Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sebastian Simon Kapufi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Mjini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha inasambaza pembejeo kwa wakati na kwa kuzingatia msimu na jiografia ya maeneo husika?

Supplementary Question 1

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, bila kuathiri wajibu wa Serikali wa kuratibu, ni kwa nini kusiwe na soko huria la mbolea kwa sababu haipatikani kwa wakati?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, wakati watu wanaongezeka, ardhi hususan inayofaa kwa kilimo haiongezeki. Nini mkakati wa Serikali wa kuja na mkakati mpya wa kuratibu kilimo chenye tija katika eneo dogo? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza ninampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa sababu ameuliza swali ambalo pia linaendana na Wabunge wote hususan wale wanaotoka katika majimbo ya mijini, naye ni Mbunge wa mjini, hususan kuhusu kwamba watu wanaongezeka lakini ardhi haiongezeki.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nilieleze Bunge lako tukufu kwamba sisi kama Serikali tumejipanga kuongeza uzalishaji na teknolojia ya hali ya juu. Vilevile lengo letu kubwa ni kuhakikisha kwamba wakulima hawa siyo tu kwamba wanalima kilimo cha kujikimu lakini vilevile kiwe ni kilimo cha kibiashara. Naasa kila Halmashauri zote nchini ziweze kuwa na zile green houses. Kilimo kile kinalimwa katika sehemu ndogo lakini uzalishaji wake unakuwa ni mkubwa.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la kwanza ni kwamba soko huria Serikali kazi yetu ni kuratibu, ku-control na ku-regualte, kwa maana hiyo, kwenye mbolea soko huria lipo, isipokuwa katika zile mbolea za DAP pamoja na Urea kwa maana ya kupandia na kukuzia, hiyo sisi kama Serikali kama tulivyosema ni kwamba Jumapili tutatoa semina kwa Waheshimiwa Wabunge ili waweze kuwa na uelewa mpana na wa pamoja kuhusu nini maana ya bei elekezi. Vilevile mbolea kuanzia sasa ziweze kufika kwa wakati na ziweze kuenea kwenye maeneo yote ya vijiji ili iwe kama soda na sukari. Ahsante.

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. SEBASTIAN S. KAPUFI aliuliza:- Je, ni lini Serikali itahakikisha inasambaza pembejeo kwa wakati na kwa kuzingatia msimu na jiografia ya maeneo husika?

Supplementary Question 2

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa Mkoa wa Katavi unazalisha mazao ya kilimo ya biashara na chakula, nini mkakati wa Serikali wa kuwasaidia wakulima hawa ambao wamejitolea, wanafanya kazi kwa bidii lakini tatizo kubwa ni ukosefu wa masoko kwa mazao wanayozalisha? Nataka kupata…

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusu mazao ya chakula na mazao yale ya kimkakati ya biashara sisi tumesema kama Serikali hatufanyi biashara, kazi yetu ni ku-regulate na ku-control. Isipokuwa kama Serikali, sisi kuanzia sasa tunatoa vibali ili wakulima wote wawe na uhuru wa kuweza kuuza bidhaa zao zote au mazao yao yote nje ya nchi lakini kwa kuhakikisha kwamba pia kama Serikali tuna chakula cha kutosha ndani ya nchi.