Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi kati ya Mbuga za Wanyama Selous – Kilwa na wananchi wanaoishi karibu na mbuga hiyo umezidi kuwa mkubwa kwa sababu mipaka halali haijulikani. Kwa mfano, mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu, mwaka 2010 mpaka huo ulisogezwa kufikia Bwawa la Kihurumila katika Kijiji cha Kikulyungu:- a) Je, Serikali iko tayari kuhakiki eneo hilo ili kuondoa mgogoro mkubwa uliopo kati ya Wanakijiji wa Kihurumila na Mbuga? b) Je, Serikali iko tayari kutatua mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kilwa na Mbuga.

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nianze kumshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri katika Bunge lililopita aliniahidi kuja Lindi kutembelea maeneo haya na kwa kweli alikuja na aliambatana na viongozi wa Mkoa na Wilaya katika kutembelea na kujionea maeneo haya ya mgogoro wa ardhi. Napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la kwanza, mwaka 1974 mpaka huu ulikuwa Mto Matandu lakini mwaka 2010 katika marejeo ya mpaka, mpaka huu ulikuwa katika Bwawa la Kihurumila, Kijiji cha Kikulyungu. Napenda kujua ni kwa nini Serikali iliamua kuhamisha mpaka huu kutoka katika Mto Matandu na ukafika katika Bwawa hili la Kihurumila?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili napenda kujua sasa baada ya ziara yake na kujionea mwenyewe, nini sasa Serikali itafanya katika kumaliza mgogoro huu wa mipaka kati ya Serikali kupitia Selous na Serikali ya Wilaya ya Kilwa lakini na mpaka wa Wilaya ya Liwale na Selous?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nichukue nafasi hii kuwashukuru Wabunge wote kwa maombi makubwa ambayo mmekuwa mkiyatoa kwa sababu siku ambapo tulikuwa tutatue hili tatizo ndiyo siku ambayo Mheshimiwa Waziri alipata ajali na hivyo ikalazimika kwamba tukatishe ile ziara na tuende kumhudumia Mheshimiwa Waziri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nilitaarifu Bunge lako tukufu kwamba Mheshimiwa Waziri jana ametolewa hospitalini na sasa yupo nyumbani, kwa hiyo, tunawashukuru sana kwa maombi yenu. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge, kweli kwa muda mrefu amekuwa akilifuatilia tatizo hili na sisi kama Serikali ndiyo maana tuliamua kwamba hili tatizo sasa lifike mahali lifikie mwisho. Naomba nijibu maswali yake mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, la kwanza, si kweli kwamba Serikali ilisogeza mpaka ilitokana tu na tafsiri. Tafsiri ya mpaka iliyoandikwa kwenye GN ya mwaka 1974 ndiyo wataalam walipotafsiri wakaona mpaka unapita wapi. Hata hivyo mwaka 2010 wananchi hawakuridhika ndiyo maana tukaamua kwamba kwa sasa hivi tufanye tena upya kwa kutumia wataalam.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimjulishe Mheshimiwa Mbunge kwamba kutokana na hiyo ziara na maagizo ambayo tulikuwa tumeshayatoa tumeamua kwamba Kamati rasmi kutoka Wizara ya Ardhi iko tayari inapitia mpaka wa Ruangwa na Kilwa ili kurekebisha ile mipaka na baada ya hapo tarehe 18 Septemba wataenda katika Kijiji cha Kikulyungu ambapo wataangalia mpaka wa Kijiji cha Kikulyungu pamoja na mpaka wa Selous. Kwa hiyo, ni imani yangu kwamba baada ya hapo tatizo hili litakuwa limekwisha kwa sababu wananchi wameahidi kushirikiana vizuri kabisa na hiyo Kamati. Naomba tu ushirikiano na Mheshimiwa Mbunge awe na subira.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi kati ya Mbuga za Wanyama Selous – Kilwa na wananchi wanaoishi karibu na mbuga hiyo umezidi kuwa mkubwa kwa sababu mipaka halali haijulikani. Kwa mfano, mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu, mwaka 2010 mpaka huo ulisogezwa kufikia Bwawa la Kihurumila katika Kijiji cha Kikulyungu:- a) Je, Serikali iko tayari kuhakiki eneo hilo ili kuondoa mgogoro mkubwa uliopo kati ya Wanakijiji wa Kihurumila na Mbuga? b) Je, Serikali iko tayari kutatua mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kilwa na Mbuga.

