Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Kituo cha Polisi cha Marine Kipili, hakina usafiri wa nchi kavu:- (a) Je, ni lini Serikali itakisaidia kitu hicho usafiri wa nchi kavu angalau hata kukipatia pikipiki? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza mgao wa petroli?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na jiografia ya Wilaya ya Nkansi, naomba hilo swali labda angesaidia kujibu Mheshimiwa Stella Manyanya, Naibu Waziri wa Elimu, Teknolojia na Elimu ya Juu. Inaonekana hilo swali halikujibiwa jinsi inavyotakiwa na aliyeandika hilo jibu, hajui Wilaya ya Nkasi ilivyo; Kipili iko wapi, Namanyere iko wapi, Kala iko wapi, Itindi iko wapi, Kabwe iko wapi? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na majambazi katika mwambao wa Ziwa Tanganyika, hilo gari haliwezi kuhudumia vijiji vya mwambao wa Ziwa Tanganyika. Kwa hiyo, lini Serikali, itawapatia mgawo wa mafuta wa kutosha Wilaya ya Nkasi?
Mheshimiwa Naibu Spika, gari lenyewe liko Wilaya ya Nkasi, hata mafuta halina! Lini itaongeza mgao wa mafuta katika Wilaya ya Nkasi? Lini itawapatia pikipiki vijana wa Marine Kipili, ili kuondoa tatizo la usafiri ambako unatokea ujambazi katika vijiji vilivyopo jirani jirani na mwambao wa Ziwa Tanganyika ili kupunguza uharamia katika mwambao wa Ziwa Tanganyika?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI, TEKNOLOJIA NA UFUNDI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Ni kweli kwamba Wilaya ya Nkasi kijiografia imekaa na changamoto nyingi sana hasa ikizingatiwa kwamba baadhi ya vijiji vyake kama Kipili, Kala, Wampembe na vijiji vingine kama Samazi, vimekaa mbali kidogo, vinahitaji mwendo mrefu kuvifuata. Kwa hiyo, vinahitaji mafuta ya ziada. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, Serikali imefanya jitihada kubwa sana katika Mkoa wa Rukwa na Nkasi kwa ujumla. Kwanza kuna maboti ya kutosha ambayo yalipelekwa kwa ajili ya Jeshi la Wananchi ambao wamekuwa wakishirikiana kwa karibu sana na Jeshi la Polisi.
Vilevile kuna vituo ambavyo vimeanzishwa katika maeneo hayo na hivyo, kuwezesha kuwa na urahisi wa kuwafikia wananchi wanapokuwa na tatizo, hususan katika kijiji cha Kipili. Kwa hali hiyo, naamini kwamba pamoja na jitihada ambazo zimekuwa zikiendelea kufanyika hali ya Nkasi kwa sasa ni bora kuliko ilivyokuwa hapo awali. Ahsante sana.

Name

Khatib Said Haji

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Kituo cha Polisi cha Marine Kipili, hakina usafiri wa nchi kavu:- (a) Je, ni lini Serikali itakisaidia kitu hicho usafiri wa nchi kavu angalau hata kukipatia pikipiki? (b) Je, ni lini Serikali itaongeza mgao wa petroli?

Supplementary Question 2

MHE. KHATIB SAID HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kuniona. Imekuwa ni kawaida kwa Serikali kuleta majibu mara zote juu ya masuala yanayohusu vituo vya polisi, juu ya usafiri na uchakavu wa vituo hivi wakitoa majibu ya kufanana kwamba hali ya uchumi itakapotengemaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumekuwa tukishuhudia matumizi makubwa na ya nguvu yanayotumika kwa kununua mabomu, virungu, kila wapinzani wanapojaribu kufurukuta kwenye nchi hii. Mnatoa wapi bajeti ya kuwezesha mambo haya yakiwemo yale ya Operation Harass Wapemba kama mlivyofanya karibuni; mlitoa wapi fedha zile; mnaposhindwa kutekeleza mahitaji muhimu ya vituo vya polisi? Ahsante.

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI: Mheshimiwa Naibu Spika, ukweli ni kwamba hali ya usalama ya nchi yetu na jinsi ambavyo imekuwa tulivu, ni jawabu tosha kwamba maamuzi ya Serikali katika kuhakikisha kwamba inatawanya rasilimali zake kulinda ulinzi na usalama wa nchi yetu ni sahihi. Yote hayo yanafanyika kwa wakati mmoja. Ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba wananchi wa nchi hii wanakuwa salama wakati wa uchaguzi, baada ya uchaguzi na kabla ya uchaguzi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunajaribu kuhudumia vituo vya oolisi, nyumba za askari na kadhalika, lakini wakati huo huo inapofika nyakati za uchaguzi tuna wajibu wa kuhakikisha kwamba usalama wa nchi yetu unaendeleaa kuimarika.