Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Mchafu Chakoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. AMINA S. MOLLEL) aliuliza:- Baadhi ya mila na tamaduni katika jamii za wafugaji hapa nchini haziwapeleki watoto wa kike shule, badala yake wanawaozesha katika umri mdogo kinyume na ridhaa yao, hivyo kukiuka sheria za nchi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa mila na tamaduni hizo haziwanyimi watoto wa kike haki yao ya kupata elimu?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA M. CHAKOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, sasa nitapenda nikuulize maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Serikali ya Awamu ya Tano ya Chama cha Mapinduzi, chini ya Rais John Pombe Magufuli imedhamiria kwa dhati kabisa kutoa elimu bure kwa watoto wote; na kwa kuwa, wazazi wengi wa jamii ya kifugaji hawajajitokeza kuwaandikisha watoto wao badala yake wanaamua kuanzisha shule zao ama kufungua shule zao na kuwapeleka watoto wao. Napenda kujua sasa je, Serikali mna taarifa na uwepo wa shule hizi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini swali langu la pili, kama Serikali inafahamu uwepo wa hizo shule ni nini sasa mkakati wa kuhakikisha mnazisaidia shule hizo, ili ziweze kufanya vizuri? Ahsante.

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli Serikali ya Awamu ya Tano ilipoingia madarakani ilikuja na mpango wa elimu bure. Lengo ni kuhakikiksha kwamba kila mtoto wa Kitanzania anapata fursa ya kuendelezwa kwa mujibu wa sheria kupitia nyanja ya elimu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na swali lake la msingi ambalo aliuliza kwamba, je, tuna ufahamu wa hizi shule bubu, ambazo naziita shule bubu;-
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi nimuombe sana Mheshimiwa Mbunge kama ana taarifa ya hizi shule basi na sisi atujulishe kwa sababu shule zetu zote za msingi ni shule ambazo zinatambuliwa Kiserikali na zimesajiliwa na Serikali na zinapata ruzuku na sisi tunapeleka walimu. Kama kunakuwa na shule bubu napata shida kuelewa kwamba hizo shule zimesajiliwa wapi? Hao walimu wanawapata wapi na aina ya elimu ambayo wanaitoa ni elimu ya namna gani?
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, mimi nimuombe sana Mheshimiwa Mbunge kama ana taarifa ya hizi shule, basi atujulishe Serikali, ili tuweze kuzitambua. Na kama tukiona kwamba, zina mazingira ambayo na sisi kama Serikali tunaweza kuzichukua, basi tutaweka utaratibu wa kuzirasimisha rasmi.

Name

Khadija Nassir Ali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. AMINA S. MOLLEL) aliuliza:- Baadhi ya mila na tamaduni katika jamii za wafugaji hapa nchini haziwapeleki watoto wa kike shule, badala yake wanawaozesha katika umri mdogo kinyume na ridhaa yao, hivyo kukiuka sheria za nchi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa mila na tamaduni hizo haziwanyimi watoto wa kike haki yao ya kupata elimu?

Supplementary Question 2

MHE. KHADIJA NASSIR ALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.
Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya Serikali kuchukua hatua kali za kuzuia ukeketaji jamii zinazojishughulisha na ukeketaji zimekuja na njia mpya za kuwakeketa watoto wakiwa bado wachanga. Je, Serikali inalifahamu hili na kama inalifahamu ni hatua gani zimechachukuliwa mpaka sasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, mwezi wa sita nilipokuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika pale Arusha liliibuliwa suala la ukeketaji wa watoto wachanga. Baada ya Serikali kubana na kutoa elimu ya kutosha na kwa watoto kujitambua mara nyingi watoto hawa ambao wana umri mkubwa wamekuwa wanatoa taarifa na sisi tumekuwa tunachukua hatua. Sasa kuna baadhi ya wazazi ambao wameendelea na sasa hivi wamehama kutoka kukeketa mabinti ambao umri umekuwa wamehamia katika kukeketa watoto wachanga.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tunalitambua hilo na tumeshatoa maelekezo katika wizara yangu ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto idara kuu ya maendeleo ya jamii kushirikiana na idara kuu ya afya kuweka utaratibu mahususi ambao tutaanza kubaini watoto wote ambao wanakeketwa wakiwa na umri mdogo hususani pale watoto wanapokuwa wanaenda kliniki. (Makofi)

Name

Susan Anselm Jerome Lyimo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA M. CHAKOMA (K.n.y. MHE. AMINA S. MOLLEL) aliuliza:- Baadhi ya mila na tamaduni katika jamii za wafugaji hapa nchini haziwapeleki watoto wa kike shule, badala yake wanawaozesha katika umri mdogo kinyume na ridhaa yao, hivyo kukiuka sheria za nchi. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa mila na tamaduni hizo haziwanyimi watoto wa kike haki yao ya kupata elimu?

Supplementary Question 3

MHE. SUSAN A. J. LYIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Waziri nina amini swali la msingi lilikuwa linahusu watoto kunyimwa haki yao ya kwenda shule kutokana na mila na destruri. Pamoja na mila na desturi sasa hivi au kwa muda mrefu kumezuka tabia ya wazazi hususani wanawake wakitembea na watoto yaani wakiwa na watoto wao wadogo au watoto wa kukodi kwa ajili ya kuombaomba, hali inayopelekea watoto hawa wasiende shule kwa sababu wakiwa na wale watoto maana yake wananchi watawahurumia na kuwapa msaada. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Serikali inajua kwamba kuna hili jambo na kama inajua ina mkakati gani kuhakikisha kwamba wazazi hao hawatumii watoto wao kama chambo cha kupata misaada na watoto hawa waweze kwenda shule kwa sababu bila hivyo watoto hawa wataendelea kuwa nyumbani? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Susan Lyimo ameuliza swali zuri sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika haki za msingi za mtoto ni pamoja na kuendelezwa, kulindwa, kutunzwa na kutotumikishwa kazi nzito. Swali hili ambalo ameliuliza katika maudhuhi yake yote haya haki zote hizi za msingi za mtoto zinavunjwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niwaombe na tumeshatoa maelekezo kwa wataalam wetu ndani ya Wizara, kwanza tumefanya katika haya majiji makubwa sensa ya kubaini watoto wote ambao wanaishi katika mazingira hatarishi na tumebaini kama watoto karibu 7,000. Mpaka sasa hivi tumeweza tuwarudisha watoto zaidi ya 1,000 majumbani kwao kutegemea na nature ya matatizo ambayo tumekutana nao, lakini tunajua database ya watoto ambao tunao.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaendelea kuwasisitiza Maafisa wetu wa Maendeleo ya Jamii na Maafisa Ustawi wa Jamii hususani katika haya majiji makubwa kuhakikisha kwamba hawa wakina mama ambao wana tabia kama hizo ambao watoto hawaendi shule na watoto wanatumikishwa kazi nzito tunaweza kuwabaini na kuchukua hatua za msingi ili kukomesha kabisa matatizo kama haya. (Makofi)