Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. MARYAM SALUM MSABAHA) aliuliza:- Mradi wa TASAF ni mradi wa kusaidia kaya maskini nchini. Je, ni wananchi wangapi ambao wananufaika na mradi huo katika Visiwa vya Pemba na Unguja?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, fedha hizi za TASAF tunafahamu ni mkopo kutoka World Bank na fedha hizi zimekuwa zikitolewa kwa kaya maskini na fedha hizi hazijawahi kuonesha matokeo ya moja kwa moja kwa wale wananchi wanaopewa. Je, Serikali sasa iko tayari kufanya uchunguzi wa kina na tathimini na kuleta taarifa hapa Bungeni yenye kuonesha matokeo ya moja kwa moja kwa kaya hizi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili ni ukweli usiopingika kwamba fedha hizi za TASAF zimekuwa zikitolewa kisiasa kwa wana CCM na fedha hizi wakati panapotokea chaguzi ndogo zimekuwa zikitumika sana kushawishi kama sehemu ya rushwa kwa wana CCM ili CCM iweze kuchaguliwa. Nini kauli ya Serikali ikizingatia kwamba fedha hizi ni mkopo na zitarudishwa na Watanzania wote?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza mimi naomba nianze kumpongeza muuliza swali Mheshimiwa Msabaha kwa swali lake zuri, lakini pia nataka niwapongeze walengwa wa TASAF Unguja na Pemba. Katika nchi yetu mikoa inayoongoza kwa kufanya vizuri miradi ya TASAF ni mikoa ya Unguja na Pemba na kwa maana hiyo nataka nimpongeze Waziri mwenzangu, Mheshimiwa Mohamed Aboud Mohamed anayesimamia TASAF kule Pemba na Zanzibar ambaye anamsaidia Makamu wa Rais ambaye ndio Waziri mwenye dhamana ya TASAF Zanzibar. (Makofi)
Baada ya pongezi hizo naomba nitoe majibu ya maswali niliyoulizwa kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwamba TASAF haijaonesha matokeo; mimi ninanomba tusichanganye mambo, hoja kwamba mnaomba taarifa ya utekelezaji wa TASAF ikoje ni hoja ya msingi na inaweza ikaletwa. Mheshimiwa Mao Tse Tung anasema no research no right to speak. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ndio Waziri wa TASAF na juzi nimetoka Kilimanjaro nimeona jinsi walengwa kule na wengi ni wakina mama walivyopambana na umaskini kwa kutumia TASAF wameanza biashara ndogo ndogo mwingine amenunua ng’ombe, wengine wamejenga majumba mimi ninamuomba ndugu yangu, ng’ombe ananunuliwa baada ya kudunduliza. (Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, namuomba muuliza swali akubali ombi lake la mwanzo kwamba tupewa taarifa ya utekelezaji wa TASAF lakini kwa uhakika Kamati husika ya Bunge inapewa taarifa ya utekelezaji wa TASAF kila baada ya muda. Mheshimiwa Spika akisema taarifa ya TASAF anataka ailete humu ndani italetwa pasipo na mashaka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kwamba zinatolewa kisiasa, zinatumika chaguzi ndogo ndogo nini kauli ya Serikali jamaa zangu ndio yale niliyosema jambo hujalifanyaia utafiti usiliseme. Walengwa wote wa TASAF wanapendekezwa na wana vijiji wenyewe, wana vijiji wanaambiwa andika jina la mtu unayemuona kijijini kwako hapo anastahili kupata msaada wa TASAF, wakishafanyiwa hivyo sasa ndiyo Watendaji wa TASAF wanazunguka kwenda kuthibitisha kwamba je, huyu yuko na katika kuthibitisha hivyo wengine tumewafuta kwa kuona hawastahili kupata.
Mimi nataka niwaambieni hakuna mtu anayechanganya siasa katika TASAF wala hakuna ushahidi kwamba hela ya TASAF inatumika katika uchaguzi, mimi ningeweze kumuomba Spika kwamba Mheshimiwa athibitishe kauli yake, tusifike huko mimi nimekusamehe. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. MARYAM SALUM MSABAHA) aliuliza:- Mradi wa TASAF ni mradi wa kusaidia kaya maskini nchini. Je, ni wananchi wangapi ambao wananufaika na mradi huo katika Visiwa vya Pemba na Unguja?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, kwanza mimi nikiri kwamba ni Mjumbe wa Kamati ya Utawala na TAMISEMI na kwamba Kamati ilikwishafanya ziara mara kadhaa kwa ajili ya kukagua miradi ya TASAF na nikiri kwamba kuna maeneo ambayo TASAF inafanya vizuri tulitembelea Maswa pale tukakuta mama mmoja amejenga kajumba kake kwa njia hiyo vizuri, lakini sasa ni ukweli pia kwamba fedha hizi zinagawanywa kibaguzi na katika ziara tulielezwa na hofu inakuja jana tumemsikia Mheshimiwa Rais anasema ukiwa na chakula chako unawapa kwanza watoto wako halafu ndio unawapa jirani. Sasa mimi naiomba Serikali isipuuze hili suala la ubaguzi kwa sababu litagawa nchi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, Wizara iko tayari kubeba hili dukuduku, haya mashaka na kuyafanyia kazi kwa ajili ya mtengamano wa nchi? (Makofi)

