Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Kilwa:- Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro huo ili kuleta amani katika Wilaya hizo kabla amani haijatoweka?

Supplementary Question 1

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Pamoja na majibu yanayoridhisha ya Mheshimiwa Waziri, mgogoro huu, kama mwenyewe anavyokiri ni wa muda mrefu na mimi nimeshakwenda kwa Mheshimiwa Waziri wa Ardhi akaniambia kwamba mgogoro huu bado uko kwenye ngazi ya mkoa, watakaposhindwa ngazi ya mkoa watauleta Wizarani. Nimekwenda kwa Mkuu wa Mkoa ameniambia kwamba yeye ameshauandikia Wizarani kwa maana ya kwamba wameshashindwa.
Mheshimiwa Spika, hata h ivyo, mimi mwenyewe binafsi nimemuandikia Mheshimiwa Waziri kumjulisha mgogoro huu mpaka sasa hivi sijapata majibu yoyote. Sasa kutokana na huu mkanganyiko wa kauli za Serikali, Mkuu wa Mkoa anasema hili na Waziri anasema lingine, nini kauli ya Serikali juu ya mgogoro huu yaani nani kati yao yuko sahihi?
Mheshimiwa Spika, swali la pili, anasema mgogoro huu utashughulikiwa mwaka huu wa 2018/2019. Je, Mheshimiwa Waziri, yuko tayari kuandamana na mimi baada ya Mkutano huu twende akaangalie hali halisi? Kwa sababu tayari watu walishaanza kuchomeana ufuta, juzi hapa ufuta wa Kijiji cha Mirui umekatwa na wananachi wa kutoka Kilwa.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya familia, napenda kuwashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa namna ambavyo wameshiriki katika msiba huu. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, ni wiki mbili tu kabla ya msiba nilikuwa kule na nimefika mpaka kwenye jimbo lake. Taarifa nilizozipokea kutoka mkoani, walisema migogoro yote walikuwa wameorodhesha na wakasema kama mkoa wameunda timu za kiwilaya wanashughulikia migogoro yao, itakapowashinda wataileta Wizarani na taarifa ya maandishi wamenipa.
Mheshimiwa Spika, nataka tu nimhakikishie kwamba pamoja na kwamba timu ya Wizara iko kule katika kushughulikia ule mgogoro, lakini pia mkoa ulijiridhisha na ukaniridhisha pia mimi nilipokuwa kule kwamba migogoro yao wanaisimamia wenyewe kwa sababu haijawashinda na wakikamilisha Wizara itakwenda kuweka mipaka, hasa katika yale maeneo ambayo yana utata wa mipaka.

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA aliuliza:- Kumekuwa na mgogoro wa muda mrefu wa mpaka kati ya Wilaya ya Liwale na Wilaya ya Kilwa:- Je, ni lini Serikali itamaliza mgogoro huo ili kuleta amani katika Wilaya hizo kabla amani haijatoweka?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa fursa hii. Kama ilivyo Liwale, Wilaya ya Hanang kila upande imezungukwa na migogoro ya mipaka kati yake na Mbulu, Singida na Kondoa. Nataka kujua TAMISEMI itachukua hatua gani, kwa sababu imekuwa muda mrefu mno, hatimaye watu watauana kule ili haya matatizo ya mpaka yanayotukabili yaweze kutatuliwa na watu waishi kwa amani? Ahsante.

Name

Dr. Angeline Sylvester Lubala Mabula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Ilemela

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Migogoro ya mipaka iko mingi katika maeneo mengi lakini suluhisho la kwanza katika kutatua ile migogoro ni kwa pande zote mbili za maeneo husika kukaa. Kwa hiyo, pale wanapokuwa wamekaa wamekubaliana kwa pande zote mbili na hasa panapokuwa na utata, hapo ndipo Wizara inakuja kuingia kwa ajili ya kusaidia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, niombe tu, pamoja na swali la Mheshimiwa Dkt. Mary Nagu na wengine ambao wana migogoro, pale inaposhindikana ndipo hapo tunatakiwa kuingilia kati kwa sababu huwezi kuingilia kati kabla pande zote mbili hazijakaa na kuridhia na kwa kuangalia zile GN zilizounda maeneo hayo ziko katika utaratibu upi.