Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Oran Manase Njeza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbeya Vijijini

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Barabara Kuu ya kwenda nchi jirani ya Zambia imepita katikati ya makazi ya watu na sehemu za biashara hasa katika Mji Mdogo wa Mbalizi na barabara hiyo inatumiwa na magari ya mizigo ambayo mara nyingi huwa ni chanzo cha ajali. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara mpya ili kuhakikisha ajali zinapungua?

Supplementary Question 1

MHE. ORAN M. NJEZA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, nina imani wahanga wengi akiwemo ndugu yangu Mheshimiwa Dkt. Mary Mwanjelwa atakuwa amefurahishwa sana na majibu haya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Bandari yetu ya Dar es Salaam ina ushindani mkubwa sana kutoka Bandari za Angola, South Africa pamoja na Msumbiji.
Mheshimiwa Mwenyekiti, je, ni lini Serikali itajenga Bandari ya Inyara ikiwa ni pamoja na reli ya kutoka Mbeya kwenda Ziwa Nyasa ili kukabiliana na ushindani huu wa kibiashara ambao ni karibu asilimia 70 ya biashara ya nje kutoka Bandari ya Dar es Salaam kwa mizigo inayokwenda nchi za nje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, ni lini Serikali itajenga kwa kiwango cha lami barabara ya Mbalizi - Shigamba - Isongole na barabara ya Mbalizi - Makongorosi ambazo ni barabara za kimkakati na ilikuwa ni ahadi ya Rais wa Awamu ya Nne na Rais wetu wa Awamu ya Tano?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niruhusu nimpe pongezi nyingi Mheshimiwa Mbunge Oran kwa kufuatilia mambo mbalimbali kwa sababu nafahamu anafuatilia masuala ya barabara, Uwanja wa Ndege wa Songwe, bandari kavu kama alivyouliza, lakini mambo muhimu kama ya kilimo na wachimbaji wake wadogo wadogo na mara nyingi tunapokea ushauri wake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kujibu swali lake la kwanza kuhusu ujenzi wa bandari kavu hususan eneo la Inyara, niseme tu kwamba Serikali inafanya maandalizi muhimu kwa ajili ya ujenzi wa hii bandari kavu ikiwa ni pamoja na kutenga eneo la heka 108 kwa ajili ya ujenzi huo. Eneo hili tumelitazama kimkakati kwa kweli kwa maana ya kuangalia ile chain supply yaani kuwa na mnyororo wa muunganiko kwa maana kwamba eneo hili linapakana na barabara inayotoka Mbeya au Kyela kwenda Malawi pia iko kandokando ya reli ya TAZARA.
Kwa hiyo, nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tumejipanga kwa ajili ya kuboresha bandari hii na hatua ambayo tuko nayo ni kufanya tathmini ya maeneo ya wakazi wanaopitiwa na mradi huu ili tuweze kuwalipa fidia na harakati zingine zitakazofuata kwa ajili ya ujenzi wa bandari hii kavu ziwezi kuendelea.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu barabara ya Mbalizi - Shigamba na barabara ya Mbalizi - Makongorosi ni barabara ambazo tumezizingatia pia katika bajeti yetu hii kwa maana ya kuziboresha. Mheshimiwa Mbunge anatambua kwamba tumetenga fedha nyingi kuboresha barabara hizi ili ziendelee kupitika wakati wote, wakati tunazitazama kwa ajili ya kuziboresha kwa kiwango cha lami.

Name

Richard Mganga Ndassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sumve

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Barabara Kuu ya kwenda nchi jirani ya Zambia imepita katikati ya makazi ya watu na sehemu za biashara hasa katika Mji Mdogo wa Mbalizi na barabara hiyo inatumiwa na magari ya mizigo ambayo mara nyingi huwa ni chanzo cha ajali. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara mpya ili kuhakikisha ajali zinapungua?