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kunipa nafasi. Niipongeze Serikali kwanza kwa kazi nzuri iliyofanyika kwenye mapori ya hifadhi ya wanyamapori Kimisi, Burigi na Biharamlo kwa kuondoa mifugo na sasa hifadhi hizo zimepanda hadhi kuwa National Parks. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuna tatizo hususani kwa Maafisa ya Wanyamapori ambao siyo waaminifu ambao sasa wanaenda vijijini na kuswaga mifugo kuingiza kwenye pori la hifadhi kwa lengo la kutengeneza mazingira ya rushwa. Serikali inachukua hatua gani kwa maafisa hawa ambao sio waamini? Hili limetokea Ngara na ushahidi upo. (Makofi)

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gashaza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza na ni kweli kabisa kwamba Serikali imepandisha mapori matano katika eneo lile kuwa sasa ni Hifadhi ya Taifa. Naomba nitumie nafasi hii kumjulisha tu kwamba baada ya kupandisha hayo mapori sasa hakuna shughuli yoyote ya kibinadamu au uwindaji wowote unaoruhusiwa katika maeneo hayo kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi za Taifa. Kwa hiyo naomba tu tuendelee kushirikiana na kuhakikisha kwamba hayo hayatokei.
Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la kwamba wafanyakazi wetu wanakamata mifugo na kuiingiza kwenye hifadhi halafu ndiyo wanaomba rushwa, naomba nitumie fursa hii kusema kwamba kwanza wafanyakazi hawaruhusiwi kufanya hivyo na pale ambapo inabainika wafanyakazi wetu wanakiuka maadili ya kiutumishi basi tunaomba taarifa wananchi watusaidie kututajia kwamba kuna mfanyakazi huyu na huyu anaomba rushwa nasi tutachukua hatua zinazostahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, katika maeneo yote ya mapori nchini hairuhusiwi mifugo wala kilimo kuingia katika maeneo hayo. Kwa hiyo, nitumie nafasi hii kuwaombeni hakuna mwananchi yeyote anayeruhusiwa kuingiza mifugo ikiingizwa itataifishwa na hivyo ndiyo sheria inavyoelekeza. Kwa hiyo, naomba ushirikiano na wananchi wote.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi kati ya Mbuga za Wanyama Selous – Kilwa na wananchi wanaoishi karibu na mbuga hiyo umezidi kuwa mkubwa kwa sababu mipaka halali haijulikani. Kwa mfano, mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu, mwaka 2010 mpaka huo ulisogezwa kufikia Bwawa la Kihurumila katika Kijiji cha Kikulyungu:- a) Je, Serikali iko tayari kuhakiki eneo hilo ili kuondoa mgogoro mkubwa uliopo kati ya Wanakijiji wa Kihurumila na Mbuga? b) Je, Serikali iko tayari kutatua mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kilwa na Mbuga.

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kuna mgogoro unataka kufukuta katika Jimbo langu kwenye Kata ya Nyatwali inayojumuisha wakazi zaidi ya 11,000. Lile sio Pori la Akiba ni maeneo yao ambayo wanaishi, inasemekana Serikali inataka kuwahamisha haijawashirikisha, hawajui wanaenda wapi na wanalipwa nini. Nini tamko la Serikali kuondoa hili tatizo kwa sababu mna migogoro mingi msitengeneze migogoro mingine na Bunda hatutakubali.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ester Bulaya, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nampongeza kwa jinsi ambavyo anawateea wananchi wake. Niseme tu kwamba mpaka sasa hivi hatuna taarifa rasmi kwamba tunataka kuihamisha hiyo Kata ya Nyatwali. Kwa hiyo, kama kuna fununu za namna hiyo lazima zitazingatia taratibu na sheria zote zilizopo kuhakikisha kwamba wananchi wanashirikishwa kikamilifu na viongozi wote wanashirikishwa ndipo hapo wananchi wanaweza kuhamishwa. Kama wananchi watakuwa waliingia kinyume na taratibu hapo ndiyo lazima nguvu zitatumika lakini kama siyo hivyo nikuhakikishie tu kwamba wananchi watashirikishwa vizuri kabisa ili kuhakikisha kwamba sheria inazingatiwa.

