Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. AIDA J. KHENANI aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kuziba nafasi zilizoachwa wazi na watumishi waliokumbwa na sakata la vyeti fake?

Supplementary Question 1

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Spika, kulingana na majibu ya Waziri nafikiri anajua kwamba kabla ya mchakato wa kuondoa watu waliokuwa wanajulikana kama wenye vyeti feki au vya kugushi, kulikuwa na upungufu mkubwa wa watumishi kwenye sekta mbalimbali zikiwemo sekta za elimu, kilimo na afya. Sasa kwa kuwa amejibu kwa data nina imani anajua upungufu mkubwa, tungependa alieleze Bunge lako; kwa kuwa kulikuwa na upungufu na wakaongoza tena upungufu ukawa mkubwa zaidi na mmeajiri kiasi hiki alichokisema, tunaomba kujua, mpaka sasa kuna upungufu wa watumishi kiasi gani?
Swali la pili, Rais wa kwanza wa Zanzibar aliwahi kusema tumesoma hatukujua, tumejifunza tumetambua. Serikali ya Tanzania inathamini zaidi vyeti kuliko kuangalia taaluma na kazi ambazo watu wamefanya. Baada ya kutumbua kuna watu walikuwa wamebakiza mwaka mmoja kustaafu. Ninapenda kujua Serikali imejipangaje kwa kuangalia mchango ambao waliutoa, kwa sababu wamefundisha watu wengine ni Wabunge, wengine ni Mawaziri… (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ninapenda kujua kwamba mna utaratibu gani wa kuweza kuwalipa watumishi wale ambao walitumikia Taifa hili kwa uaminifu mkubwa? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Niwakumbushe tu Waheshimiwa Wabunge wenzangu, tunapowauliza maswali Mawaziri hatutakiwi kuwataka takwimu maana hatutembei na takwimu kichwani.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali lake la pili, nadhani hili swali humu ndani limeulizwa tena na tena na wanasheria wakafafanua. Maelezo yako hivi, mwajiri alikuajiri wewe akiamini kwamba vyeti ulivyompa ni vyeti sahihi ndiyo maana ukaingia naye mkataba. Kile kitendo tu cha mwajiri kubaini kwamba ulimdanganya umepeleka cheti feki, Waingereza wanasema ina-nullify mkataba wako, mkataba wako unakuwa null and void, unakuwa umejifuta kwa sababu upande mmoja umewasilisha taarifa ambazo sizo.
Kwa hiyo hapa ndani hatujajipanga kumlipa mtu ambaye mkataba wake ni fake.