Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD (K.n.y MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Minara mingi ya simu imejengwa katika makazi ya watu na minara hiyo inatumia mionzi hatari kwa maisha ya binadamu. Je, Serikali inaliangaliaje suala hilo?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA KOMBO HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. pamoja na jibu la Mheshimiwa Waziri lakini zipo tafiti kadhaa na nyingi ambazo kimsingi zinaonesha kwamba bado kuna madhara makubwa ya watu kuumwa na kichwa na hata kupoteza kumbukumbu kutokana na mionzi inayotokana na minara hii ya simu.
Je, Serikali haioni kwamba kuna haja hasa ya kufanya tafiti za kina zaidi ili kubaini kwamba madhara haya yapo na namna gani Serikali itatumia njia ili kuyaondoa madhara hayo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, minara hii imejengwa na imo ndani ya Halmashauri, sasa kimsingi kuna malalamiko makubwa kwa wananchi ambao wamo ndani ya Halmashauri hizo ambazo minara hii imejengwa kwamba hawafaidiki na uwepo wa minara hii ingawa minara hii ipo kibiashara. Je, Serikali haioni kwamba kuna haja sasa kuandaa utaratibu maalum ili kuona kwamba wananchi na Halmashauri ambazo minara hii ipo zinafaidika? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI UCHUKUZI NA MAWASIALIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa tafiti zilizofanyika na Umoja wa Mawasiliano Duniani (ITU) kama nilivyoeleza katika majibu yangu ya msingi siyo kwamba madhara hakuna kabisa, madhara yapo na hatua mbalimbali zimekuwa zikichukuliwa na makampuni ya simu kwa kuzungushia uzio eneo ambalo wamefunga mnara. Katika kufanya hivyo tunaamini kwa ule upungufu madhara wa mara 1,000 kwa kila mita moja kutoka kwenye mnara hakuna mtu anayeweza kudhurika. Hayo madhara mengine yanayotokana na mtu kuumwa kichwa ni yale ambayo siyo ajabu inawezekana hayatokani na matatizo ya mnara kwa mujibu wa tafiti zilizofanywa kimataifa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa swali lake la pili ni kweli kwamba kumekuwa na changamoto ya wale ambao minara imefungwa kwenye maeneo yao na kutopata chochote kutokana na hilo na hilo limekuwa likishughulikiwa. Tumekuwa tukipata changamoto kama Wizara kwamba tunapowapa kazi wale watoa huduma labda Tigo, Vodacom, Airtel na kadhalika wanakwenda kwanza kuongea na wananchi kule vijijini. Kwa hiyo, wakishaongea nao wananunua maeneo yao kwa hiyo mwananchi wa kijijini kwanza anakuwa anapokea rent, lakini kunakuwa na tozo ya Halmashauri ambayo huwa inatoa kutokana na vikao walivyokaa Madiwani husika.
Kwa hiyo, hilo linakuwa ni gumu sana sisi kama Serikali kuendelea kuliingilia lakini nimuahidi Mheshimiwa Mbunge na Waheshimiwa Wabunge kwamba tunaendelea kulifuatilia kuhakikisha kwamba Serikali kupitia Halmashauri inapata tozo ambazo ni stahiki. (Makofi)

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD (K.n.y MHE. MGENI JADI KADIKA) aliuliza:- Minara mingi ya simu imejengwa katika makazi ya watu na minara hiyo inatumia mionzi hatari kwa maisha ya binadamu. Je, Serikali inaliangaliaje suala hilo?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue nafasi hii nimpongeze Naibu Waziri kwa kazi nzuri ambazo anazifanya. Kwa kuwa wananchi wa Kilolo bado hawajaanza kupata athari yoyote ya minara hii sasa naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa muda mrefu nimekuwa nikiulizia swali la kupata mawasiliano ambayo hayapo kabisa katika vijiji vya Imalutwa, Mazombe, Isele, Kising’a, Mahenge, Maganailindi na Ilambo. Je, Serikali sasa safari hii itakuwa tayari hasa Mheshimiwa Waziri na ulitoa ahadi kwamba utafika ili wananchi hawa waweze kupata mawasiliano ili waendane na sera ya viwanda kwenye nchi yao? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI NA MAWASIALIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Venance kwa jinsi anavyofuatilia sana suala la wananchi wake kupata mawasiliano katika shughuli zao, kwa kweli amefuatilia sana na katika awamu hii ambapo tumetenga kata 173 za kupelekewa mawasiliano kuna Kata zake nafikiri tatu ambazo tayari tumeshazitengea kwenda kupata mawasiliano.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuahidi tu kwamba hizo kata nyingine ambazo hazijapatiwa mwisho wa mwezi huu kuna kata nyingine 205 ambazo tunategemea zitaingizwa kwenye mpango wa kupelekewa mawasiliano ya simu. (Makofi)