Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dua William Nkurua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA (K.n.y. MHE. RASHID A. AKBAR) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuliendeleza Bonde la Mto Ruvuma ili lilete tija kwa wananchi hasa wakulima?

Supplementary Question 1

MHE. DUA W. NKURUA: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, kwa kuwa Mheshimiwa Akbar amekuwa akiliuliza swali hili mara kwa mara, je, Mheshimiwa Waziri haoni umuhimu wa kutembelea Jimbo lake ili aweze kujionea hali halisi ya kule?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa Vijiji vya Masuguru, Mtambaswala, Nanderu, Ngonji na Marumba vimepitiwa na Bonde hili la Mto Ruvuma katika Jimbo la Nanyumbu, je, Serikali haioni umuhimu wa kuwapatia wananchi hawa skimu ya umwagiliaji ili kuwakwamua katika hali ya maisha? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote, napenda nitumie nafasi hii kumpongeza sana Mheshimiwa Akbar kwa namna anavyowatetea wananchi wake. Ni kweli amekuwa akiliuliza swali hili na amekuwa akilifuatilia mara kwa mara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya jukumu la Naibu Waziri ni kufuatilia miradi na kwenda kuangalia uhalisia. Niko tayari kwenda kuona mradi huo kama alivyoomba.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu mkakati wa kilimo cha umwagiliaji Nanyumbu, sisi kama Wizara ya Maji tuna eneo la hekta milioni 29.4 linalofaa kwa kilimo cha umwagiliaji na katika mikakati yetu ambayo tunataka kuhakikisha kwamba umwagiliaji unakuwa na tija kubwa kwenye uzalishaji, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge wa Nanyumbu, hatutawasahau wala hatutawaacha wananchi wa Nanyumbu katika kuhakikisha tunawapa kilimo cha umwagiliaji. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Daniel Edward Mtuka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Mashariki

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA (K.n.y. MHE. RASHID A. AKBAR) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuliendeleza Bonde la Mto Ruvuma ili lilete tija kwa wananchi hasa wakulima?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL E. MTUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba nami niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kushirikiana na Mbunge mwenzangu wa Bahi, Mheshimiwa Badwel, tumeweza kuchonga mfereji kutoka Mto Bubu kwenda kwenye vijiji vyetu kwenye skimu za umwagiliaji kwa kushirikiana na wananchi na Mfuko wangu wa Jimbo. Je, Serikali itakuwa tayari kutusaidia kuboresha miundombinu kwa maana ya mifereji midogo pamoja na mabanio katika Vijiji vyangu vya Lusilule, Udimaa, Ndamloi na Igose?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mtuka pamoja na Mheshimiwa Badwel wa Bahi kwa mapenzi ya dhati kwa wananchi wao katika kuhakikisha wanawasaidia. Sisi kama Wizara ya Maji katika kuwaunga mkono, hatutakuwa kikwazo katika kuhakikisha tunawasaidia ili wananchi wao waweze kupata miundombinu mizuri.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. DUA W. NKURUA (K.n.y. MHE. RASHID A. AKBAR) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuliendeleza Bonde la Mto Ruvuma ili lilete tija kwa wananchi hasa wakulima?

Supplementary Question 3

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mtemi, nakushukuru kwa kunipa fursa hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Lindi, tuna mto ambao una-flow maji kipindi chote, Mto Lukuledi unaopatikana katika Jimbo la Mtama na kuna skimu za umwagiliaji ambazo zilianzishwa na Serikali lakini kwa bahati mbaya zimeishia katikati, zime-stuck sasa zaidi ya miaka mitano. Tunataka kujua ni lini Serikali itakwenda kufanya upembuzi ili kujua kitu gani kilikwamisha na kuweza kufanya mpango ili zile skimu ziweze kufanya kazi yake kama ilivyokuwa imekusudiwa? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii kwanza kumpongeza Mheshimiwa Mbunge. La pili, tuna skimu zaidi ya 2,947. Sisi kama Wizara kwa muda huu tumeona tuna skimu nyingi lakini kwenye uzalishaji matokeo ni madogo sana. Waziri wangu akaona haja ya kuunda timu kuangalia changamoto zilizoko katika hizi skimu za umwagiliaji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya changamoto tulizoziona, tuna skimu nyingi lakini bado hazijakamilika. Mkakati wetu ni kwamba tunataka tuwe na skimu chache lakini ziwe na tija kubwa ili tuweze kufikia uchumi wetu ule wa viwanda katika kuhakikisha tunakuwa na kilimo cha umwagiliaji kizuri. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.