Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Martin Alexander Mtonda Msuha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbinga Vijijini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya mapitio ya mipaka ya baadhi ya maeneo kama vile mikoa, wilaya na majimbo ya uchaguzi kwani baadhi ya mipaka ya maeneo hayo yana muingiliano unaoleta ugumu wa utoaji wa huduma za jamii? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuligawa Jimbo la Mbinga Vijijini kwa kuzingatia ukubwa wake wa kata 29?

Supplementary Question 1

MHE. MARTIN M. MSUHA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali. Hata hivyo, nitakuwa na maswali mawili madogo ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, wataalam wakati wa kuweka mipaka katika baadhi ya maeneo wamekuwa wakishirikisha upande mmoja badala ya kushirikisha pande zote mbili na hivyo kusababisha migogoro ya mipaka katika maeneo hayo hususani mipaka ya vijiji vyetu. Je, nini kauli ya Serikali ili kuondoka na tatizo hilo?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kule Jimboni kwetu Mbinga Vijijini kuna migogoro ya mipaka kati ya Vijiji vya Kilagano, Lugagala na Liganga ambavyo vipo Jimbo la Peramiho, Songea Vijijini. Upande mwingine mgogoro huo unasisha Kijiji cha Litumbandyosi, Mabuni pamoja na Luhugara kwa upande wa Jimbo la Mbinga Vijijini. Je, lini Serikali itashuka ili kwenda kutatua mgogoro huo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la kwanza kwamba wataalam wamekuwa hawashirikishi pande zote zinazohusika kwenye maeneo ya utawala, hilo ni tatizo na tumeshawapa maelekezo kwa sababu ya migogoro ambayo imesababishwa na kadhia hiyo. Hapa nchini tunayo jumla ya migogoro 366 ambayo imeibuliwa na Kamati ile ya Pamoja ya Wizara mbalimbali ambayo sasa hivi inashughulikiwa. Sasa hivi tumeshawaelekeza wataalam wetu wale wanaoratibu, wakienda kwenye eneo lolote watakapoanza upimaji upya lazima washirikishe pande zote mbili au pande zote zinazohusika.
Mheshimiwa Mwenyekiti, katika swali lake la pili kuhusu migogoro inayoendelea chini ya uratibu wa Wizara ya Ardhi kitaifa, migogoro yote nchini imeanza kushughulikiwa tangu mwezi Aprili, 2018 na tunaimani mpaka mwisho wa mwaka huu migogoro yote itakuwa imeshughulikiwa ile ya kijiji kwa kijiji, kata kwa kata, wilaya kwa wilaya, mkoa kwa mkoa, maeneo ya wananchi na maliasili na maeneo mengine yote ambayo yana migogoro tuna imani kwamba mpaka mwisho mwa mwaka huu yatakuwa yametatuliwa. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Dr. Mary Michael Nagu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya mapitio ya mipaka ya baadhi ya maeneo kama vile mikoa, wilaya na majimbo ya uchaguzi kwani baadhi ya mipaka ya maeneo hayo yana muingiliano unaoleta ugumu wa utoaji wa huduma za jamii? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuligawa Jimbo la Mbinga Vijijini kwa kuzingatia ukubwa wake wa kata 29?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. MARY M. NAGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba kuuliza, hivi haionekani kwamba wanapokuja wataalam wa TAMISEMI kugawa upya vijiji na hata vitongoji wanaleta migogoro ambayo haiishi na maendeleo kusitishwa? Je, Waziri anasema nini kwa migogoro ambayo ipo na imewadhuru watu ambao wako kwenye maeneo hayo?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye maswali ya nyongeza ya muuliza swali la msingi, migogoro yote inashughulikiwa isipokuwa kuna baadhi ya maeneo ambayo kulikuwa na matatizo ya usajili wa vijiji na vitongoji ambapo baada ya kupitia upya taratibu imeonekana kwamba kuna baadhi ya maeneo taratibu zilikiukwa.
Kwa hiyo, kule ambako taratibu zilikiukwa, pengine usajili wa kijiji au kitongoji ulipenyezwa bila kufuata utaratibu rasmi wa Serikali, maeneo hayo baadaye yamefanyiwa marejeo ya kufuta usajili wa kijiji au kitongoji. Kwa hiyo, suala hilo likishafanyika inakuwa siyo mgogoro tena. Kwa hiyo, nimuombe Mheshimiwa Mbunge kama kuna migogoro ya aina hiyo basi tuwasiliane ofisini kwa Katibu Mkuu wa TAMISEMI ili kuweza kufuatilia vizuri zaidi na kurekebisha.

