Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Victor Kilasile Mwambalaswa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupa

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, Idara ya Mahakama iliandika Ripoti za Sheria (Law Reports) ngapi kwa mwaka 2017?

Supplementary Question 1

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Swali la kwanza, majibu ya Serikali yanaonyesha kwamba uchapishaji wa mara kwa mara wa ripoti hizi ni muhimu sana, kwanza kwa best practice, openness na ease of reference.
Ni kitu gani kimefanya ripoti hizi zisichapishwe kwa miaka minne mfululizo? La kwanza.
Mheshimiwa Spika, swali la pili, naiunga mkono sana Serikali kwa juhudi zake za kupunguza mlundikano wa kesi Mahakamani kwa ku-appoint Majaji wengi. Hata hivyo, kuna practice hii ya Majaji kwenda likizo mwezi Desemba na Januari ambayo ni ya historia tu. Je, Serikali haioni kwamba umefika wakati sasa wa kuwapangia Majaji likizo wakati wowote wa mwaka (Januari mpaka Desemba) badala ya kuwaweka wote kazini na kwenda likizo Desemba mpaka Januari?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Victor Kilasile Mwambalaswa, Mbunge wa Lupa, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, moja ya sababu iliyosababisha Law Reports kutotoka kwa wakati, kwanza ilikuwa ni mabadiliko makubwa sana ya Editorial Board. Editorial Board ya Law Reports hizi ni Shule Kuu ya Sheria ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na pamekuwa na mabadiliko makubwa pale ambayo yalifanya kazi ya uhariri wa hizo kesi ichukue muda kwa sababu siyo kuzihariri tu ni pamoja na kuzichambua na kuzihariri.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, napenda kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tatizo hilo limeonekana na ndiyo maana tumeamua kuchapa ripoti zote nne kwa wakati mmoja na baada ya hapo Mahakama na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam tumekubaliana kwamba sasa tutaanza kutoa annual reports.
Napenda tu kumfahamisha Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari katika huu mwaka wa 2018 tumekwishaandaa asilimia 42 ya mashauri yaliyoamuliwa. Kwa hiyo, ni mategemeo yetu mwisho wa mwaka tutatoa ripoti ya mwaka 2018.
Mheshimiwa Spika, kuhusu likizo ya Majaji mwezi Desemba mpaka Januari, nikubaliane na wewe kabisa kwamba ni utamaduni wa nchi za Commonwealth kwamba Desemba na Januari Majaji wote wanakwenda likizo kwa sababu huko kwa wenzetu Uingereza mwezi Desemba na Januari kila kitu kinasimama na miezi hiyo watu hawafungwi ili wamalize Krisimasi ndiyo waende jela. Ni utamaduni tumeurithi, kwa hiyo, nitamshauri Mheshimiwa Jaji Mkuu tuuangalie kwa mukhtadha na mazingira ya Tanzania. (Makofi)

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICTOR K. MWAMBALASWA aliuliza:- Je, Idara ya Mahakama iliandika Ripoti za Sheria (Law Reports) ngapi kwa mwaka 2017?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Na mimi naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Spika, sambamba na Mahakama nyingi kuwa chakavu na wale wazee wa Mahakama maslahi yao ni duni, ni lini Serikali itakarabati Mahakama zote na kuboresha stahiki za wazee wale?

Name

Prof. Palamagamba John Aidan Mwaluko Kabudi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilosa

Answer

WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Spika, moja, Mahakama inatekeleza mpango wa miaka kumi wa ukarabati na ujenzi wa Mahakama zote. Baada ya Bunge leo anione ili niweze kumpa mpango wote wa miaka kumi, lakini tuonane hapa hapa Bungeni. (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Spika, pili, wazee wa Mahakama, tutaangalia maslahi yao ili yazidi kuboreshwa.