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ninachompenda Mheshimiwa Selasini ni mtu mkweli, maana utangulizi wake amesema maeneo mengine TASAF wanafanya vizuri, mimi nampongeza kwa kuwa mkweli, lakini tulivyo sisi binadamu katika matarajio ya utendaji hawaweze watoto wote 100 wakafanya vizuri kama unavyotaka wewe. Mimi kama Waziri mwenye dhamana ya TASAF nakubali rai yake kwamba yale maeneo yenye malalamiko niyafanyie kazi na kwa uzoefu wangu mnavyo nifahamu hili jambo tutaliweka vizuri na naomba Mbunge yeyote ambaye ana ushahidi kwamba mahala fulani hizi pesa zinafanyika kwa upendeleo mimi nitalifanyia kazi. (Makofi)

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. MARYAM SALUM MSABAHA) aliuliza:- Mradi wa TASAF ni mradi wa kusaidia kaya maskini nchini. Je, ni wananchi wangapi ambao wananufaika na mradi huo katika Visiwa vya Pemba na Unguja?

Supplementary Question 3

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi nichangie kuuliza swali dogo. Kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake, lakini kwa kuwa huu sio mchango ni maswali ya nyongeza mimi naomba niseme kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa TASAF inafanya kazi nzuri sana hapa nchini na kwa kuwa TASAF imefanya kazi maeneo mengi sana hapa nchini kama vile upande wa afya, elimu sasa hivi TASAF inasimamia wanafunzi kwenda shuleni ambao zamani walikuwa hawaendi kutokana na kupunguza umaskini. Lakini nimesema hivi kwa uchungu kwa sababu gani TASAF kazi inayofanya haichagui vyama, haina mpango wa vyama tumeshuhudia Pemba, tumeshuhudia Unguja na tumeshughulikia na hapa Tanzania vyama vyote sichangii. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba sasa niulize swali kwa kuwa TASAF inafanya kazi nzuri, je, Serikali ipo tayari kuwaongezea fedha ili wakidhi haja zote?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kwanza kumshukuru Mheshimiwa Mchemba kwa pongezi alizolitoa kwa TASAF na sisi tutaendelea kuchapa kazi zaidi, lakini kuhusu swali lake kwamba je, TASAF iko tayari kuwaongezea fedha? Nataka niseme kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, malengo ya TASAF ni ya kuwafikia walengwa wote wanaohitaji kusaidiwa, mpaka sasa tumefikia walengwa asilimia sabini ndio maana kuna vijiji TASAF haijafika, kuna vijiji TASAF imefika lakini hatujawapata walengwa wote, huu mpango wa TASAF uko sehemu “A” na “B”. sehemu a ndio hii tunayoitekeleza sasa, TASAF ya Awamu ya Tatu “B” malengo ya Serikali ni kuwafikia walengwa wote, na ili kuwafikia walengwa wote ni dhahiri lazima tuongeze fedha.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO (K.n.y. MHE. MARYAM SALUM MSABAHA) aliuliza:- Mradi wa TASAF ni mradi wa kusaidia kaya maskini nchini. Je, ni wananchi wangapi ambao wananufaika na mradi huo katika Visiwa vya Pemba na Unguja?

Supplementary Question 4

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana naomba nimuulize bwana Waziri.
Mheshimiwa Bwana Waziri TASAF One ilifanya vizuri sana, TASAF Two nayo imefanya vizuri, na pia sasa TASAF Three nayo inaendelea vizuri. Lakini Mheshimiwa Waziri vipo viporo vya TASAF Two mfano, Barabara ya Bungulwa kwenda Hundya ambayo ilitengeneza makalavati 100, yapo pale Bungulwa zaidi ya miaka mitano sasa. Barabara ya Chibuji - Upamwa miaka mitano zaidi ilikuwa ilete pesa za ukamilishaji wa miradi hiyo miwili ya barabara ni viporo.
Mheshimiwa Waziri Mkuchika ni lini viporo hivyo vya barabara hizo vitaletwa ili kusudi barabara zitengenezwe?

Name

Capt. (Mst). George Huruma Mkuchika

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Newala Mjini

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, MENEJIMENTI YA UTUMISHI WA UMMA NA UTAWALA BORA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la rafiki yangu Mheshimiwa Ndasa kama ifuatavyo kuhusu viporo anavyouliza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninamuagiza Mkurugenzi wa TASAF huko aliko anakonisikiliza apeleke timu katika maeneo hayo, nipate taarifa ya hiyo miradi na baadae nitafanya maamuzi.