Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO) aliuliza:- Kuna upungufu wa magari katika Vituo vya Polisi Mkoa wa Ruvuma. Yaliyopo sasa ni mabovu kabisa na hayafanyiwi matengenezo kutokana na ukosefu wa fedha. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka magari kwenye vituo hivyo? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka pesa kwenye vituo hivyo kwa ajili ya matengenezo ya magari na mafuta ya magari hayo ili polisi waweze kufanya kazi zao kwa wakati?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa kuwa Mkoa wa Ruvuma unapakana na nchi za Msumbiji na Malawi. Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza idadi ya magari pamoja na boti kwa polisi ili kudhibiti uhalifu katika sehemu za mipakani?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge, hata nilipotembelea Songea Mheshimiwa Mbunge pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma walileta hoja hiyo ya magari. Niseme tu kwamba Serikali tutazingatia maombi hayo punde tutakapopata magari. (Makofi)

Name

Joseph Osmund Mbilinyi

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Mbeya Mjini

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO) aliuliza:- Kuna upungufu wa magari katika Vituo vya Polisi Mkoa wa Ruvuma. Yaliyopo sasa ni mabovu kabisa na hayafanyiwi matengenezo kutokana na ukosefu wa fedha. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka magari kwenye vituo hivyo? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka pesa kwenye vituo hivyo kwa ajili ya matengenezo ya magari na mafuta ya magari hayo ili polisi waweze kufanya kazi zao kwa wakati?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPH O. MBILINYI: Mheshimiwa Spika, ahsante, good to see you again. (Kicheko)
Mheshimiwa Spika, pamoja na matatizo waliyokuwa nayo polisi kwenye masuala ya vyombo vya usafiri lakini nikuhakikishie Jeshi la Magereza lina hali mbaya sana, siyo tu magari mabovu ni kwamba hawana magari kiasi kwamba wanafikia kupeleka wafungwa ambao wana kesi au rufaa wanawafunga pingu wanawapeleka Mahakamani kwa miguu. Sasa hii ni mbaya sana kwa usalama wao Askari Magereza, lakini pia kwa usalama wa wale watuhumiwa ambao wamefungwa pingu na kutembezwa kwa miguu kwa sababu mathalani mtu anatuhumiwa kwa ujambazi halafu anapita mitaani wale wanaomtuhumu wanamuona, wanaweza wakamvamia na kumshambulia na kuhatarisha maisha ya yule mfungwa. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nimpongeze sana Mheshimiwa Sugu kwa kuuliza swali kwa experience na niseme tu kwamba yeye ni mshauri mzuri tutazingatia hilo ili tuweze kuweka mgao upande Jeshi la Magereza ili kuweza kuepuka tahadhari hiyo aliyoisema. (Makofi)

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO) aliuliza:- Kuna upungufu wa magari katika Vituo vya Polisi Mkoa wa Ruvuma. Yaliyopo sasa ni mabovu kabisa na hayafanyiwi matengenezo kutokana na ukosefu wa fedha. (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka magari kwenye vituo hivyo? (b) Je, ni lini Serikali itapeleka pesa kwenye vituo hivyo kwa ajili ya matengenezo ya magari na mafuta ya magari hayo ili polisi waweze kufanya kazi zao kwa wakati?

Supplementary Question 3

MHE. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, kwa kuwa katika Mkoa wetu wa Iringa kuna magari ambayo huwa yanaharibika tu kidogo yanawekwa katika vituo lakini tumekuta kuna mlundikano mkubwa sana wa magari mabovu. Ni kwa nini Serikali sasa aidha itengeneze au iyauze haraka sana ili yaweze kusaidia upungufu mkubwa ulipo katika Mkoa wetu wa Iringa?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Ritta kwa wazo alilotoa. Niseme tu kama Serikali tunapokea ushauri huo, tutayatengeneza yale yanayotengenezeka na tutafanya utaratibu wa kuyauza yale yasiyoweza kutengenezeka.
Mheshimiwa Spika, kuhusu maoni yako upande wa pikipiki nilishatoa maelekezo kwamba vijana wa bodaboda wanaokamatwa kwa makosa madogo madogo wafanyanyiwe utaratibu wa kuandikisha na kuruhusiwa waendelee na kazi zao ili waweze kulipia kama kuna faini ambazo walitakiwa kulipa kuliko kuzirundika pikipiki hizo na zingine kuweza kuharibika wakati wangeweza kulipia. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, la mwisho, juzi sikukuona pale Uwanja wa Taifa, tunamshukuru sana Mheshimiwa Rais kwa kwenda pale kwa sababu kwa kweli kwa matokeo yale kama Rais asingekuwepo viti visingebaki salama. (Makofi/ Kicheko)