Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/ mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwanza nishukuru kwa majibu hayo ambayo yamejibiwa sasa hivi lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, Madiwani wanafanya kazi sawa na Wabunge. Kwa nini Serikali isiwalipe mishahara kama ambavyo Wabunge wanapewa mishahara? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kwa nini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa, sasa hivi Serikali haijaona umuhimu wa kuwalipa posho ambayo wanastahili kupata maana wanalipwa posho ndogo sana. Serikali ingeona umuhimu kwa sababu wao wanasimamia kazi za miradi ya maendeleo katika mitaa. Kwa hiyo, ningeomba sasa Serikali ifanye maamuzi ya kuwaongezea posho ili waweze kukidhi mahitaji yao. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) : Mheshimiwa Spika, katika swali lake la kwanza, ni kweli kwamba Madiwani wamekuwa na mtazamo huo wa kuomba kwamba kuwe na malipo hayo ya mshahara, Serikali iliyapokea na hata wakati Rais alivyohudhuria kikao cha ALAT mwaka jana alipokea maombi yao. Mimi nasema tu kwamba majibu yaliyotolewa pale ndiyo sahihi na hadi hapo Serikali itakapotoa maelekezo mengine lakini kwa sasa hivi tutaendelea na utaratibu ambao tunao.
Mheshimiwa Spika, katika swali lake la pili kuhusu Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Vitongoji na Mitaa kwamba posho ni ndogo sana, msisitizo ambao tunautoa sisi kila Halmashauri ifanye mapitio (review) ya vyanzo vyake vya ndani pamoja na mbinu zao za makusanyo, wakusanye kiwango cha kutosha cha mapato ya ndani na wahakikishe kwanza, hata hiyo ndogo maana maeneo mengine mengi tuna malalamiko kwamba hawalipi, hata hiyo ndogo basi inalipwa baada ya hapo sasa ndiyo tutaona tunaendaje huko mbele. (Makofi)

Name

Hasna Sudi Katunda Mwilima

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Kigoma Kusini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/ mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 2

MHE. HASNA S. K. MWILIMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Posho ya Wenyeviti wa Serikali za Vijiji kwenye Halmashauri zingine hawalipwi kabisa. Sasa nataka niulize tu swali kwa nini Wizara ya TAMISEMI isitoe Waraka Maalum kwenda chini kwa Wakurugenzi wote kuwaelekeza kwamba katika own source za Halmashauri wawe wanatoa kiasi fulani kwa ajili ya Wenyeviti wa Vijiji huku tukijua hao ndiyo wanaotusaidia kufanya kazi kubwa za maendeleo kwa niaba ya Serikali? (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) : Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi, huo Waraka ambao Mheshimiwa Mbunge anaupendekeza ulitolewa mwaka 2003, lakini kwa sababu umekuwa ni wa muda mrefu pengine labda baadhi ya wenzetu wanaanza kuusahau, basi tutachukua ushauri wake ili tutoe maelekezo tena.
Mheshimiwa Spika, msisitizo ni kwamba lazima Halmashauri zote zifanye mapitio ya vyanzo vyao vya mapato, waongeze mbinu za ukusanyaji wa mapato ya ndani ili kusudi wawe na uwezo mzuri wa kuweza kulipa. Hii ni kwa sababu hata taarifa za CAG zinaonesha kwamba ile asilimia 20 katika baadhi ya Halmashauri imekuwa hairudi kule kwenye vijiji kwa sababu tu ya malalamiko kwamba wamekusanya kidogo sana. Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- (a) Je, ni lini Serikali itadhamini Wenyeviti wa Serikali za Mitaa ili waweze kupata mikopo kama ilivyo kwa Madiwani na Wabunge? (b) Je, ni lini Serikali itaanza kuwalipa posho/ mishahara Wenyeviti wa Serikali za Mitaa?

Supplementary Question 3

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Mimi ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa Mstaafu, Mtaa wa Kivule. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, kitendo cha Serikali kutokutoa maelekezo mahsusi ya Wenyeviti wa Mitaa kulipwa posho inapelekea mzigo huu kupelekwa kwa wananchi ndiyo matokeo ya zile barua ambazo zinalipiwa, wananchi wanatwishwa mzigo huu. Kwa hiyo, ningeomba nijue, kwa kuwa Serikali imechukua vyanzo mbalimbali vya mapato kutoka Halmashauri na Halmashauri haipeleki fedha hizo kulipa Wenyeviti wa Mitaa na wanafanya kazi kubwa masaa 24.
Mheshimiwa Spika, ni kwa nini isiwekwe sheria moja kwa moja ili wadai kama haki? Kwa sababu sasa hivi ni posho kwa hiyo hawana uhalali wowote ule, Halmashauri inaamua ilipe ama asilipe. Ni kwa nini Serikali isiwajali watu ambao ni wengi sana katika nchi hii, wanafanya kazi kubwa sana ya miradi, ulinzi na usalama, usafi na ku-impose sheria mbalimbali walipwe pesa ya kisheria badala ya hii ambayo ni hiari? Mheshimiwa Spika, ahsante. (Makofi)

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA) : Mheshimiwa Spika, kama anavyosema ni kweli Wenyeviti wa Serikali za Vijiji, Vitongoji na Mitaa wanafanya kazi kubwa na nyingi na kweli mzigo ni mkubwa sana kwa upande wao. Sisi kama Wabunge na Serikali tunawategemea sana katika kazi zetu za kila siku. Ili kazi zetu na za Serikali ziende lazima wale wafanye kazi.
Mheshimiwa Spika, sasa mapendekezo ambayo anayatoa na kuhusisha kwamba Serikali imechukua vyanzo vingi vya mapato kwenye Halmashauri, mimi nataka nimhakikishie kwanza kwamba vyanzo ambavyo vimechukuliwa siyo vingiā€¦
Mheshimiwa Spika, vyanzo vingi bado vipo katika Halmashauri na ndiyo maana tumewaambia kwamba wafanye mapitio. Wakishafanya mapitio Halmashauri ambayo itakuwa na changamoto za ziada basi wataleta taarifa TAMISEMI na tutaweza kuifanyia kazi.