge kwa kuwatetea watu wake wa Dodoma ambao ni maarufu kwa kilimo cha zabibu hapa nchini lakini ni kweli bei ya wine inayotokana na zabibu ya Tanzania ipo juu kuliko ya wine zinazotoka nje ya nchi. Hii inatokana na sababu ya gharama kubwa za uzalishaji hapa nchini na tija ndogo wanayopata wakulima, wanatumia gharama kubwa lakini wanapata faida ndogo. Serikali tumeliona hilo na kwa sasa tunapitia na wenzetu wa Wizara ya Fedha kuangalia mfumo wa kodi zetu na ushuru ili kupunguza gharama za uzalishaji kuwezesha wine hii kuuzwa kwa bei nafuu ili soko liwe la uhakika. (Makofi)

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Wananchi wa Kanda ya Kati ni wakulima wazuri wa zao la alizeti:- Je, Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko kuanzisha Mfuko mahsusi wa uendelezaji wa zao la alizeti?

Supplementary Question 2

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Mazingira ya Mkoa wa Simiyu yanafanana na mazingira ya Mikoa ya Kati kwa zao la alizeti lakini wakulima wa Simiyu wamekuwa wakilima zao hili kwa kubahatisha mbegu za alizeti zisizo na tija ukilinganisha na Mikoa ya Kati. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuleta mbegu zenye tija ikiwemo na kutoa elimu kwa wakulima wa Mkoa wa Simiyu?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa majibu yangu ya swali la msingi nilizungumzia mikakati iliyopo kwa Shirika letu la ASA, TOSKI na TARI. Mbegu zipo na nawaelekeza watu wa ASA wapeleke mbegu kule kwa Mheshimiwa Mbunge ili mbegu hizi zipatikane kwa gharama nafuu kwa hii mbegu aina ya Record. Pia kuna makampuni binafsi ambayo yamethibitishwa na Taasisi yetu ya Kudhibiti Ubora ya TOSCI yanauza mbegu kihalali nayo nayaomba yapeleke mbegu katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge ili wananchi wapate mbegu kwa urahisi zaidi.

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Wananchi wa Kanda ya Kati ni wakulima wazuri wa zao la alizeti:- Je, Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko kuanzisha Mfuko mahsusi wa uendelezaji wa zao la alizeti?

Supplementary Question 3

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi wa Mkoa wa Singida ni wakulima wazuri wa zao la alizeti, je, Serikali haioni umefika wakati sasa wa kulifanya zao hili la alizeti kuwa ni zao la kimkakati ili kuongeza tija na kipato kwa wananchi? (Makofi)

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, zao la alizeti ni moja ya zao la kimkakati. Kama unavyofahamu kipaumbele cha kwanza cha Serikali ni mazao ya chakula na alizeti ni moja ya mazao ya chakula. Kwa hiyo, lipo kwenye zao la kimkakati na ndiyo maana lipo chini ya Bodi ya Mazao Mchanganyiko.

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FELISTER A. BURA aliuliza:- Wananchi wa Kanda ya Kati ni wakulima wazuri wa zao la alizeti:- Je, Serikali haioni ni muda muafaka sasa wa Bodi ya Mazao Mchanganyiko kuanzisha Mfuko mahsusi wa uendelezaji wa zao la alizeti?

Supplementary Question 4

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Wanasayansi wamefanya utafiti na wanasema kwamba vyombo vya plastiki vikikutana na joto kali vinasababisha madhara makubwa sana kwa afya ya binadamu kwa sababu yanatoa kemikali fulani inayoitwa BPA. Je, Serikali inalitambua hili na kama inalitambua inachukua hatua gani kuwasaidia wakulima hawa wa alizeti ambao wanauza mafuta yao barabarani na yanapigwa jua kali sana? Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba wanahifadhi mafuta hayo ipasavyo ili wananchi wetu wasipate madhara hasa ya kansa?

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO (MHE. OMARY T. MGUMBA):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli bidhaa za plastiki kuwekea vyakula hasa vya moto kuna madhara yake lakini kwa haya ya baridi bado tunafanyia utafiti katika Serikali na tumeshaagiza taasisi zetu za utafiti wafanye utafiti kujua madhara yanayopatikana kwa mafuta kuwekwa kwenye vyombo vya plastiki ili wakituletea majibu tutakuja kumpa Mheshimiwa Mbunge.