Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Fakharia Shomar Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Kwa sasa kumekuwa na wimbi kubwa la upimaji wa viwanja kwenye Manispaa mbalimbali nchini. • Je, kwa nini wananchi wanalazimishwa kuuza maeneo hayo kwa Manispaa na kulipwa bei ndogo badala ya kufanya zoezi hilo kwa ubia? • Kwa sababu maeneo hayo mengi ni mashamba, je, Serikali haioni kufanya hivyo kunasababisha Watanzania kukosa kazi maana asilimia 75 ni wakulima?

Supplementary Question 1

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri maswali mawili madogo ya nyongeza.
Kwa kuwa kitendo hicho cha kuwachukliwa ardhi wananchi sio kitendo chema, je, Serikali haioni kwamba wananchi hao tayari imewatumbukiza katika dimbwila umaskini?
Swali la pili, kwa kuwa mwananchi huyo ameridhia zoezi la kuchukuliwa ardhi yake pasina ridhaa yake, je, kwa nini Serikali isingelitoa sehemu mbadala ili kuondoa manung’uniko kwa wananchi hao kuona wameporwa ardhi yao?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza anasema kitendo cha kutwaa maeneo ya wananchi pasipo ridhaa yao ni kwamba ni kuwaingiza katika umaskini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, Sheria ina ruhusu eneo likishatangazwa kuwa ni eneo la upangaji miji, Mamlaka za Upangaji kisheria zimeruhusiwa kuyatoa yale maeneo. Hiyo ni alternative ambayo iko kisheria, lakini katika hali halisi ambayo inaendelea sasa na kwenye kanuni ambazo zipo tumesema kwamba unapotaka kutwaa ardhi ya mtu, wananchi wanapaswa kushirikishwa. Kwa hiyo, kile kitendo cha kutwaa ardhi bado sheria inawaruhusu Mamlaka za Upangaji kuitoa ile ardhi na kupanga kile wanachoona inafaa katika utaratibu huo.
Sasa tunasema tunayo hiyo room ya kufanya makubaliano au maelewano na wananchi, lakini Serikali inapotaka kufanya jambo na eneo limeshaanishwa hauwezi tena wewe mwananchi kuzuia shughuli za Serikali zisifanyike. Sasa katika ule utoaji ndio hapa sasa tunasema hekima na busara pia itumike katika kuwaelimisha wale wananchi ili waweze kuelewa lengo na nia njema ya Serikali ni nini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili anaongelea habari ya kwamba Serikali kwamba kwa nini isitoe maeneo mengine ambayo bado hayajaendelezwa ili kuondokana na taratibu hizi. Sasa labda nitoe tu rai kwa Mamlaka za Upangaji Miji. Kwa sababu suala la upangaji miji ni suala ambalo liko chini ya Halmashauri zetu. Kwa hiyo kwa vyovyote vile wanapoandaa mipango yao ile ni master plan waangalie utaratibu mzima namna ya kuukuza ule mji ili uweze kwenda vizuri kutegemeana na mahitaji ya wakati huo. Lakini kikubwa kinachofanyika pale ushirikishwaji hata kama utatwaa eneo ambalo ni la wananchi ni yale makubaliano kwa mfano kama umepanga hapani eneo la biashara au la huduma za jamii maana yake mwananchi atapaswa kupisha. Kama ni biashara mpe nafasi yeye ya kwanza kama anaweza kuendeleza yeye mwenyewe apewe kipaumbele badala ya kumuondoa na kuleta mtu mwingine mpya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na hilo tumekuwa tukilisema sana kwa sababu imekuwa ni kelele, watu wanalalamika. Kwa hiyo narudia kusema pale mnapopanga matumizi ya maeneo yenu, mnapoweka mikakati ya mipango kabambe, lazima mwananchi aliyepo afikiriwe mwanzo kama ni viwanda basi kama yeye ataweza ajenge, hawezi atauza lakini mmilikishe na umpe masharti kwamba hili ni eneo la viwanda utapaswa kujenga kiwanda, hawezi ataingia ubia, hawezi atauza ataondoka.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Kwa sasa kumekuwa na wimbi kubwa la upimaji wa viwanja kwenye Manispaa mbalimbali nchini. • Je, kwa nini wananchi wanalazimishwa kuuza maeneo hayo kwa Manispaa na kulipwa bei ndogo badala ya kufanya zoezi hilo kwa ubia? • Kwa sababu maeneo hayo mengi ni mashamba, je, Serikali haioni kufanya hivyo kunasababisha Watanzania kukosa kazi maana asilimia 75 ni wakulima?

