Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Josephine Tabitha Chagulla

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Kumekuwepo na tatizo kubwa la ukosefu wa maji safi na salama katika Mkoa wa Geita pamoja na Wilaya zake kama Bukombe, Chato, Mbogwe na Nyang’hwale. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hilo la maji kwa wananchi wa Mkoa wa Geita na Wilaya zake?

Supplementary Question 1

MHE. JOSEPHINA T. CHAGULA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri na ya kujitosheleza. Nina maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa mahitaji ya maji katika Mji wa Geita na vitongoji vyake ni makubwa mno ukilinganisha na maji tunayopata; mahitaji halisi ni lita milioni 15 kwa siku, lakini maji tunayopata ni lita milioni nne kwa siku. Kwa hiyo, tuna upungufu wa lita milioni 11 ambayo ni sawa na asilimia 29 kwa siku. Je, Serikali haioni kuna haja sasa ya kuongezea nguvu na uwezo Mradi wa Ziwa Victoria ili tuweze kupata maji ya kutosha kulingana na mahitaji yetu? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kuna mradi wa maji katika Wilaya ya Nang’hwale. Mradi huu ni wa siku nyingi sana, hivi sasa ni miaka sita tangu uanzishwe, bado wananchi wanateseka wanahangaika kwa kupata maji. Naishukuru Serikali kwa kuweza kutenga shilingi bilioni moja kwa ajili ya maji katika Wilaya ya Nang’hwale, je, Naibu Waziri yuko tayari sasa kwenda Nang’hwale ili akajionee hali halisi ya mradi ule ambao sasa hivi ni miaka sita haujakamilika na wananchi wanaendelea kuteseka mpaka sasa? Ahsante. (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Chagula, yeye ni mama na anadhihirisha kwamba mama wajibu wake ni kuhakikisha familia inapata maji. Nimkumbushe kwamba Serikali tayari imeshatekeleza awamu mbili za Programu ya Kulinda Ziwa Victoria, awamu ya kwanza ilikamilika na awamu ya pili imekamilika Desemba, 2017.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa hivi tumeanza awamu ya tatu na katika awamu hii Mheshimiwa Chagula, tayari tumepanga kutekeleza miradi kutoa maji Ziwa Victoria kupeleka Ilemela, Buchosa, pale Geita, Katoro Buseresere. Pia tunatarajia haya maji tutapeleka hadi Mbogwe. Hili eneo la Mbogwe linaweza likapata maji kutoka eneo la Katoro, Buseresere au kutoka Msalala.
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, mradi huu utahusisha pia kupeleka maji Buhongwa, Sumve na Usagara. Majadiliano na wafadhili wakiwemo European Investment Bank, Benki ya Maendeleo ya Afrika, yanaendelea vizuri na pia tutahakikisha kwamba hili eneo la Geita Mjini ambao ni mkoa mpya nalo limeingizwa ili tuweze kuongeza kiwango cha maji katika hilo eneo.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusu Nyang’hwale, kwa bahati nzuri nimetembelea Nyang’hwale nikakuta ule mradi umekaa muda mrefu sana. Nilitoa maelekezo na kila siku tatu naongea na Mbunge wa Nyang’hwale ili awe ananipa progress nini kinaendelea. Ameniridhisha kwamba mkandarasi sasa yuko site. Na mimi sasa kwa sababu ameomba kwenda na Mheshimiwa Naibu Waziri, nampa kibali hapa hapa Mheshimiwa Mbunge aende naye. (Makofi/Kicheko)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JOSEPHINE T. CHAGULA aliuliza:- Kumekuwepo na tatizo kubwa la ukosefu wa maji safi na salama katika Mkoa wa Geita pamoja na Wilaya zake kama Bukombe, Chato, Mbogwe na Nyang’hwale. Je, Serikali ina mpango gani wa kumaliza tatizo hilo la maji kwa wananchi wa Mkoa wa Geita na Wilaya zake?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa matatizo ya Geita yanafanana kabisa na yale ya Wilaya ya Kigamboni na Mbagala katika Wilaya ya Temeke, pamoja na juhudi za Serikali za kuchimba visima virefu katika Kata ya Kisarawe II Wilaya ya Kigamboni, lakini wananchi wale hawana kabisa mtandao wa maji safi na salama.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuweka mtandao wa maji safi na salama katika Wilaya ya Kigamboni na maeneo ya Mbagala? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza napenda kumpongeza sana mama yangu, Mheshimiwa Mariam kwa namna ya kipekee anavyowapigania wananchi wake, lakini kubwa mimi kama Naibu Waziri nilipata kibali cha kufanya ziara katika Mkoa wa Dar es Salaam na moja ya maeneo ambayo nilifanya ziara ni eneo la Kigamboni, Temeke na maeneo mengine. Ni kweli zipo changamoto katika suala zima la maji, hususan pembezoni mwa Dar es Salaam.
Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Wizara ya Maji tumechimba visima 20 pale Mpera na Kimbiji katika kuhakikisha tunatatua tatizo hili la maji, lakini visima vile bado havijafanyiwa utandazaji. Sisi kama Wizara tumeona haja sasa ya kufanya phase one ili kuhakikisha wananchi wale wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza.
Kwa hiyo, Mheshimiwa mama yangu Mheshimiwa Mariam, sisi kama Wizara ya Maji na kwa kuwa siyo Wizara ya ukame, tupo tayari kuhakikisha wananchi wa Kigamboni wanapata maji safi, salama na yenye kuwatosheleza. (Makofi)