Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. GIMBI DOTTO MASABA) aliuliza:- Tanzania inakabiliwa na tishio la mabadiliko ya tabianchi linalosababishwa na uchafuzi wa mazingira, hasa wa viwandani:- Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wamiliki wa viwanda wanaokiuka Sheria za Mazingira?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru, nina maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, moja ya sababu inayosababisha mabadiliko ya tabianchi ni uharibifu wa mazingira kwa ukataji miti. Kwa kuwa hapa nchini ukataji miti uko kwa juu sana kwa sababu watu wengi tunategemea nishati ya kuni au mkaa kwa ajili ya mapishi nyumbani na shughuli nyinginezo. Serikali ina mkakati gani kuhakikisha kwamba huu uharibifu wa mazingira kwa kutumia nishati hizi ambazo zinapunguza idadi ya miti nchini inakuwa imepunguzwa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, majibu ya Serikali inaonesha kwamba wale wachafuzi wa mazingira kupitia viwanda hutozwa faini au baadhi kufungiwa. Serikali haioni kwamba inafaa iwe na mikakati mahsusi ya kudhibiti viwanda hivi kuangalia miundombinu yake kabla haijaanza kazi kwamba haitakuwa inaharibu mazingira?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwa nishati mbadala na sisi tumekuwa tukisisitiza na tumeanza mkakati huo na tumeshirikisha na ndugu zetu wa TFS sasa wanatoa miti ambayo inahimili ukame na wanatenga maeneo maalum kwa ajili ya kuvunwa na maeneo maalum kwa ajili ya hifadhi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia swali la pili namna ya kudhibiti wamiliki wa viwanda, kama ambavyo nimeeleza kwenye majibu yangu ya swali la msingi kwamba tutaendelea kuzingatia sheria ileile. Niwaombe wamiliki wa viwanda wajue kabisa kwamba wanao wajibu wa kuyatunza mazingira na wanao wajibu wa ku-treat yale maji ambayo yanaleta zile taka hatarishi. Ahsante sana.

Name

Ruth Hiyob Mollel

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. GIMBI DOTTO MASABA) aliuliza:- Tanzania inakabiliwa na tishio la mabadiliko ya tabianchi linalosababishwa na uchafuzi wa mazingira, hasa wa viwandani:- Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wamiliki wa viwanda wanaokiuka Sheria za Mazingira?

Supplementary Question 2

MHE. RUTH H. MOLLEL: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na uchafuzi wa viwanda, vilevile mifuko ya plastick ni source mbaya sana ambayo inachafua mazingira. Je, kwa nini Ofisi ya Makamu wa Rais haitumii ule Mfuko wa Technological Transfer and Adaptation Fund kuwawezesha hao wenye viwanda wabadilishe teknolojia waweze kuzalisha mifuko ambayo ni rafiki kwa mazingira?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa mifuko ya plastick imekuwa ikileta uchafuzi wa mazingira kwa kiasi kikubwa sana. Niseme tu kwamba, Serikali tayari ilishazuia kutoa leseni mpya kwa wazalishaji ama viwanda vipya vinavyokuja kwa ajili ya mifuko ya plastic. Pia, tumeendelea ku-encourage wawekezaji wa viwanda vya mifuko rafiki ili waweze kuwekeza na hatimaye huko mbele tuweze ku-ban kabisa mifuko ya plastic.

Name

Yussuf Salim Hussein

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Chambani

Primary Question

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. GIMBI DOTTO MASABA) aliuliza:- Tanzania inakabiliwa na tishio la mabadiliko ya tabianchi linalosababishwa na uchafuzi wa mazingira, hasa wa viwandani:- Je, Serikali inatoa kauli gani kwa wamiliki wa viwanda wanaokiuka Sheria za Mazingira?

Supplementary Question 3

MHE. YUSSUF SALIM HUSSEIN: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yake amesema kwamba wale wanaokiuka taratibu hizi sheria inawapa mamlaka ya kuwafungia ama kuwapiga faini, zote hizo ni force approach. Dunia ya leo ni dunia shirikishi, Wizara ina mpango gani wa kuwashirikisha na kuwaelimisha wenye viwanda na kushirikiana nao kuona tatizo hili linamalizwa kabisa badala ya kutumia nguvu?

Name

Mussa Ramadhani Sima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS (MUUNGANO NA MAZINGIRA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza ni kwamba kabla ya mwekezaji kuanza kuwekeza hatua ya kwanza sisi huwa tunatoa elimu. Mpaka afikie hatua ya kupata certificate ya EIA, maana yake amekidhi vigezo vyote. Kinachofuata akikiuka utaratibu ambao tumeuweka ni lazima tumpige faini.