Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Nuru Awadh Bafadhili

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI (K.n.y. MHE. REHEMA J. MIGILLA) aliuliza:- Je, kwa nini Serikali haitaki kujenga Hospitali ya Wilaya ya Tabora Mjini baada ya Hospitali ya Wilaya kupewa hadhi ya Hospitali ya Rufaa?

Supplementary Question 1


MHE. NURU A. BAFADHILI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Napenda kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imetenga shilingi milioni 70 kwa ajili ya kuendeleza jengo la OPD; na kwa kuwa pesa hizo huenda zisikidhi kukamilisha jengo hili, je, Serikali ina mpango gani kuhakikisha inawaongezea fedha Wilaya ya Tabora ili waweze kupata Hospitali ya Rufaa ili kuepuka wagonjwa kupelekwa Hospital ya Bugando au Muhimbili? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Bafadhili, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa Mkoa wa Tabora tayari tunayo Hospitali ya Rufaa. Katika swali la msingi ambacho kinaulizwa ni Hospitali ya Wilaya. Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba ni azma ya Serikali kuhakikisha Wilaya zote ambazo hatuna Hospital za Wilaya zinajengwa. Ndiyo maana tumeanza na hospitali 67. Ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba fedha ambayo inapelekwa inaenda kutumika vile ilivyokusudiwa. Naomba nimkikishie, kama hicho kiasi cha fedha kilichotengwa shilingi milioni 70 hazitakidhi, Serikali itakuwa tayari kuhakikisha kwamba inaongeza fedha ili Hospitali ya Wilaya iweze kukamilika.

Name

George Malima Lubeleje

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. NURU A. BAFADHILI (K.n.y. MHE. REHEMA J. MIGILLA) aliuliza:- Je, kwa nini Serikali haitaki kujenga Hospitali ya Wilaya ya Tabora Mjini baada ya Hospitali ya Wilaya kupewa hadhi ya Hospitali ya Rufaa?

Supplementary Question 2

MHE. GEORGE M. LUBELEJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa baadhi ya Vituo vya Afya vimepewa shilingi milioni 500 ili vikamilishe ujenzi wake; na kwa kuwa ujenzi wa Kituo cha Afya Mbori, Wilayani Mpwapwa sasa ni miaka 10 haujakamilika. Je, Mheshimiwa Waziri yuko tayari kutoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya Kituo cha Afya Mbori ili waweze kukamilisha ujenzi?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE):
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Lubeleje, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ambavyo nimejibu katika jibu langu la msingi, ni azma ya Serikali kuhakikisha Vituo vya Afya 513 vinafanyiwa ukarabati ili ziweze kutoa huduma tunayokusudia. Namwomba Mheshimiwa Mbunge aridhike na kasi ya Serikali kwamba tumeanza na vituo 208 na juzi vimeongezeka viwili ikiwa ni Kituo cha Afya cha Kibondo na kingine Nsimbo. Baada ya wafadhili kuona kasi nzuri ya Mheshimiwa Dkt. John Joseph Magufuli kuhusiana na suala zima la afya, nao wameamua kuweka nguvu katika maeneo ambayo yanahudumia wakimbizi. Kwa hiyo, badala ya vituo 208 sasa tuna vituo 210.