Bunge la Tanzania
Jamhuri ya Muungano ya Tanzania
Name
Silafu Jumbe Maufi
Sex
Female
Party
CCM
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:- Kumekuwa na changamoto katika kuwapatia maji safi na salama wananchi wa Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma pamoja na kuwa Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa yako katika mikoa hiyo. Je, Serikali sasa haioni umuhimu wa kuanzisha mradi wa maji kutoka kwenye vyanzo hivyo na kusambaza kwa wananchi wetu?
Supplementary Question 1
MHE. SILAFU J. MAUFI: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili madogo ya kuiuliza Serikali yangu.
Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, mikoa hii ya pembezoni Serikali imekuwa inasuasua kuwapelekea huduma zinazohitajika kwa maendeleo ya jamii. Napenda kuiambia Serikali kwamba huu uzoefu walioupata kutoka Ziwa Victoria kupeleka maji Shinyanga, Tabora, Simiyu na kadhalika naomba basi uzoefu huu wakaupeleke katika mikoa ya Katavi, Rukwa na Kigoma. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, hii speed ya kupeleka maji katika Mji wa Ujiji ni ndogo sana, haina matunda mazuri kwa mikoa hii mitatu. Je, Serikali inasema nini katika kuhamisha uzoefu huu wa Ziwa Victoria na kuuweka katika mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, je, Serikali haioni kwamba inatumia fedha nyingi za kuchimba visima virefu katika vyanzo ambavyo havina uhakika, inaonaje ikatumia vyanzo hivi ambavyo ni vya uhakika…
Mheshimiwa Spika, ni katika kujenga hoja na kuweka mambo sawa. Napenda kufahamu ni lini hii awamu ya pili itaanza ili hivi vyanzo vya uhakika vya Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa vifanyiwa kazi ili wananchi wa Rukwa wapate maji ya uhakika? (Makofi)
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, awali ya yote kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge na ukimuona mtu mzima analia ujue kuna jambo. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, najua changamoto kubwa sana ya maji katika eneo lake. Sisi kama Wizara tupo tayari sasa kutoa ushirikiano na uzoefu wetu katika kuhakikisha wananchi wake wa maeneo ya Rukwa wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Mheshimiwa Spika, ikumbukwe sisi ni Wizara ya Maji na siyo Wizara ya Ukame, tupo tayari kuwapatia maji wananchi wa Rukwa.
Mheshimiwa Spika, katika kuongeza jitihada, nipo tayari kufanya ziara maeneo ya Mheshimiwa Mbunge ili kuangalia namna ya kuweza kutatua tatizo hili kwa haraka. Ahsante sana. (Makofi)
Name
Devotha Methew Minja
Sex
Female
Party
CHADEMA
Constituent
Special Seats
Primary Question
MHE. SILAFU J. MAUFI aliuliza:- Kumekuwa na changamoto katika kuwapatia maji safi na salama wananchi wa Mikoa ya Rukwa, Katavi na Kigoma pamoja na kuwa Ziwa Tanganyika na Ziwa Rukwa yako katika mikoa hiyo. Je, Serikali sasa haioni umuhimu wa kuanzisha mradi wa maji kutoka kwenye vyanzo hivyo na kusambaza kwa wananchi wetu?
Supplementary Question 2
MHE. DEVOTHA M. MINJA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, changamoto ya tatizo la maji safi na salama kwa wananchi wa Manispaa ya Morogoro bado ni kizungumkuti. Bwawa la Mindu ambalo limekuwa likitegemewa na wananchi wa Manispaa kwa sasa halitoshelezi. Kwa kuwa Mkoa wa Morogoro una mito mingi, je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga bwawa lingine ili iwe mwarobaini kwa wananchi wa Manispaa ya Morogoro ambao wanakosa maji kwa muda mrefu?
Name
Jumaa Hamidu Aweso
Sex
Male
Party
CCM
Constituent
Pangani
Answer
NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Spika, nikubaliane na Mheshimiwa Mbunge dada yangu Devotha, ni kweli Morogoro kumekuwa na changamoto kubwa sana ya maji na tunajua kabisa tunaelekea Tanzania ya Viwanda, lazima tuwe na mahitaji ya maji kwa maana ya maji yenye utoshelevu. Sisi kama Wizara ya Maji tumeliona hilo, tupo kwenye majadiliano ya dola milioni 70 katika kuhakikisha tunaondoa kabisa tatizo la maji safi na salama katika Mkoa wa Morogoro. (Makofi)
Copyright © Bunge Polis 2024. All Rights Reserved