Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucia Ursula Michael Mlowe

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE (K.n.y. MARY D. MURO) aliuliza:- Kumekuwepo na mkanganyiko wa watumishi wa zimamoto kwenye viwanja vya ndege na viwanja hivyo kutokuwa huru katika kuwatumia kutokana na kuwa si sehemu ya waajiri wao:- Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha viwanja vinajitegemea?

Supplementary Question 1

MHE. LUCIA M. MLOWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Pamoja na majibu ya Waziri naomba niulize kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza; kwa kuwa watumishi wa Jeshi la Zimamoto wanafanya kazi katika mazingira magumu na mazingira hatarishi, lakini hawana vifaa vya kufanyia kazi. Je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha watumishi hawa anapata vitendea kazi nchi nzima?
Mheshimiwa Spika, swali la pili; kwa kuwa Mkoa wa Njombe hadi sasa Jeshi la Zimamoto hawana Ofisi, je, Serikali ina mkakati gani kuhakikisha inajenga Ofisi pale Njombe? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Spika, ni kweli tuna changamoto ya vifaa ama vitende kazi kwenye Jeshi la Zimamoto na tunafanya jitihada mbalimbali kukabiliana na changamoto hiyo. Moja katika jitihada ambazo tunafanya ni kutenga fedha kwenye bajeti yetu kila mwaka ili kuweza kununua vifaa zaidi ikiwemo magari na vitendea kazi vingine mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, vile vile tunajaribu kuimarisha mahusiano kati ya Jeshi la Zimamoto kupitia halmashauri pamoja na majiji mengine. Wakati huo huo tumekuwa tukibuni mikakati mbalimbali ikiwemo mikakati ya kuweza kuchukua program za mikopo ambazo sasa hivi tuna mchakato ambao unaendelea. Nisingependelea kuzungumza sasa hivi kwa sababu haujafikia katika hatua ya mwisho, lakini ni moja katika jitihada ambazo tunafanya kuhakikisha kwamba Jeshi la Zimamoto linapata vifaa.
Mheshimiwa Spika, kuhusiana na suala la Njombe, ni changamoto ya Ofisi katika mikoa hii mipya. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunalifahamu hilo na tunalichukulia kwa uzito na pale ambapo hali ya kifedha itaruhusu tutakabiliana na changamoto ya Ofisi katika Mkoa wa Njombe na mikoa mingine hususani mikoa mipya.

Name

Julius Kalanga Laizer

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Monduli

Primary Question

MHE. LUCIA M. MLOWE (K.n.y. MARY D. MURO) aliuliza:- Kumekuwepo na mkanganyiko wa watumishi wa zimamoto kwenye viwanja vya ndege na viwanja hivyo kutokuwa huru katika kuwatumia kutokana na kuwa si sehemu ya waajiri wao:- Je, nini kauli ya Serikali kuhakikisha viwanja vinajitegemea?

Supplementary Question 2

MHE. JULIUS K. LAIZER: Mheshimiwa Spika, ahsante, nashukuru kwa kunipa nafasi. Tumekuwa na tatizo la kuungua kwa majengo mbalimbali ya Serikali ikiwemo vyuo na shule za sekondari hata katika Halmashauri ya Wilaya ya Monduli. Je, nini mkakati wa kuhakikisha kwamba angalau kila halmashauri inapata gari moja la Zimamoto?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Spika, swali lake linafanana sana na swali ambalo limeulizwa kwenye swali la msingi ambalo nimeshalijibu. Kwa hivyo jibu lake linakuwa vile vile, kwamba, mikakati ni ile ile ambayo nimeizungumza kuhakikisha kwamba tuna dhamira hiyo hiyo ya kuona kwamba magari yanafika katika maeneo takribani yote. Ndiyo maana tumeanza jitihada sasa hivi za kutanua wigo wa kuweza kupeleka huduma ya Zimamoto katika Wilaya nyingi zaidi.
Mheshimiwa Spika, kila mwaka tumefanya jitihada hizo kwa kufungua Ofisi, kupeleka Maaskari wetu kuanza kutoa huduma za kutoa elimu ili pale ambapo magari yatakapokuwa yamepatikana na vifaa vingine tuweze kuvifikisha huko viweze kusaidia jitihada hizi ambazo tumeanza nazo kwa mafanikio makubwa.