Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Risala Said Kabongo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Vwawa ambayo inatoa huduma kwa Halmashauri nne za Mbozi, Ileje, Songwe na Momba inakabiliwa na upungufu wa vifaatiba, wodi, watumishi pamoja na Madaktari Bingwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kupandisha hadhi Hospitali ya Vwawa kuwa Hospitali ya Mkoa ili iweze kutengewa bajeti ya kutosha kukabiliana na changamoto zilizopo sasa?

Supplementary Question 1

MHE. RISALA S. KABONGO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Nimesikia majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa idadi ya wagonjwa wanaotibiwa katika Hospitali ya Vwawa ni kubwa, out patient tu wanaotibiwa pale ni 150 mpaka 200 kwa siku. Je, Serikali kwa nini isijenge jengo kubwa la OPD ili kuweza kukidhi mahitaji ya wagonjwa wanaopata huduma kwa sasa? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, idadi ya wanawake wanaojifungua katika Hospitali ya Vwawa ni kuanzia 15 mpaka 20 kwa siku, huku vifo vya watoto kuanzia sifuri mpaka miezi 28 ni 180 kwa takwimu za2015. Je, Serikali ina mkakati gani wa haraka wa kuongeza Madaktari, Wauguzi na vifaa tiba ili kupunguza vifo vya akina mama na watoto katika Hospitali ya Vwawa na pia kupunguza vifo vya wananchi katika Mkoa wetu wa Songwe? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la msingi la Mheshimiwa Risala aliongelea suala zima la kuwa na Hospitali ya Rufaa na katika majibu ambayo tumetoa tunamhakikishia na taratibu za ujenzi zimeshaanza na pesa imeshapelekwa. Sasa katika swali lake la nyongeza anarudi tena katika ile hospitali ambayo tumesema kwamba itaendelea kuwa Hospitali ya Wilaya na kwa sasa hivi inatumika temporarily kama Hospitali ya Rufaa.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimwambie Mheshimiwa Mbunge, ni vizuri tuchague njia moja ya kupita, hatuwezi kuwa na mawili kwa wakati mmoja. Jitihada ambazo zinafanyika na Serikali za kuhakikisha kwamba inajengwa Hospitali ya Rufaa ikizingatia ramani ya Hospitali ya Rufaa ni vizuri tukaiheshimu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili anaongelea juu ya suala zima la vifo vya watoto na akina mama kutokana na upungufu wa madaktari. Naomba nimhakikishie na yeye alikuwepo wakati Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ya Utumishi akiwa anatoa takwimu juu ya tarajio la Serikali la kupata vibali kwa ajili ya kuajiri watumishi wa sekta ya afya na elimu, ni wajibu wa Serikali kuhakikisha kwamba tunaajiri watumishi wa kutosha ili kupunguza vifo vya mama na mtoto. (Makofi)

Name

Alfredina Apolinary Kahigi

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Vwawa ambayo inatoa huduma kwa Halmashauri nne za Mbozi, Ileje, Songwe na Momba inakabiliwa na upungufu wa vifaatiba, wodi, watumishi pamoja na Madaktari Bingwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kupandisha hadhi Hospitali ya Vwawa kuwa Hospitali ya Mkoa ili iweze kutengewa bajeti ya kutosha kukabiliana na changamoto zilizopo sasa?

Supplementary Question 2

MHE. ALFREDINA A. KAHIGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi nami niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Wilaya ya Bukoba Vijijini tuna tatizo la ma-engineer wa ujenzi na tulitengewa fedha za force account shilingi milioni 900 kwa ajili ya kutujengea Kituo cha Afya katika kata mbili, kata za Kishanje na Rubafu, lakini hatuna ma-engineer wa ujenzi. Tunajenga chumba cha mama na mtoto, mortuary na chumba cha Mganga katika kata hizo mbili.
Je, ni lini Serikali itatusaidia ma-engineer wa ujenzi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nikupongeze kwa Tulia Marathon mmefanya vizuri sana. Hongera sana. (Makofi)
Pia nampongeza sana Mheshimiwa Mama Kahigi kwa sababu amekuwa mfuatiliaji mzuri sana tokea alipokuwa Mjumbe wa Kamati ya TAMISEMI. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, tumesikia kilio hiki kwa sababu tunajua kwa Mkoa wa Kagera tulikuwa hatuna hospitali zile za Wilaya na ninyi mmeleta concern hizo kubwa na ndiyo maana mwaka huu wa fedha tunaenda kujenga hospitali tatu mpya kule Karagwe, Kyerwa pamoja na Bukoba Vijijini. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, tunapeleka infrastructure nyingi sana katika eneo hilo na suala zima la kupata wataalam tutaweka kipaumbele chetu, lengo kubwa ni kwamba vile vituo vya afya na hospitali ambazo tunaenda kuzijenga tuwe na wataalam wa kutosha kwa ajili ya kuweza kusimamia. Kwa hiyo, tunalichukua kwa ajili ya kwenda kulifanyia kazi. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. RISALA S. KABONGO aliuliza:- Hospitali ya Wilaya ya Vwawa ambayo inatoa huduma kwa Halmashauri nne za Mbozi, Ileje, Songwe na Momba inakabiliwa na upungufu wa vifaatiba, wodi, watumishi pamoja na Madaktari Bingwa. Je, Serikali ina mkakati gani wa kupandisha hadhi Hospitali ya Vwawa kuwa Hospitali ya Mkoa ili iweze kutengewa bajeti ya kutosha kukabiliana na changamoto zilizopo sasa?

Supplementary Question 3

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa uongozi wa Mkoa wa Arusha chini ya Mkuu wa Mkoa Ndugu Mrisho Gambo, anafanya jitihada mbalimbali za ujenzi wa vituo vya afya na zahanati katika Mkoa wetu wa Arusha. Mfano tu katika Jiji la Arusha kuna ujenzi wa Kituo kikubwa cha Afya cha Murieth pamoja na Hospitali ya Wilaya ya Arusha Mjini unaendelea. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nataka kufahamu, Serikali imejipanga vipi kutuletea watumishi mara tu vituo hivi vitakapokamilika? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba uniruhusu nichukue fursa hii kuupongeza Mkoa wa Arusha kwa kazi nzuri ambayo wanafanya katika suala zima la ujenzi wa vituo vya afya na hasa hicho Kituo cha Afya cha Murieth maana na mimi nimeenda kukitembelea, ni miongoni mwa Vituo vya Afya ambavyo vimejengwa vizuri.
Mheshimiwa Naibu Spika, ni azma ya Serikali kuhakikisha kwamba Vituo vya Afya vinapokamilika huduma ziweze kutolewa na hakuna Kituo cha Afya hata kimoja ambacho kitakamilika Serikali ikakosa kupeleka watumishi.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie, immediately baada ya kwamba Vituo vya Afya vyote vya Arusha na maeneo mengine vikishakamilika, Serikali itapeleka watumishi pamoja na vifaa ili huduma za afya ziweze kutolewa kama ambavyo Serikali imekusudia. (Makofi)