Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mendard Lutengano Kigola

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa miundombinu ya maji katika Kata za Igowele, Nyololo, Mninga, Mtambula, Nyigo na Idunda?

Supplementary Question 1

MHE. MENDRAD L. KIGOLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Naibu Waziri. Mheshimiwa Waziri alikuja Mufindi na alikuja kwenye Kata ile ya Mtwango. Mradi wa Kata ya Mtwango una miaka karibu sita na mkandarasi yupo site, Serikali haijapeleka fedha mpaka leo. Hebu awaambie wananchi wa Kata ya Mtwango, ni lini Serikali itapeleka fedha kwenye kata ile?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, naishukuru Serikali kwa kutenga bilioni 2.67 kwa ajili ya Miradi ya Igowole, Mtambula, Nyololo, Idunda na Itandula. Sasa, je, Naibu Waziri, ni lini atakuja katika Jimbo la Mufindi Kusini awaeleze haya aliyoeleza leo Bungeni? Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana kwa kazi kubwa anayoifanya na amekuwa na usumbufu mkubwa sana kuhusu suala zima la maji katika Jimbo lake. Naendelea kusema sisi Wizara ya Maji na kwa kuwa siyo Wizara ya Ukame, nataka nimwambie Katibu wangu Mkuu ndani ya mwezi huu tutapeleka fedha wananchi wako waweze kupata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kuhusu mimi kwenda Mufindi, nipo tayari, baada ya Bunge tuongozane na Mheshimiwa Mbunge twende tukazungumze na wananchi wake. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MENDRAD L. KIGOLA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itamaliza ujenzi wa miundombinu ya maji katika Kata za Igowele, Nyololo, Mninga, Mtambula, Nyigo na Idunda?

Supplementary Question 2

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabisa natambua uwepo wa Simba hapa ndani, lakini pia niwaombe watoe tofauti zao na zetu ili waweze kuwaombea Yanga waweze kufanya vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu linasema hivi, kwa kuwa kuna skimu kubwa ya umwagiliaji kule Mahenge, Mgambilenga, je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kutembelea mradi ule kwa sababu ni muda mrefu sasa haujafanyiwa kazi kwa sababu fedha nyingi zilikuwa zinatoka nje ya nchi?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nipo tayari na nadhani katika ziara nitakayokwenda Mufindi nitapita katika Jimbo la Mheshimiwa Mbunge. Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.