Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Abdulrahiman Ghasia

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mtwara Vijijini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA) aliuliza:- Wadhibiti wa Ubora wa Elimu ngazi ya Wilaya wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa vitendea kazi. • Je, Serikali ina mkakati gani wa kushughulikia changamoto za ofisi hizo ili ziweze kutekeleza majukumu yao? • Je, ni lini Wizara itapeleka Wadhibiti Ubora wa Elimu katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba badala ya kutegemea wale wa Halmashauri ya Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA A. GHASIA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kuuliza maswali ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Mji wa Nanyamba ina umri wa zaidi ya miaka mitatu tangu kuanzishwa kwake, je, mchakato wa kuanzisha ofisi mpya ya udhibiti ubora inachukua muda gani ikiwemo ni pamoja na kupata vitendea kazi pamoja na watumishi wa kutosha. (Makofi)
Mheshimiwa Spika, Halmashauri mama ambayo ni Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara, bajeti ambayo imetengewa na imepelekwa na Serikali imeweza kukagua shule 18 tu kati ya shule 106; je, Serikali inapoilekeza ikakague Nanyamba kwa bajeti ipi ambayo imeipeleka? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, kuhusu ni muda gani inahitajika kazi ya kuanzisha ofisi ya udhibiti ubora itachukua, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba hakuna muda maalum, yote inategemeana na upatikanaji wa fedha na tunachosema tu ni kwamba kwa sasa tumejipanga kwamba tutahakikisha kwamba Wilaya zote zinakuwa na wadhibiti ubora. Kwa hiyo, tutaendelea kutafuta fedha ili kuhakikisha kwamba ofisi hizo zinakuwepo.
Mheshimiwa Spika, kuhusu swali la pili kwamba Halmashauri mama ya Mtwara yenyewe bado haijaweza kufanya ukaguzi kwa kiwango kikubwa.
Naomba nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba lengo letu ni kuhakikisha kwamba kadri tunavyoendelea tunapanua uwezo wa wadhibiti ubora wetu kuweka kufanya udhibiti ubora. Kwa hiyo, hata kama sasa kiwango cha udhibiti ubora kilichofanyika bado ni kidogo lakini lengo letu ni kuendelea kuongeza fedha ili tuhakikishe kwamba tunaweza tukafanya hiyo kazi kwa ufanisi na kwa wingi zaidi.

Name

Edwin Mgante Sannda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. HAWA A. GHASIA (K.n.y MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA) aliuliza:- Wadhibiti wa Ubora wa Elimu ngazi ya Wilaya wanakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa vitendea kazi. • Je, Serikali ina mkakati gani wa kushughulikia changamoto za ofisi hizo ili ziweze kutekeleza majukumu yao? • Je, ni lini Wizara itapeleka Wadhibiti Ubora wa Elimu katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba badala ya kutegemea wale wa Halmashauri ya Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. EDWIN M. SANNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Katika jitihada za kuendelea kuinua ubora wa elimu suala la kuimarisha kitengo hiki cha udhibiti ubora ni suala ambalo kwa kweli halina mjadala. Hali ilivyo sasa hivi wale wenzetu pale ni kama wamevunjika moyo na wamekata tamaa kwa kukosa motisha.
Mheshimiwa Spika, je, ni lini sasa Serikali itawaweka hawa watumishi wa kitengo hiki kwenye viwango kama ilivyo maafisa elimu au walau waweze kupewa posho za madaraka kama zilivyo za Walimu Wakuu, Wakuu wa Shule na Wataribu wa Elimu Kata? (Makofi)

Name

William Tate Olenasha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA:
Mheshimiwa Spika, Serikali inachukua hatua mbalimbali kujaribu kuboresha namna tunavyofanya udhibiti ubora. Kitu cha kwanza kikubwa ambacho kimefanyika ni kubadilisha mfumo wenyewe.
Mheshimiwa Spika, huko nyuma tulikuwa tunazungumzia kuhusu ukaguzi au tulikuwa tunawazungumzia wakaguzi wa shule, sasa hivi mfumo ule umebadilika tunasema ni udhibiti ubora. Mfumo ambao wanaohusika sio wale wadhibiti ubora tu lakini hata walimu wenyewe na wadau wengine kama wazazi kwa mfano kama kuna watu wanamiliki shule binafsi.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, mfumo uliopo sasa ni mfumo ambao ni shirikishi; tunaamini mfumo huo utatusaidia kwa sababu kila mmoja wetu anahusika.
Mheshimiwa Spika, vilevile changamoto ambazo zipo kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kwa mfano kama magari, vitendea kazi na idadi ya Wadhibiti Ubora wenyewe kama nilivyosema Serikali inaendelea kuboresha na kwa kuanzia nafikiri karibuni tutagawa hata magari kwa zaidi Halmashauri 40 kama sehemu hiyo ya jitihada zetu za kuhakikisha kwamba tunaondokana na upungufu wa vitendea kazi vilivyopo.
Mheshimiwa Spika, vilevile tuna mpango wa kujenga ofisi zaidi ya 50 kwenye Halmashauri zetu, lengo ni kuhakikisha kwamba tunaendelea kuboresha huduma ya udhibiti ubora.
Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kusema kwamba kwa sasa hatutegemei tena tuwasikie Wadhibiti Ubora wakifanya kazi za kipolisi, ni lazima washirikishe wadau wote wakati wanafanya zoezi la udhibiti ubora.