Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nzasa – Kilungule – Buza – Temeke:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hiyo muhimu kwa wakazi wa Mbagala, Mwanagati na Temeke?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYNABU M. VULU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa barabara ya Nzasa – Kilungule – Kwa Mwanagati na Buza ni muhimu sana kwa wakazi wa Mbagala, kwa maana ya Jimbo la Temeke na vile vile kwa wakazi wa Jimbo la Ukonga. Je Serikali, ina mpango gani wa muda mfupi wa kuweza kuboresha barabara hiyo ili wakazi hao waweze kupita kwa ufasaha na wepesi kusafirisha mazao na huduma za kijamii? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Wilaya Kisarawe, imepakana na Mkoa wa Dar es Salam na Jimbo la Ukonga; na kwa kuwa barabara inayopita Msimbu inaanzia Chanika. Je, Serikali ina mpango gani wa kuboresha au kujenga lami ya muda mrefu barabara inayoanzia Chanika – Msimbu hadi Masaki ambapo itaungana na barabara ya Mwanaromango ili kusaidia ujenzi wa taifa na kuendana na speed ya Mheshimiwa Rais kwa sababu tuko kwenye awamu ya viwanda na biashara? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi utaona jitihada kubwa ambazo zinafanywa na Serikali kwa kupitia mradi wa DMDP kuhakikisha kwamba Dar es Salam inajengeka, kwa maana ya miundombinu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Wilaya ambayo ameisema Mheshimiwa Mbunge kuna jumla ya shilingi bilioni 260 kati ya shilingi bilioni 660 imetengwa kwa ajili ya mradi huu. Naomba nimwondoe hofu, katika mipango ambayo inafanywa na taratibu karibu zote zimekamilika; tukishakamilisha ujenzi wa barabara hiyo ambayo na mimi nimeenda kuitembelea tutaenda mpaka Kisarawe.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nzasa – Kilungule – Buza – Temeke:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hiyo muhimu kwa wakazi wa Mbagala, Mwanagati na Temeke?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya barabara ambazo zina changamoto ya muda mrefu, lakini ni muhimu sana ni barabara ya Makongo kwa mantiki ya kwamba UCLAS, Makongo Juu kwenda Goba, hii barabara nimeuliza kwenye swali la TAMISEMI kwa sababu ni barabara ya halmashauri, lakini ina hudumiwa na TANROADS kwa mantiki ya ujenzi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nafahamu kwamba zoezi la tathimini ya kulipa fidia wananchi limeshakamilika, lakini lime stuck kwa muda mrefu. Sasa kwa sababu ya umuhimu wa hii barabara na ni barabara ya kimkakati kwa sababu inasadia kupunguza foleni wakati wa ujenzi wa madaraja pale njia ya Ubungo…
Mheshimiwa Mwenyekiti, nataka sasa Waziri aniambie; ni lini ujenzi wa barabara hii utakamilika kumalizia kipande ambacho kimeshaanzwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba katika ujenzi wa barabara kuna hatua mbalimbali na katika huu mradi wa DMDP lazima ipatikane no objection kwa kila hatua. Pale ambapo fidia inatolewa nafasi ili kama kuna malalamiko mengine ambayo yatakuwa yame-raise, baada ya kuwa sorted out ndipo tunaendelea na hatua ya pili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Halima, na bahati nzuri swala hili tumekuwa tukiwasiliana hata na Mheshimiwa Susan Lymo naamini na yeye labla anaishi maeneo hayo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliongea na Meneja wa TARURA kwanza kufanya marekebisho kwa muda wakati wa ujenzi mwingine unasubiriwa. Naomba avute subira, ni nia ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara hii inajengwa; lakini pia kusiwe na malalamiko kutoka kwa wananchi.

Name

Joyce Bitta Sokombi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nzasa – Kilungule – Buza – Temeke:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hiyo muhimu kwa wakazi wa Mbagala, Mwanagati na Temeke?

Supplementary Question 3

MHE. JOYCE B. SOKOMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kuiuliza Serikali; ni lini itajenga barabara itokayo Bunda kwenda Musoma Vijijini ili wananchi wa Kangetutya, Saragana, Bugoji na Kandelema wafaidike kwa sababu wakulima wanapolima mazao yao wanapata shida sana kusafiri kutoka Musoma Vijijini kwenda Bunda? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

M NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara zote kubwa zinajengwa; na nimepata fursa ya kwenda Mkoa wa Mara kuna kipande tumeanza kwa ajili ya kujenga daraja pale na yeye mwenyewe ni shuhuda kama atakuwa amepata nafasi ya kwenda hivi karibuni. Naomba nimhakikishie, Serikali ya Awamu ya Tano, suala la miundombinu ni kipaumbele chetu. Avute subira, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara zote zinajengwa.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. ZAYNABU M. VULU (K.n.y. MHE. MARIAM N. KISANGI) aliuliza:- Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya ujenzi wa Barabara ya Nzasa – Kilungule – Buza – Temeke:- Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara hiyo muhimu kwa wakazi wa Mbagala, Mwanagati na Temeke?

Supplementary Question 4

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Barabara za Jimbo la Ilala zote za Mjini ni mbaya, na tukamuita Waziri wa TAMISEMI, Mheshimiwa Jafo akaja akashuhudia, wakaitwa watu wa TARURA wote wakashuhudia, lakini mpaka leo barabara za Kalenga, Mindu, Mchikichi, Pemba, Aggrey, Likoma, Bonde, Mali, Utete, Morogoro, Kikuyu, Mafuriko, pamoja na barabara ya Pemba; barabara hizi zote; na barabara zote hizi ndiyo sehemu ya uchumi wa Dar es Salaam na huchangia asilimia 70 ya mapato ya Taifa katika Taifa hili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba Serikali ione umuhimu wa kuboresha kiundombinu hii ili wananchi waendelee kulipa kodi vizuri.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nawe ni shuhuda jinsi ambavyo Mheshimiwa Zungu anazifahamu barabara, amezitaja nyingi kweli kweli. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Zungu ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba barabara ndani ya Jiji la Dar es Salaam zinajengwa na kuboreshwa kwa kiwango kikubwa. Ndiyo maana kwa kupitia mradi wa DMDP imetengwa jumla ya shilingi bilioni 660 na zitajengwa kilomita 210.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naamini kabisa barabara ambazo Mheshimiwa Zungu amezitaja zitakuwa ni miongoni mwa barabara ambazo zitajengwa. Tuko kwenye hatua nzuri, baada ya muda si mrefu tutakuwa tumeshaweka Mkandarasi kwa ajili ya kuanza kujenga barabara hizo.