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya mapitio ya mipaka ya baadhi ya maeneo kama vile mikoa, wilaya na majimbo ya uchaguzi kwani baadhi ya mipaka ya maeneo hayo yana muingiliano unaoleta ugumu wa utoaji wa huduma za jamii? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuligawa Jimbo la Mbinga Vijijini kwa kuzingatia ukubwa wake wa kata 29?

Supplementary Question 3

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili na mimi niweze kuuliza swali la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa matatizo ya Mbinga Vijijini yanafanana kabisa na matatizo ya Jimbo la Mbagala katika Mkoa wa Dar es Salaam. Jimbo la Mbagala sasa hivi lina watu takribani watu 1,100,000. Idadi hii ya watu ni kubwa sana kiasi kwamba utoaji wa huduma katika jimbo hili unakuwa mgumu na miundombinu inaharibika mara kwa mara kutokana na wingi wa watu waliopo katika eneo hilo. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuligawanya Jimbo hili la Mbagala ili liweze kufikika na hata Mbunge aweze kutoa huduma zake kwa wakati?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza huyu ni ndugu yangu kabisa katika ukoo. Ni kweli Jimbo la Mbagala kwa idadi ya watu ni miongoni mwa majimbo yenye watu wengi ikiwemo Temeke na majimbo mengine hasa ya Dar es Salaam, lakini hivi karibu tumegawa majimbo ya Dar es Salaam. Kwa hiyo, nashauri kwa vigezo vile ambavyo nimevizungumza kwenye jibu la msingi, naomba sasa Halmashauri ya Manispaa ya Temeke wakae ili waweze kupendekeza, lakini wapeleke mapendekezo yao moja kwa moja Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. MARTIN M. MSUHA aliuliza:- (a) Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya mapitio ya mipaka ya baadhi ya maeneo kama vile mikoa, wilaya na majimbo ya uchaguzi kwani baadhi ya mipaka ya maeneo hayo yana muingiliano unaoleta ugumu wa utoaji wa huduma za jamii? (b) Je, Serikali ina mpango gani wa kuligawa Jimbo la Mbinga Vijijini kwa kuzingatia ukubwa wake wa kata 29?

Supplementary Question 4

MHE. DANIEL N. NSANZUGWANKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nami nina swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, ugawaji wa maeneo ya utawala ngazi ya kata, tarafa na mitaa yaliyokosewa sana au kusahaulika katika Wilaya ya Kasulu. Unakuta kijiji kimoja chenye wakazi 10,000 ni mtaa mmoja, kijiji chenye wakazi 12,000 ni mtaa mmoja. Nina mifano halisi, kwa mfano wa Kijiji cha Nyantale ni kimoja na mtaa ni huo huo. Je, maeneo yaliyokosewa na kusahaulika ni lini sasa TAMISEMI wanakwenda kurekebisha kasoro hizo kwa sababu hazihitaji miundombinu wala uwekezaji wowote?

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPH G. KAKUNDA): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikiri kwamba kuna baadhi ya maeneo wakati wa kutenga maeneo hayo yaliyokosewa, vigezo havikuangaliwa vizuri. Kwa sasa hivi kulingana na payroll iliyopo Serikalini ambayo bado tunaendelea kuirekebisha itakuwa vigumu sana ndani ya miaka hii miwili kumuahidi kwamba tutarekebisha mwaka ujao au mwaka 2020. Naomba sana wananchi katika maeneo hayo waweze kuwa na uvumilivu, kwa nchi nzima zoezi hilo litafanyika baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.