Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaynab Matitu Vulu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNAB M. VULU aliuliza:- Kilimo cha mwani kinalimwa baharini na asilimia kubwa ya wakulima wa zao hilo ni wanawake:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha zao hilo? (b) Je, Serikali inamsaidiaje mkulima wa mwani kupata soko la uhakika hususani nje ya nchi?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYNAB M. VULU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona na kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, kwa kuwa kilimo cha mwani kimekuwa hatarishi kutokana na mazingira kinapolimwa na kinalimwa na wanawake wanaoishi katika visiwa na ukanda wa bahari. Kutokana na mazingira hayo hatarishi, je, Serikali ina mpango gani kupitia benki, mashirika au taasisi zinazoendesha masuala ya bima ili kuweza kwenda kuwafikia wanawake hao na kuwapa elimu ya kuweza kuwapatia fedha za kutosha ili waweze kujikwamua katika vifaa na halikadhalika kuweza kujikinga na athari zozote zinazotokana na kilimo hicho kwa kuwa kinakuwa baharini? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa kilimo cha mwani mavuno yake ni mengi sana kutokana na zao lenyewe linavyofyonza maji mengi, je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha viwanda vidogo vidogo ili zao hilo liweze kuchakatwa na kuweza kusafirisha kwa wingi na kupata bei inayoweza kumkomboa mkulima wa mwani? Mheshimiwa Spika, nashukuru. (Makofi)

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya mama yangu, Mheshimiwa Zaynab Vulu, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoani kwetu Pwani, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza ni uhatarishi wa kilimo chenyewe cha mwani ambacho kinalimwa kama ulivyosema Msheshimiwa Spika ni pamoja na Jimboni kwangu Mkuranga katika Kata ya Kisiju kwenye Kisiwa cha Koma.
Mheshimiwa Spika, kwa bahati njema sana Shirika letu la Bima la Taifa (NIC) limekuja na mpango la kuhakikisha kwamba linaanzisha Bima ya Kilimo. Kwa hivyo, kwa kutumia dirisha hili la Bima ya Kilimo kutoka NIC na kwa kutumia mpango wetu wa ushirika kwa vikundi vya wakulima, naomba mimi na Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum mama yangu Mheshimiwa Zaynab Matitu Vulu na Wabunge wengine wakulima wa mwani tuwahamasishe wakulima wetu wa mwani kule vijijini wajiunge katika ushirika na hatimaye tuwaunganishe na Shirika letu la Bima ili kuweza kupata nafuu hii endapo litatokea lolote la kutokea.
Mheshimiwa Spika, jambo la pili ameniuliza juu ya viwanda vidogovidogo. Ni kweli kwamba tunahitaji kutengeneza viwanda vidogovidogo. Changamoto kubwa inayoonekana hivi sasa pamoja naye kusema kwamba uzalishaji ni mkubwa lakini kwa soko la kimataifa bado tunayo changamoto kubwa ya uzalishaji mdogo lakini na ubora wenyewe wa lile zao letu. Ndiyo maana tumeweka mkakati wa kuhakikisha tunazalisha zaidi na pili tunazalisha kilicho bora.
Mheshimiwa Spika, kwa upande wa viwanda vidogovidogo tumekuwa tukivisaidia sana pale Bagamoyo maeneo ya Mlingotini ni eneo mojawapo ambalo Wizara yangu inasaidia vidogovidogo. Kipo kiwanda kidogo ambacho kinafanya uchakataji na ku-pack mazao yanayotokana na zao hili la mwani. Sisi Serikalini tupo tayari kuhakikisha kwamba tunaendelea kuhamasisha uwekezaji katika viwanda vidogovidogo na kuwapa support wakulima wetu.

Name

Dr. Immaculate Sware Semesi

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYNAB M. VULU aliuliza:- Kilimo cha mwani kinalimwa baharini na asilimia kubwa ya wakulima wa zao hilo ni wanawake:- (a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha zao hilo? (b) Je, Serikali inamsaidiaje mkulima wa mwani kupata soko la uhakika hususani nje ya nchi?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa nafasi.
Mheshimiwa Spika, wakulima wa mwani sasa hivi wanapata shida kutokana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa sababu ya ule mfumo wa ukulima unafanyika katika maji mafupi, mazao yale ya mwani mengi yamekuwa yakifa kwa sababu ya joto la maji na mchanga. Napenda kujua nini mkakati wa Serikali kuwawezesha wakulima hawa ambao wengi wao ni wanawake waweze kufanikiwa katika kilimo hiki ukiangalia sasa hivi wanapata tatizo la mabadiliko ya tabianchi uzalishaji wa mazao yao unashuka chini? Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Abdallah Hamis Ulega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkuranga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mwalimu wangu Mheshimiwa Dkt. Sware Semesi, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kutokana na mabadiliko ya tabianchi kilimo cha mwani ambacho kilikuwa kikifanyika katika maji mafupi sasa kinawalazimisha wakulima wa mwani wasogee na waende katika maji marefu. Je, mkakati wetu ni nini kuwasaidia akina mama hawa ambao wana vifaa duni vya kuwapeleka katika haya maji marefu. Mojawapo ya mkakati ni kusisitiza na kupatikana kwa zile kamba, tunayo teknolojia ya kamba za kisasa za kufunga mwani ule ili uweze kuwa imara zaidi na upate ubora zaidi. Pili, ni kuwapa vyombo kwa maana ya boti ama mashine za kuwasaidia kuweza kufika walau kina kirefu kidogo. Kwa hivyo, huu ndiyo mkakati wetu na tayari Serikali tunazo mashine za kukopesha vikundi vya wavuvi, ikiwemo wakulima wa mwani. Kwa hivyo, Wabunge wote tunayo kazi ya kuvileta Wizarani vile vikundi vyetu ili tuweze kuwakopesha kile tulichonacho ili waweze kusogea katika hayo maji marefu zaidi. Ahsante.