Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA - (K.n.y. MHE. JEROME D. BWANAUSI) aliuliza:- Madaraja ya Mwitika – Maparawe, Mipande – Mtengula na Mbangara – Mbuyuni yalisombwa na maji wakati wa mafuriko miaka mitano iliyopita na kusababisha matatizo makubwa ya usafiri:- Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo ili kuondoa adha ya usafiri inayowakabili wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, kwanza naishukuru Serikali kwa kufanya tathimini ya ujenzi wa madaraja haya. Eneo hili ni muhimu sana kwa uzalishaji wa zao la korosho na wananchi wanapata shida kweli wakati wa kusafirisha korosho kupeleka mnadani. Sasa je, Serikali leo inatoa tamko gani kwamba ni lini ujenzi huu unaanza hata kama ni kwa awamu?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, kikwazo kikubwa cha ujenzi huu ni bajeti ndogo ambayo wamepewa TARURA. Sasa je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza fedha ambazo zinaenda TARURA ili ujenzi wa madaraja nchini uweze kwenda kwa kasi inayotakiwa?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavo nimekiri kwenye majibu yangu ya msingi, kwamba umuhimu wa madaraja haya haina ubishani; lakini pia ni ukweli usiopingika kwamba ili kujenga madaraja haya kwa kiasi cha pesa kama tulivyotaja kwenye tathmini, bilioni 3.5 ni kiasi kingi cha fedha. Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge aiamini Serikali kwamba ina nia ya dhati ya kuhakikisha kwamba changamoto hii inatatuliwa ipo kinachogomba ni bajeti.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili anauliza uwezekano wa TARURA kuongezewa fedha ili iweze kufanya kazi kubwa. Jana nilijibu swali la nyongeza, kwamba ni vizuri pia tukazingatia kazi kubwa ambayo inafanywa na TANROADS na TARURA ndiyo tumeanza kuijenga, tuipe muda tuone namna ambavyo inatenda kazi kwa sababu pia itakuwa si busara kusema kiasi kingi cha fedha kitoke TANROADS kiende TARURA kwa sababu nao wana kazi kubwa ya kujenga barabara kwa kiwango cha lami.

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA - (K.n.y. MHE. JEROME D. BWANAUSI) aliuliza:- Madaraja ya Mwitika – Maparawe, Mipande – Mtengula na Mbangara – Mbuyuni yalisombwa na maji wakati wa mafuriko miaka mitano iliyopita na kusababisha matatizo makubwa ya usafiri:- Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo ili kuondoa adha ya usafiri inayowakabili wananchi?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri ukweli utabaki pale pale kwamba TARURA inahitaji nyongeza ya fedha. Pamoja na ubovu wa daraja liko tatizo la barabara ambazo zina mawe hazipitiki, kwa mfano katika Jimbo la Rombo, Kata za Handeni, Shimbi, na Makiidi ni Kata ambazo zilikumbwa na volkano na kwa hiyo mawe ni mengi barabara hazitengenezeki. Sasa, je, ni mkakati gani Serikali itakayofanya ili barabara kama hizi ziweze kupitika kwa sababu Vijijini ndiko kwenye uzalishaji?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na yeye kwamba kuna baadhi ya ameneo ambayo uhitaji wa pesa ni mkubwa. Kwa hiyo iko case by case, naomba Mheshimiwa nimhakikishie kwamba Ofisi ya Rais, TAMISEMI imekuwa ikichukua case by case, pale ambapo kuna uhitaji maalum kuna fedha ambazo zimekuwa zikitengwa ili kutatua changamoto ambazo zinakuwa zinawakabili wananchi wa maeneo husika.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA - (K.n.y. MHE. JEROME D. BWANAUSI) aliuliza:- Madaraja ya Mwitika – Maparawe, Mipande – Mtengula na Mbangara – Mbuyuni yalisombwa na maji wakati wa mafuriko miaka mitano iliyopita na kusababisha matatizo makubwa ya usafiri:- Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo ili kuondoa adha ya usafiri inayowakabili wananchi?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa daraja la Gwedegwede lilisombwa na maji wakati wa masika; na kwa kuwa wananchi wa Kata wa Zagaligali, Mbuga, Lumuma, Pwaga na Godegode wanazunguka mpaka Kibakwe, zaidi ya kilomita 75 ndipo wafike Mpwapwa Mjini. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga daraja la Godegode ili kuondoa usumbufu kwa wananchi wa maeneo hayo?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, daraja ambalo Mheshimiwa analitaja ana uelewa mzuri na daraja hilo. Naomba baada ya kumaliza kipindi hiki cha Bunge tuwasiliane ili tujue; kabla ya kuanza kujenga daraja hilo lazima tufanye tathimini tujue gharama kiasi gani cha fedha inahitajika ili tuhakikishe kwamba daraja hilo linajengwa ili kuondoa adha kwa wananchi ambao wanalazimika kuzunguka umbali mrefu.

Name

Janet Zebedayo Mbene

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ileje

Primary Question

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA - (K.n.y. MHE. JEROME D. BWANAUSI) aliuliza:- Madaraja ya Mwitika – Maparawe, Mipande – Mtengula na Mbangara – Mbuyuni yalisombwa na maji wakati wa mafuriko miaka mitano iliyopita na kusababisha matatizo makubwa ya usafiri:- Je, ni lini Serikali itajenga madaraja hayo ili kuondoa adha ya usafiri inayowakabili wananchi?

Supplementary Question 4

MHE. JANET Z. MBENE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana na pia nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Kwa kuwa suala la madaraja yanayounganisha Wilaya kwa Wilaya au hata Kata kwa Kata ni ya muhimu sana; Ileje tulijiongeza kuhusiana na suala hilo kuwa fedha inayohitajika ni kubwa, lakini mahitaji yaliyopo ni madogo. Kwa hiyo tumeomba kwa ombi maalum kuomba fedha ya kimkakati kwa ajili ya daraja linalopita mto Mwalwisi ambalo ndiyo linalotumika na mgodi wa makaa ya mawe Kiwira na Kabulo. Kwa hiyo nilitaka kujua hatima yake ni nini? Ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nilipata fursa ya kutembelea Ileje, na nimefika Jimboni kwake naomba nimpongeze sana jinsi ambavyo wananchi wa Ileje; hakika Ileje ambayo ilikuwa inatazamwa miaka hiyo siyo Ileje ya sasa hivi, Ileje inafunguka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba katika maeneo ambayo yana uwekezaji wa kimkakati ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba yanatatuliwa changamoto ili tunapoongelea kwenda kufuata makaa ya mawe kule isiwe ni adha. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mipango ya Serikali ya kuhakikisha kwamba makaa yale tunaanza kuyatumia lazima tufike daraja likiwa limekamilika. (Makofi)