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi kati ya Mbuga za Wanyama Selous – Kilwa na wananchi wanaoishi karibu na mbuga hiyo umezidi kuwa mkubwa kwa sababu mipaka halali haijulikani. Kwa mfano, mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu, mwaka 2010 mpaka huo ulisogezwa kufikia Bwawa la Kihurumila katika Kijiji cha Kikulyungu:- a) Je, Serikali iko tayari kuhakiki eneo hilo ili kuondoa mgogoro mkubwa uliopo kati ya Wanakijiji wa Kihurumila na Mbuga? b) Je, Serikali iko tayari kutatua mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kilwa na Mbuga.

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwa vile sasa kuna mgogoro mwingine umeanza kuzuka kati ya wananchi na wanyama waharibifu kama tembo na viboko. Je, Serikali inasaidiaje wananchi ambao wanaishi kando kando ya hifadhi hizi pamoja na ziwa kuepukana na mgogoro huu ambapo sasa tembo wanajeruhi watu na kuharibu mali za watu pamoja na kuuwa watu lakini viboko wanafanya uharibifu mkubwa sana wa mazao ya wananchi. Serikali ina mpango gani sasa kuwasaidia wananchi hawa kuondokana na mgogoro huu?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la kaka yangu Mheshimiwa Dkt. Raphael Chegeni, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kumekuwa na changamoto ya wanyama wakali na waharibifu katika maeneo mengi nchini lakini Serikali imekuwa ikichukua hatua mbalimbali za kuhakikisha kwamba inawaelimisha wananchi ipasavyo kuhakikisha kwamba wanakabiliana na hao wanyamapori pamoja na kuweka maafisa katika kila wilaya kuhakikisha kwamba wanashirikiana na wananchi na wale wa vijiji kuhakikisha kwamba wanawadhibiti hao wanyama wakali na waharibifu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia kwa kutumia Kikosi chetu cha Kupambana na Ujangili (KDU) na katika maeneo yale ambayo imeoneka kwamba wanyama wale wamezidi tumekuwa tukichukua hatua za kufungua kituo katika hilo eneo ili kuhakikisha askari wetu wanakuwepo hapo kwa muda mrefu na ili kuwadhibiti hao wanyama wakali na waharibifu. Kwa hiyo, naomba tu tuendelee kushirikiana tuhakikishe kwamba tunapambana na hao wanyama wakali na waharibifu.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza:- Mgogoro wa ardhi kati ya Mbuga za Wanyama Selous – Kilwa na wananchi wanaoishi karibu na mbuga hiyo umezidi kuwa mkubwa kwa sababu mipaka halali haijulikani. Kwa mfano, mwaka 1974 mpaka halali ulikuwa Mto Matandu, mwaka 2010 mpaka huo ulisogezwa kufikia Bwawa la Kihurumila katika Kijiji cha Kikulyungu:- a) Je, Serikali iko tayari kuhakiki eneo hilo ili kuondoa mgogoro mkubwa uliopo kati ya Wanakijiji wa Kihurumila na Mbuga? b) Je, Serikali iko tayari kutatua mgogoro uliopo kati ya wananchi wa Kilwa na Mbuga.

Supplementary Question 5

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Wakati katika baadhi ya maeneo kumekuwa na migogoro baina ya Serikali na hayo maeneo ya mbuga za wanyama, lakini kuna maeneo mengi ya utalii kwa mfano maeneo ya kihistoria kama kule Iringa Isimila kuna maeneo yana maporomoko ya maji ambayo pia ni kivutio cha utalii na kuna maeneo yana misitu na ndege wazuri ambapo ni vivutio vya utalii. Je, Serikali haioni sasa ni wakati muafaka wa kuwekeza nguvu kutangaza vivutio hivyo ili walao kupunguza pressure huko kwenye mbuga za wanyama?

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa nchi yetu imebahatika kuwa na maeneo mengi ya vivutio vya utalii ikiwemo misitu, malikale, maeneo ya historia na mambo mengine. Hivi sasa Serikali imetengeneza mkakati mkubwa wa kuhakikisha kwamba vivutio vyote vinatangazwa ipasavyo ili kuhakikisha utalii wa ndani na utalii wa nje unaongezeka katika maeneo yote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pia tumechukua hatua kuhakikisha kwamba Mikoa ya Kusini tunapanua utalii ili kupunguza pressure kubwa upande wa Kaskazini. Tunaamini jitihada hizi zitazaa matunda makubwa na kuhakikisha kwamba vivutio vyote vinafahamika na watalii wengi wanaongezeka zaidi nchini.