Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Aysharose Ndogholi Mattembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mkoa wa Singida unakua kwa kasi sana na ujenzi wa majengo makubwa ya kisasa umeongezeka, lakini kwa muda mrefu sasa hakuna gari la zimamoto linaloweza kuhudumia mkoa; gari lililopo kwa sasa ni bovu na lina ujazo wa lita 1,500 tu na lenye ujazo wa lita 7,000 lilipata ajali miaka iliyopita na Serikali iliahidi kulifanyia matengenezo lakini mpaka sasa haijafanya hivyo:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kisasa la zimamoto Mkoani Singida ili kukabiliana na majanga ya moto yanayoweza kutokea?

Supplementary Question 1

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Pamoja na majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuwa Mkoa wa Singida unakua kwa kasi na majanga ya moto yamekuwa yakitokea mara kwa mara, yakihusisha makazi na pia vile vile kwenye barabara kuu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuupatia Mkoa wa Singida gari la kisasa la zimamoto ili kuokoa maisha na mali za wananchi wake?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa gari la zimamoto lililopo ni bovu na halikidhi mahitaji; na ili kutoka Singida Mjini hadi kufika Wilayani Iramba, Manyoni, Mkalama na Ikungi kuna umbali mrefu. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzipa kipaumbele Wilaya hizi kwa kuzipatia magari ya kisasa ya zimamoto? Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu ni mpango gani wa Serikali wa kupeleka magari Singida pamoja na wilaya nyingine ambazo inazunguka; ni kama ambavyo nimejibu kwenye swali la msingi, kwamba, kwanza tutahakikisha tunafanya ukarabati wa lile gari bovu haraka iwezekanavyo pale tu fedha itakapopatikana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, katika bajeti yetu mwaka huu tumepanga kununua gari tano, kwa hiyo tutaangalia Singida kama ni mmoja wa Mkoa wa vipaumbele.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lingine kama ambavyo nimesema, ule mchakato wa kurekebisha sheria utakapokuwa tayari nadhani itasaidia sasa Halmashauri za Wilaya zilizopo katika Mkoa wa Singida kuweza kuchangia katika kununua magari haya yaweze kusaidia katika wilaya za nchi nzima.

Name

Oliver Daniel Semuguruka

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mkoa wa Singida unakua kwa kasi sana na ujenzi wa majengo makubwa ya kisasa umeongezeka, lakini kwa muda mrefu sasa hakuna gari la zimamoto linaloweza kuhudumia mkoa; gari lililopo kwa sasa ni bovu na lina ujazo wa lita 1,500 tu na lenye ujazo wa lita 7,000 lilipata ajali miaka iliyopita na Serikali iliahidi kulifanyia matengenezo lakini mpaka sasa haijafanya hivyo:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kisasa la zimamoto Mkoani Singida ili kukabiliana na majanga ya moto yanayoweza kutokea?

Supplementary Question 2

MHE. OLIVER D. SEMUGURUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Swali namba 19 lililoulizwa linafanana kabisa na changamoto iliyopo Jimbo la Ngara. Hivi juzi tulishuhudia gari zikiungua border ya Rusumo na ikapelekea kifo cha dereva, hakukuwa na gari la zimamoto. Je, ni lini Serikali itatuletea gari la zimamoto Wilaya ya Ngara?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Oliver kutokana na kuumwa kwake na maendeleo ya vyombo ama taasisi zetu zilizopo Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi kwa Mkoa wa Kagera ikiwemo Jeshi la Zimamoto. Kuhusiana na Wilaya ya Ngara, ukiachilia mbali mikakati ambayo nimeizungumzia nikijibu swali la msingi la Mheshimiwa Aisharose Matembe ambalo linagusa Wilaya zote nchini, mikakati ni ile ile.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini tuna pia tuna mipango mingine mbalimbali ambayo tunaendelea nayo, ambayo tunaamini kabisa ikikaa sawa basi changamoto hii ya upungufu wa magari ya zimamoto itapungua.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mpango wa kuweza kupata mkopo kupitia nchi za Belgium na Australia ambayo itatuwezesha kupata vitendea kazi ikiwa ni pamoja na magari mapya kabisa. Michakato ya kupata mikopo hiyo nayo inakwenda vizuri na iko katika hatua nzuri pale ambapo itakapokuwa imekamilika naamini kabisa tukichanganya na mikakati niliyozungumza katika swali la msingi basi matatizo ya magari ya zimamoto na vitendea kazi nchini ikiwemo Ngara yatakuwa yamepungua kwa kiasi kikubwa. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Alex Raphael Gashaza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. AISHAROSE N. MATEMBE aliuliza:- Mkoa wa Singida unakua kwa kasi sana na ujenzi wa majengo makubwa ya kisasa umeongezeka, lakini kwa muda mrefu sasa hakuna gari la zimamoto linaloweza kuhudumia mkoa; gari lililopo kwa sasa ni bovu na lina ujazo wa lita 1,500 tu na lenye ujazo wa lita 7,000 lilipata ajali miaka iliyopita na Serikali iliahidi kulifanyia matengenezo lakini mpaka sasa haijafanya hivyo:- Je, ni lini Serikali itapeleka gari la kisasa la zimamoto Mkoani Singida ili kukabiliana na majanga ya moto yanayoweza kutokea?

Supplementary Question 3

MHE. ALEX R. GASHAZA: Mheshimiwa, Mwenyekiti, pamoja na kwamba…
Mheshimiwa Oliver Semuguruka ameuliza swali hilo lakini nataka kusema kwamba Ngara ni sehemu ambayo ni special zone, ni mpakani. Tuna vituo viwili vya forodha vya pamoja, one stop border post kwenye mpaka wa Burundi na Tanzania na mpaka wa Rwanda na Tanzania.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ajali iliyotokea ya moto ya tarehe 19 mwezi wa jana ni ajali kubwa, gari sita zikaungua, dereva akafa, kwa hiyo tunaiomba Serikali iweze kuchukua nafasi na iweze kuchukua hatua ili tuweze kupata gari kwenye vituo hivi ambavyo sasa kumekuweko na msongamano mkubwa. Tayari Kamati ya Ulinzi na Usalama ilikwisha andika barua tangu tarehe 18 Mei, kwa hiyo tunaomba ichukue hatua ya dharura kwa ajili ya maeneo haya (Makofi). Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, hoja ya Mheshimiwa Mbunge ni ya msingi na tunaichukulia kwa uzito unaostahili. Tunatambua changamoto na location ya ile wilaya yake, Wilaya ya Ngara ama jimbo lake lilivyo, kuna umuhimu wa kuwepo kwa gari la polisi pale kwa sababu Mkoa wa Kagera tuna gari nadhani hazizidi nne ambazo zinasaidia kutoa huduma ikiwemo maeneo ya Ngara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, natambua umuhimu wa hilo jambo na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutalichukulia uzito unaostahili.