Supplementary Question 2

MHE. RICHARD M. NDASSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri kwamba barabara ya kutoka Magu (Ilungu) – Nkalalo – Ngudu - Hungumalwa ni barabara muhimu sana katika kuleta uchumi kwa maeneo yale na imeshafanyiwa usanifu wa kujengwa kwa kiwango cha lami. Je, ni lini sasa barabara hiyo itajengwa kiwango cha lami?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Mbunge kwani amekuwepo katika Bunge hili muda mrefu na naamini kabisa hata hii hatua ya barabara hii kusanifiwa na kupata michoro ni pamoja na juhudi zake mwenyewe. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Ndassa tuendelee kuwasiliana kuifuatilia barabara hii.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme kwamba Serikali ilikuwa inafanya juhudi kubwa sana za kuunganisha mikoa. Baada ya kuwa sasa tumekuwa na hatua nzuri, naamini tutaendelea kutafuta fedha na muda siyo mrefu barabara hii ya Ilungu – Ngudu – Hungumalwa tutaweza kuitafutia fedha ili tuweze kuijenga kwa kiwango cha lami. Kwa hiyo, nimuombe tu uvute subira yeye na wananchi wake muda siyo mrefu tutaipatia ufumbuzi barabara hii.

Name

Eng. James Fransis Mbatia

Sex

Male

Party

NCCR-Mageuzi

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. ORAN M. NJEZA aliuliza:- Barabara Kuu ya kwenda nchi jirani ya Zambia imepita katikati ya makazi ya watu na sehemu za biashara hasa katika Mji Mdogo wa Mbalizi na barabara hiyo inatumiwa na magari ya mizigo ambayo mara nyingi huwa ni chanzo cha ajali. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga barabara mpya ili kuhakikisha ajali zinapungua?

Supplementary Question 3

MHE. JAMES F. MBATIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Swali la msingi linasema pia vyanzo sababishi ni ajali na ajali nyingi zimekuwa zikitokea kwa uzembe. Sasa niulize Serikali, Kitengo cha Kupambana na Majanga yaani Risk Management katika Wizara ambapo kuna known risk, known-unknown risk and unknown–unknown risk lakini ajali nyingi zinasababishwa na known-known risk ambazo tunajitakia sisi binadamu. Sasa Serikali ni kwa kiasi gani inaimarisha Kitengo cha Risk Management kitaalamu na kibajeti ili kiweze kupunguza vyanzo vya ajali hizi ambapo maisha ya binadamu hayana thamani?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi kama Serikali tunatambua kwamba kumekuwa na ajali nyingi na hizi tumezizungumza sana kwenye Baraza la Usalama Barabarani. Ziko hatua kabambe nyingi ambazo zinachukuliwa na Serikali ili kuhakikisha kwamba ajali hizi zinapungua. Kwa kipindi hiki kifupi ajali zimepungua lakini tunapenda tuendelee kuzipunguza zaidi na zaidi. Nafikiria tunajaribu kutazama muundo wa Baraza hili sasa ili kuwa na mechanism nzuri ya kuhakikisha kwamba tunazitambua vizuri hizi risk ambazo zipo ili tuweze kuzishughulikia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niseme tu suala la kupunguza ajali ni letu sisi wote. Kwa hiyo, nitoe tu ombi kwa Waheshimiwa Wabunge tuendelee kushauri wanaotumia vyombo, madereva wetu, madereva wa bodaboda ili wakati Serikali inachukua hatua ni vyema wote tuwe pamoja ili kuhakikisha kwamba tunatoa hamasa, tunatoa elimu na kuwafanya watumiaji wote wa vyombo waweze kutumia barabara vizuri. Pamoja na watumiaji wa miguu, hatari ziko nyingi tunaziona katika majiji na maeneo mbalimbali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tushirikiane ili tuhakikishe kwamba ajali zinapungua na kama ikiwezekana tuziondoe kabisa.