Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Jimbo la Segerea ni kati ya majimbo yaliyosahaulika katika miundombinu ya barabara na kupelekea mitaa mingi kuwa na madimbwi sugu na mafuriko kila mvua inaponyesha. Kadhia hii imepelekea barabara za mitaa kupitika kwa taabu na kupelekea foleni kubwa katika barabara ya Segerea mpaka barabara ya Mandela kwa kuwa ndiyo barabara pekee inayotumiwa na wananchi. Je, ni lini jimbo hili litatengewa bajeti kwa barabara zake za mitaa kwa kiwango cha lami, changarawe na ujenzi wa mifereji?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nadhani waliomwandikia Mheshimiwa Naibu Waziri hawakunielewa vizuri. Swali langu nimeuliza hivi, ni kwa kiwango gani barabara za mitaa ina maana kutoka barabara ya Segerea kwenda Mandela road tutaweza kupunguza foleni. Kwa maana tutafungua vipi barabara za mtaa?
Mheshimiwa Mwenyekiti, wameainisha kwamba wametenga fedha ya ujenzi wa barabara kutoka Barakuda
- Chang’ombe, sasa ukitoka Barakuda - Chang’ombe bado hawajapunguza foleni. Wangesema kutoka Barakuda - Chang’ombe - Kimanga ili wananchi wapite Kisiwani wasiingie Mandela road. Vivyo hivyo kutoka Kinyerezi - Kimara watu waingie Morogoro road wasirudi barabara ya Segerea, tuna changamoto sana ya foleni. Vivyo hivyo …
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali ni lini barabara ya Segerea itapunguziwa foleni kwa kuboresha barabara za mitaa zinazotoka na siyo kurudi barabara kwenye moja? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, wamesema wametenga fedha kwa ujenzi wa daraja wa Tabata Kisiwani. Namwomba Naibu Waziri aje tumuonyesha daraja hilo kwa sababu lina changamoto kubwa. Matajiri wamevamia eneo, daraja haliwezekani kwa sababu mkondo ni mdogo. Ni lini atakuja kuona changamoto ili kuwaondoa wale watu tuweze kujenga daraja pale? Vinginevyo ni kupoteza fedha.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimeeleza barabara ambazo zinatengenezwa na tafsiri yake ni nini? Mwananchi ambaye alikuwa anataka kwenda Segerea ana-option ya kutumia barabara ya zingine na ambacho kimekuwa kikitokea ni kwamba hizi barabara zikiwa mbovu sana hata ambaye angeweza kupita kwa Mnyamani hawezi kupita.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kadri barabara hizi zingine zinavyotengenezwa inampa nafuu mwananchi wa maeneo hayo. Si kwamba gari zote ambazo zinazopita huko wanataka ni kwa sababu barabara za mtaani zinakuwa siyo nzuri. Aidha, kwa Jiji la Dar es Salaam kuna mpango kabambe wa kuhakikisha kwamba tunali-decongest, mpango uko vizuri, naomba Mheshimiwa Mbunge avute subira hilo liko mbioni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusiana na daraja ambalo analizungumzia na kuuliza nitakwenda lini, weekend iliyopita nilienda nikafika mpaka Mnyamani bahati mbaya tu Mheshimiwa Mbunge hakuwa na taarifa. Mimi niko tayari kwenda kwa kadri nafasi itakavyoruhusu ili tukatizame site kuona nini kilichopo ili tuweze kushauri vile ambavyo inatakiwa.

Name

Mussa Azzan Zungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ilala

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Jimbo la Segerea ni kati ya majimbo yaliyosahaulika katika miundombinu ya barabara na kupelekea mitaa mingi kuwa na madimbwi sugu na mafuriko kila mvua inaponyesha. Kadhia hii imepelekea barabara za mitaa kupitika kwa taabu na kupelekea foleni kubwa katika barabara ya Segerea mpaka barabara ya Mandela kwa kuwa ndiyo barabara pekee inayotumiwa na wananchi. Je, ni lini jimbo hili litatengewa bajeti kwa barabara zake za mitaa kwa kiwango cha lami, changarawe na ujenzi wa mifereji?

Supplementary Question 2

MHE. MUSSA A. ZUNGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwanza nichukue nafasi hii kumpongeza Mbunge wa Segerea, Mheshimiwa Bonnah Kaluwa kwa kazi nzuri za miundombinu anazofanya kwenye jimbo lake. Hivi karibuni alikuwa na ziara na Waziri wa Ujenzi kutazama miundombinu kwenye jimbo lake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na Segerea na Mkoa wa Dar es Salaam, naomba kujua ni lini sasa Serikali itaweka mkazo kwenye barabara za Jimbo la Ilala ambalo ndilo linabeba magari yote kutoka maeneo yote ya Mkoa wa Dar es Salaam? (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze Naibu Waziri, TAMISEMI kwa majibu yake mazuri.
Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze sana Mheshimiwa Zungu kwa kufuatilia kwa pamoja na maeneo mengine. Kama alivyosema nimekuwa na ziara Segerea Jumamosi, nimezitembelea barabara ambazo pia ziko chini ya TARURA ili kuweza kuona changamoto zilizopo ili kwa upande wa Serikali tuweze kuona namna sahihi ya kuweza kuzitatua. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini niseme tu kwa maana ya kupunguza msongongamano katika Jiji la Dar es Salaam hususani Ilala, kama tulivyopitisha bajeti tunaendelea na ule mkakati wa kupunguza msongamano. Tutakuwa na BRT III na IV lakini pia ipo mbioni BRT V na VI ili hatimaye msongamano katika Jiji la Dar es Salaam uweze kuondoka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Mheshimiwa Mbunge avute subira na wakati mwingine tunaweza kupeana mrejesho ili aone namna tulivyojipanga. Kwa kweli BRT I na II imefanya vizuri na imekuwa na rekodi nzuri kitaifa na watu na mashirika mengi yapo tayari kuja ku-support tutakwenda mpaka BRT V na VI.

Name

Abdallah Ally Mtolea

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza:- Jimbo la Segerea ni kati ya majimbo yaliyosahaulika katika miundombinu ya barabara na kupelekea mitaa mingi kuwa na madimbwi sugu na mafuriko kila mvua inaponyesha. Kadhia hii imepelekea barabara za mitaa kupitika kwa taabu na kupelekea foleni kubwa katika barabara ya Segerea mpaka barabara ya Mandela kwa kuwa ndiyo barabara pekee inayotumiwa na wananchi. Je, ni lini jimbo hili litatengewa bajeti kwa barabara zake za mitaa kwa kiwango cha lami, changarawe na ujenzi wa mifereji?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH A. MTOLEA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Tatizo lililopo katika Jimbo la Segerea linafanana pia na lililopo katika Jimbo la Temeke ambapo katika Kata za Buza, Tandika na Kata 14 Temeke barabara zimeharibika sana na hasa baada ya mvua hizi. Kwa kuwa kata hizi hazipo katika ule mpango DMDP, nilitaka kujua Serikali ina mpango gani kwenda kukarabati barabara za mitaa katika kata hii angalau kwa kiwango cha changarawe?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni ukweli usiopingika kwamba baada ya mvua kunyesha maeneo mengi miundombinu yake imeharibika na hasa kwa Jiji la Dar es Salaam ambapo mvua zimenyesha nyingi sana.
Naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafanya tathmini ya uharibifu uliotokea ili tujue hatua za dharura za kuchukua ili wananchi waendelee kutumia barabara katika hali nzuri.