Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sonia Jumaa Magogo

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali inasaidiaje watoto wa Shule za Msingi Wilayani Handeni ambao wamekuwa wakisongamana sana kwenye darasa moja?

Supplementary Question 1

MHE. SONIA J. MAGOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha na kujenga nyumba za walimu ili kuondoa adha ya tatizo hili ambalo limekuwa kubwa? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Serikali ina mkakati gani wa kuboresha miundombinu ya majengo ya shule nyingi ambazo kipindi cha mvua watoto wamekuwa wakipata wakati mgumu? (Makofi) Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Sonia Jumaa Magogo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ni kweli kama tulivyojibu kwenye jibu la swali la msingi ni kwamba tunayo changamoto kubwa sana katika nchi ambayo ilitokana na kutekeleza mpango wetu wa maendeleo wa elimu ambao sasa hivi kuanzia mwaka 2015 mwezi Desemba, tunatoa Elimu Msingi Bila Malipo. Hiyo imevutia wanafunzi wengi zaidi kudahiliwa katika shule kuanzia elimu ya awali, elimu ya msingi na sekondari. Kwa hiyo, tuna uhaba mkubwa sana wa madarasa, nyumba za walimu na vyoo.
Mheshimiwa Spika, hadi sasa Serikali imejenga vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, matundu ya vyoo katika shule za msingi 6,200 nchi nzima na kazi bado inaendelea, tunaendelea kufanya hivyo kwa kushirikiana na wananchi. Katika shule za sekondari tumezifikia shule za sekondari 3,159, hii ni kazi kubwa na ndiyo maana nikatoa wito kwamba jambo hili haliwezi kufanywa na Serikali peke yake, tuna jumla ya shule 22,000 za msingi na sekondari. Sasa kama tumefikia shule 9,000 bado tuna kazi kubwa ya kufanya, tunataka mpaka ifikapo mwaka 2020 angalau tuwe tumezifikia shule 17,000, hatuwezi kuzifikia shule 17,000 peke yetu bila ushirikiano wa wananchi.

Name

Salma Rashid Kikwete

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali inasaidiaje watoto wa Shule za Msingi Wilayani Handeni ambao wamekuwa wakisongamana sana kwenye darasa moja?

Supplementary Question 2

MHE. SALMA R. KIKWETE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona, naomba niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, Shule ya Msingi Majimatitu ina wanafunzi zaidi ya 4,000 hali ambayo husababisha wanafunzi wasipate haki yao ya msingi kitaaluma. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka kuhakikisha shule hii inaongezewa madarasa pamoja na kwamba amesema kuna shule nyingi zinaongezewa madarasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Salma Kikwete, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, shule ambazo zina wanafunzi zaidi ya 1,500 ni shule ambazo kwa kweli zimezidiwa na wanafunzi wanaohitajika kuwa katika shule moja. Kwa maana kwa viwango ambavyo vinakubalika shule ikiwa na wanafunzi 4,000 kwa kweli ni suala ambalo linahitaji tulishughulikie haraka sana. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Kikwete na wadau wengine wote wa hii Shule ya Msingi Majimatitu kama kweli ina wanafunzi 4,000 basi tutapeleka jicho letu haraka sana ikiwezekana basi tuigawanye ile shule ziwe shule mbili. Mheshimiwa Spika, ahsante sana. (Makofi)

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Naibu Waziri wangu kwa majibu mazuri sana ya awali.
Mheshimiwa Spika, nilitaka kuongezea tu kidogo, ni kweli shule ya Msingi Majimatitu mwaka jana darasa la kwanza peke yake walikuwa wanafunzi 1,200 na hii ni kutokana na programu ya elimu bure ambapo watoto wengi waliokuwa wanakosa fursa ya elimu wameenda pale. Serikali tulichokifanya ni kutafuta eneo lingine kwa ajili ya kujenga shule pacha jirani. Naomba niseme kwamba Serikali itafanya kila liwezekanalo ili ile shule pacha iweze kukamilika haraka iwezekanavyo tupunguze idadi ya wanafunzi walioko katika Shule ya Msingi Majimatitu.

Name

Goodluck Asaph Mlinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ulanga

Primary Question

MHE. SONIA J. MAGOGO aliuliza:- Je, Serikali inasaidiaje watoto wa Shule za Msingi Wilayani Handeni ambao wamekuwa wakisongamana sana kwenye darasa moja?

Supplementary Question 3

MHE. GOODLUCK A. MLINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, Shule ya Msingi Iputi iliyoko Kijiji cha Mbunga katika Jimbo langu la Ulanga ina msongamano mkubwa sana wa wanafunzi. Sisi tumejenga wenyewe shule nyingine, tumejenga ofisi ya mwalimu kwa kushirikiana na Mbunge wao, tunachoomba usajili na kutuletea walimu. Je, Serikali ipo tayari? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA TAWALA ZA MIKOA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA):
Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Godluck Mlinga, Mbunge wa Ulanga, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, ametupa habari hapa Bungeni kuhusu Shule ya Msingi Iputi ambayo tayari wananchi kwa kushirikiana na Mheshimiwa Mbunge wao wameshaanza ujenzi wa miundombinu ya shule hiyo katika Kijiji cha Mbuga. Nataka nimhakikishie kwamba, naomba ushirikiano wake tukitoka hapa Bungeni leo tuwasiliane na wenzetu wa Wizara ya Elimu ili shule ile tuanze taratibu za kuisajili na tukishaisajili tutaipatia walimu. Mheshimiwa Spika, ahsante.