Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. PAULINE P. GEKUL (K.n.y. MHE. JOSEPH M. MKUNDI) aliuliza:- Je, lini Serikali itapeleka umeme katika Vijiji vya Kakerege na Nkilizya vilivyopo Nansio Ukerewe?

Supplementary Question 1

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, maeneo mengi nguzo zimeshapelekwa katika vijiji hususani Mkoa wangu wa Manyara, kinachokosekana ni zile conductor na nyaya kwa ajili ya kuunganisha zile nguzo na umeme uwake na Mkandarasi wetu wa Mkoa wa Manyara ameagiza hizo conductors na nyaya muda mrefu viwandani na hili halijafanyika huenda hili tatizo lipo maeneo mengine. Naomba nifahamu ni lini sasa hizo conductors na nyaya zitatoka ili umeme uwake kwenye maeneo na vijiji vyetu ambavyo nguzo zimeshafikishwa?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naomba nitambue jitihada kubwa ambazo zimefanywa na Wizara hii, wamelipa shilingi milioni 102 kwa fidia ya wananchi wa Haraa kwa ajili ya umeme huu wa REA, Naibu Waziri anafahamu tulilishughulikia kwa karibu sana. Nitambue jitihada za KV400 ambazo zimefanyika na hivi navyoongea katika Mkoa wangu wa Manyara pale TANESCO Babati …
Mheshiwa Spika, ahsante. Jitihada hizi zinaendelea isipokuwa Mheshiwa Naibu Waziri kuna tatizo moja limejitokeza la variation kati ya Wizara ya Fedha na Wizara ya Nishati kwa baadhi ya wananchi ambao wanadai fidia hii ya KV400. Naomba nifahamu, hili tatizo la variation na reconciliation kujua hawa wanastahili kiasi gani linamalizwa lini kabla hawajaondoka Babati waweze kupata fedha hizo? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Subira Khamis Mgalu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Pauline Gekul, Mbunge Babati Mjini, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, kwanza kwa niaba ya Serikali tunapokea shukrani za Mheshimiwa Pauline kutokana na jitihada mbalimbali ambazo zimefanyika katika miradi hii ya REA. Amekiri na kutambua kwamba nguzo zimefika katika maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, kwenye suala la vifaa vya conductors na nyaya, nataka nimtaarifu Mheshimiwa Mbunge ni kweli hivi vifaa kwa mfano conductors wanaagiza nje ya nchi, lakini kwa kuliona tatizo la ucheleweshaji ndiyo maana baadhi ya vifaa katika mradi huu tulitoa maelekezo viwanda vyetu vya ndani vizalishe na wakandarasi waagize. Kwa hiyo, suala hili la vifaa hususani nyaya, viwanda vinavyohusika ni ni East African Cable pamoja na Kilimanjaro Cable, jambo ambalo limejitokeza wakandarasi wengi wanapenda kuagiza kwa mtu mmoja.
Mheshimiwa Spika, tumetoa rai kwamba kwa kuwa Serikali ilivyotoa maagizo ya kuviwezesha viwanda vya ndani kusambaza vifaa vya utekelezaji wa miradi hii, wakandarasi wote waone namna gani ya ku-order hivi vifaa wasirundike order kwa mtu mmoja. Kwa hiyo, naomba nilichukue hili tuende tukashulighulikie kwa kuwa nguzo zimefika maeneo mengi, basi vifaa vilivyosalia vifike ili kazi ikamilike na wananchi wapate huduma ambayo imekusudiwa.
Mheshimmiwa Spika, swali lake la pili nami nimshukuru kwa kufuatilia malipo ya fidia kwa wananchi wake na maeneo mbalimbali hususani katika mradi huu wa ujenzi wa njia ya umeme KV400 unaotoka Singida mpaka Namanga. Katika Wilaya yake kama alivyosema Serikali imeanza kulipa fidia, niishukuru sana Wizara ya Fedha kwa kutekeleza ahadi hiyo lakini amesema kuna variation. Naomba baada ya kikao hiki tukutane naye Mheshimiwa Mbunge ili tuweze kushughulikia suala ambalo amelisema. Mheshimiwa Spika, ahsante sana.