Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kiza Hussein Mayeye

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE (k. n. y MHE. ZITTO KABWE) aliuliza:- Kigoma Ujiji ni Mji wa kibiashara kwa kuwa ni Lango la Magharibi la nchi yetu kuelekea nchi jirani za Maziwa Makuu. Kutokana na hali hiyo Serikali ya Japan kupitia JICA imekuwa ikiandaa mradi wa kuboresha Bandari ya Kigoma kwa miaka kadhaa sasa:- (a) Je, Mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani hadi sasa? (b) Je, mradi huo utagharimu kiasi gani cha fedha na utaboresha maeneo gani ya Bandari ya Kigoma? (c) Je, mradi huo utaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 1

MHE. KIZA H. MAYEYE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nimshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri, lakini napenda kuuliza maswali ya nyongeza. Swali la kwanza, upanuzi wa Bandari hii ya Kigoma unakwenda sambamba na Bandari Ndogo za Ujiji na Kibirizi ni lini sasa Serikali watakamilisha ujenzi wa Bandari ya Ujiji na Kibirizi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, mwezi wa Nne Mheshimiwa Zitto aliuliza kuhusu Azimio la Mawaziri wa Maziwa haya Makuu ambapo walikubaliana Kigoma kuwa Bandari ya mwisho katika usafirishaji wa mizigo kwenda Mashariki ya Congo na Burundi. Je, Serikali wamefikia wapi katika utekelezaji wa azimio hili na lini watakamilisha ujenzi wa Bandari Kavu ya Katosho Kigoma? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Bandari Ndogo za Ujiji na Kibirizi ni moja kati ya Bandari za kipaumbele ambazo zinatafutiwa pesa ya ujenzi na Mamlaka ya Bandari Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, mpaka sasa hivi ninavyoongea Mheshimiwa Mbunge nikutaarifu tu kwamba Bandari ndogo ya Ujiji na Kibirizi ziko kwenye lot moja na zilishatangazwa tenda ya kutafuta mkandarasi wa kujenga na tenda hiyo ilifunguliwa tangu tarehe 28 Agosti na sasa hivi taratibu za kumpata mnunuzi wa kuendelea kuzijenga na kusanifu zinaendelea, na tutakapopata tutamtaarifu lini hizo Bandari zitaanza makandarasi na kuanza kujengwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu swali lake la pili Mheshimiwa Mayeye, ni kweli kwamba kulikuwa na changamoto ya kulipa fidia kwa wananchi ambao wako eneo la pale Katosho na wananchi walishalipwa na walishaachia sehemu kwa ajili ya kujenga Bandari kavu ya Katosho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hatua zilizofanyika mpaka sasa hivi ni kusafisha eneo lote kuona mipaka, lakini vilevile tumetangaza tenda kwa ajili ya kumpata mtu wa ku-design na kujenga majengo mbalimbali ndani ya eneo hilo na tenda inategemewa kufunguliwa katikati ya mwezi huu.

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE (k. n. y MHE. ZITTO KABWE) aliuliza:- Kigoma Ujiji ni Mji wa kibiashara kwa kuwa ni Lango la Magharibi la nchi yetu kuelekea nchi jirani za Maziwa Makuu. Kutokana na hali hiyo Serikali ya Japan kupitia JICA imekuwa ikiandaa mradi wa kuboresha Bandari ya Kigoma kwa miaka kadhaa sasa:- (a) Je, Mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani hadi sasa? (b) Je, mradi huo utagharimu kiasi gani cha fedha na utaboresha maeneo gani ya Bandari ya Kigoma? (c) Je, mradi huo utaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 2

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa swali la nyongeza. Kwa kuwa Bandari Ndogo za Kirando, Lukoma, Mgambo na Sibwesa hazijakamilika na kwa vile wafanyabiashara wa Jimbo langu la Kigoma Kusini kwenye kata zinazopakana na nchi za DRC, Burundi na Zambia hufanya biashara zao na kupitishia mizigo kwenye Bandari hii ya Kigoma. Swali langu; kwa kuwa wafanyabiashara hawa hutumia magari makubwa na wanapitia kwenye kivuko cha Ilagala na kivuko hiki hakina uwezo wa kubeba magari makubwa, je, kwa nini sasa tenda ya kutangazwa ujenzi wa Daraja la Ilagala haijatangazwa mpaka leo ilhali tumepitisha pesa kwenye bajeti ya mwaka 2018/2019? (Makofi)

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni kweli Serikali kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA) inayo mpango wa kujenga Bandari ndogo katika eneo la Kilando na Sibwesa. Mpaka sasa hivi Bandari ya Sibwesa imeshakamilika kwa asilimia 93, tunasubiri tu taratibu mbalimbali za kikandarasi na za kiufundi kwa ajili ya kwenda kuifungua hiyo Bandari ya Sibwesa ianze kutumika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari ya Kilando utaratibu wa kumpata mkandarasi unaendelea, tayari watu wameshafanya design; tunasubiri tu taratibu zikikamilika tutangaza tenda kwa ajili ya kumpata mtu wa kufanya ukarabati na ujenzi wa Bandari hiyo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ujenzi wa Daraja la Ilagala nimtaarifu tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari taratibu za mwanzo zimeshaanza za upembuzi yakinifu. Baada ya hapo tutafanya usanifu wa kina ili kupata gharama tutangaze tenda kwa ajili ya kumpata mkandarasi wa kujenga daraja hilo. Ahsante. (Makofi)

Name

Mbaraka Kitwana Dau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Primary Question

MHE. KIZA H. MAYEYE (k. n. y MHE. ZITTO KABWE) aliuliza:- Kigoma Ujiji ni Mji wa kibiashara kwa kuwa ni Lango la Magharibi la nchi yetu kuelekea nchi jirani za Maziwa Makuu. Kutokana na hali hiyo Serikali ya Japan kupitia JICA imekuwa ikiandaa mradi wa kuboresha Bandari ya Kigoma kwa miaka kadhaa sasa:- (a) Je, Mchakato wa mradi huo umefikia hatua gani hadi sasa? (b) Je, mradi huo utagharimu kiasi gani cha fedha na utaboresha maeneo gani ya Bandari ya Kigoma? (c) Je, mradi huo utaanza kutekelezwa lini?

Supplementary Question 3

MHE. MBARAKA K. DAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Gati la Kilindoni lilipo Wilayani Mafia lipo katika hali mbaya sana. Mbao zake zimechakaa, ngazi imekatika na lile tishali ambalo abiria pale wanapandia limekaa vibaya kiasi kwamba wakati wowote inaweza ikatokea ajali. Sasa Mheshimiwa Waziri ningependa atufafanulie, kwamba imekuwaje, ni lini Serikali itafanya ukarabati mkubwa wa gati la Kilindoni ukizingatia kwamba ile boti ya DMY itaanza kazi mwezi wa 10? Ahsante.

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ENG. ATASHASTA J. NDITIYE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kwamba gati la Kilindoni lipo katika hali isiyoridhisha kwa matumizi ya abira. Serikali kupitia Mamlaka ya Bandari Tanzania pamoja na wataalam kutoka TEMESA na DMY wameshatumwa maeneo yale kwa ajili ya kwenda kufanya ukaguzi na kuleta gharama ambazo zitatumika kutengeneza BOQ kwa ajili ya kufanya marekebisho makubwa ambayo tunakiri yanahitajika katika eneo hilo. Ahsante.