Supplementary Question 2

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi kwanza niipongeze Wizara hii kwa kazi kubwa wanayoifanya chini ya Waziri mwenye dhamana Naibu Waziri na watendaji wote.
Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo hili la ardhi limekuwa na changamoto kubwa hususan katika kutatua migogoro kutokana na uchache wa watumishi kwenye Mabaraza ya Ardhi hususan Mabaraza ya Wilaya. Kwa mfano Wilaya yangu ya Ngara Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi Wilaya anahudumia zaidi ya Wilaya mbili, na hivyo kupelekea kesi kukaa muda mrefu bila kukamilika, na wananchi wanatoka maeneo mbalimbali na kutumia gharama kubwa hata kuweza kukata tamaa.
Ni lini Serikali itaweza uajiri Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi la Wilaya ya Ngara ili kuondoa usumbufu huu atakaekuwa yuko stationed katika Wilaya hiyo ya Ngara?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Gashaza ametaka kujua ni lini Wizara itapanga Mwenyekiti wa Baraza katika eneo lao, napenda tu nitoe taarifa kwamba upangaji wa Wenyeviti wa Mabaraza kutokana na uchache wa Wenyeviti tulionao unapangwa kutegemeana na wingi wa mashauri katika eneo lile. Lakini kwa habari tu nzuri kwenu ni kwamba sasa hivi tayari tumetangaza nafasi 20 tumepewa, kwa ajili ya kuajiri Wenyeviti watakaokwendakatika Mabaraza.
Kwa hiyo, kitakachofanyika ni tathimini kujua ni Wilaya ipi ina mashauri mengi na inahitaji kuongezewa nguvu na Wilaya zipi ambazo zinakwenda kuanzishwa ili kuweza kupewa Wenyeviti kama Wilaya ya Mbulu ambao huwenda wakapata Mwenyekiti kwa sababu ya shughuri hizo. Kwa hiyo, nimtoe wasiwasi tu kwamba tutalifanyia kazi na kuweza kujua kama watahitaji kuongezewa mtu mwingine.

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FAKHARIA SHOMAR KHAMIS aliuliza:- Kwa sasa kumekuwa na wimbi kubwa la upimaji wa viwanja kwenye Manispaa mbalimbali nchini. • Je, kwa nini wananchi wanalazimishwa kuuza maeneo hayo kwa Manispaa na kulipwa bei ndogo badala ya kufanya zoezi hilo kwa ubia? • Kwa sababu maeneo hayo mengi ni mashamba, je, Serikali haioni kufanya hivyo kunasababisha Watanzania kukosa kazi maana asilimia 75 ni wakulima?

Supplementary Question 3

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na mimi naomba nimuulize Naibu Waziri swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa mashamba mengi ya mkonge yalikuwa wanamilikiwa na wakulima wale wahifadhi wa mikonge. Lakini mashamba yale yamekuwa Mashamba pori na wananchi wengi na hasa wa hususa wananchi wa Korogwe wanahangaika mashamba ya kulima na mashamba yale hayaendelezwi. Je, Serikali ina mpango gani kurudisha mashamba haya kwa wananchi wa Korogwe ili nao wapate kulima?

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake anataka kujua ni lini pengine yale mashamba ambayo yamekuwa mashamba pori hayaendelezwi tuweze kuyarejesha pengine kwa wananchi waweze kuyatumia.
Napenda tu nilifahamishe Bunge lako suala la kutambua shamba hili ni shamba pori, halijaendelezwa na limekiuka taratibu jukumu hilo analo Afisa Ardhi Mteule katika Halmashauri husika. Kwa hiyo ni jukumu la Halmashauri husika kuanza kufanya zile hatua za awali za kuweza kuchukua taratibu zote za kisheria, kuweza kuona kwamba huyu mtu amekiuka taratibu zake basi utaratibu wa kumnyang’anya unafuata.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo mimi niwaombe sana kwa sababu tulishasema, ni jukumu la Halmashauri sisi kama Wizara mkishakamilisha kazi yetu ni kumshauri Mheshimiwa Rais kuweza kuyafuta na yanarudi kupangiwa matumizi. Lakini pia kwa nafasi hii nitoe rai mashamba yote yale ambayo yanafutwa na Mheshimiwa Rais, yakirudishwa katika maeneo yetu msiyapangie matumizi ya makazi mashamba yote kwa sababu sasa hivi unajikutakwamba hata pale ambapo panahitaji kuendeleza kilimo watu wanagawana mashamba. Kinachotakiwa eneo lile likisharudishwa lazima pawekewe mpango mzuri wa matumizi. Kama linaendelea kuwa shamba basi tuweze kujua ni mwekezaji yupi atafanya kazi hiyo, au kama mnabadilisha matumizi kwa sababu mengine yanakuwa yameshavamiwa na wananchi basi pia tuwe na utaratibu wa kuwa na akiba ya ardhi kwa baadae, lakini tuwe pia na kutenga maeneo kwa ajili ya uwekezaji, ili tena tusije tukapata shida, Kwa sababu ardhi haiongezeki na watu wanaongezeka. Kwa hiyo ni jukumu la kila Halmashauri kuona namna bora ya kutumia Wizara tupo kwa ajili ya kutoa ushauri, kwa ajili kutoa Wataalam kuweza kufanikisha azma ya Halmashauri.