Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mahmoud Hassan Mgimwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize maswali mawili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri Mkuu mstaafu alipotembelea kwenye kijiji hiki alikuta tayari Serikali imeshaanza kutekeleza, lakini yalijitokeza mapungufu ambayo yalikuwa yanagharimu milioni 295,000,000 kwa ajili ya kujenga mifereji (main canal), kwa ajili ya kujenga vivuko vya watu na wanyama na kwa ajili ya kujenga vigawa maji kuelekea mashambani. Pia kumalizia na kuongeza eneo la mfereji lifike kilometa 2.2 na ndiyo maana Mheshimiwa Waziri Mkuu baada ya kuona hilo akaahidi kwa wale wananchi wa Nundwe kwamba niko tayari kutoa shilingi 295,000,000 mradi huu uweze kukamilika. Mradi huu ukikamilika utaajiri vijana…
Mheshimiwa Mwenyekiti, ninakwenda kwenye swali, utaajiri vijana walio wengi. Sasa swali langu hapa linasema lini hiyo shilingi 295,000,000 itatoka kusudi haya mambo ambayo tunayazungumza yaweze kutekelezwa Mheshimiwa Waziri? Hilo la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili nilikuwa namuomba sana Mheshimiwa Naibu Waziri au Waziri aje kwenye site aone hili jambo ambalo tunalizungumzia.

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge mzee wangu Mgimwa, lakini pia nitumie nafasi hii kumpongeza kwa kuchaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kilimo, Mifugo na Maji. Kwa hiyo kama Mwenyekiti wangu ahadi ni deni na sisi kama viongozi wa Wizara hii hatutokuwa kikwazo katika kuhakikisha tunakamilisha ahadi ile ambayo imetolewa na Waziri Mkuu Mstaafu, Mheshimiwa Mizengo Pinda.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu ahadi ya mimi kwenda kule katika jimbo lake, nipo tayari Mheshimiwa Mbunge na Mwenyekiti wangu kuongozana pamoja katika kuangalia hali halisi ya utekelezaji wa mradi ule ili hatimaye tuongeze jitihada kwa haraka. Ahsante sana. (Makofi)

Name

Ally Seif Ungando

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibiti

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 2

MHE. ALLY S. UNGANDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya swali la nyogeza. Kwanza sina budi kuwashukuru vyombo vyote vya ulinzi na usalama, Kibiti hali shwari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, wananchi wa maeneo ya Delta, Mbwela, Msala, Salale, Mapaloni, Kiongoloni wana shida kubwa ya maji ambayo sasa inapelekea hata ndoa kulegalega kwenye nyumba. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapatia maji safi na sala katika maeneo?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo la Delta tayari tumelifanyia utafiti na tumechimba visima kiasi. Ukienda zaidi ya mita tano unapata maji ya chumvi, kwa hiyo, sasa tunajaribu kuangalia mfumo mzuri ambao utahakikisha kwamba wananchi wa Delta wanapata maji bila shida, lakini ukienda mita nne tayari tumechimba visima wanapata maji safi na salama.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 3

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, matatizo yaliyopo huko kwenye jimbo Mheshimiwa Mgimwa yanafanana kabisa na matatizo yaliyopo katika jimbo langu ambapo Serikali imeonesha nia njema ya kujenga skimu ya umwagiliaji katika Bwawa la Itagata. Sasa kwa kuwa bwawa hili lilikuwa lilishaanza kuvuja na ile pesa ya kujenga skimu Serikali; maana ya Wizara ilituambia tutoe ili tuwape wale wakandarasi wa umwagiliaji kutoka Wizarani wa kuziba mabwawa; sisi pesa tumeshalipa.
Je, Serikali sasa iko tayari kurudisha ile pesa haraka ili na sisi certificate iliyioko kwenye halmashauri tuweze kumlipa mkandarasi katika Skimu ya Umwagiliaji ya Itagata? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, kwanza nimpongeze kwa jinsi anavyofuatilia shughuli za ujenzi wa mabwawa kwa ajili ya umwagiliaji na kweli Bwawa la Itagata limekamilika. Naomba Mheshimiwa Mbunge baada ya kikao hiki leo tukutane ili tuweze kuangalia jinsi ya kukupa hiyo fedha muende mkakamilishe miradi mingine inayoendelea.

Name

Hamidu Hassan Bobali

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Mchinga

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 4

MHE. HAMIDU H. BOBALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa fursa hii. Mheshimiwa Waziri amekuwa akija Mkoani Lindi mara kwa mara, zaidi ya mara mbili au tatu nimekutana naye kwa ajili ya mradi ule wa maji pale Napa. Lakini tuna Skimu ya Umwagiliaji iliyopo kwenye Jimbo la Mchinga, ya Kinyope na skimu nyingine iko Jimbo la Mtama kwa Mheshimiwa Nape, ya Kiwalala. Skimu hizi zilijengwa chini ya kiwango na hivi sasa hazifanyi kazi vizuri ingawa zilitumie pesa nyingi ya Serikali. Je, Waziri uko tayari kutuma wawakilishi wako au wewe mwenyewe kwenda kujionea kinachoendelea katika skimu hizo?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli skimu hizo zilitekelezwa, zilikumbwa na matatizo ya mafuriko lakini kwa sasa tayari tunazifanyia kazi ili ziweze kujengwa na kutimiza matakwa ambayo yalikuwa yanatakiwa kwa ajili ya kuwapatia wananchi huduma nzuri ya maji ili waweze kufanya kilimo cha umwagiliaji. Niko tayari kwenda kutembelea eneo hilo.

Name

Venance Methusalah Mwamoto

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 5

MHE. VENANCE M. MWAMOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la msingi lilikuwa linauliza habari ya ahadi za viongozi. Mheshimiwa Rais aliahidi pale Ilula, Kilolo kwamba suala la maji litakuwa ni historia. Nataka nijue Mheshimiwa Waziri ni lini mkataba ule utasainiwa ili wananchi wa Kilolo, Ilula tatizo la maji liwe historia kama alivyoahidi Mheshimiwa Rais?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kulikuwa na ahadi ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuhusu ujenzi wa mfumo wa maji Kilolo. Tulikuwa tunatarajia kwamba fedha ambazo zingetumika ilikuwa ni fedha kutoka Austria, lakini baada ya kuona kwamba fedha za Austria zinachelewa Serikali kwa kutumia makusanyo ya ndani imefanya mchakato imekamilisha na tarehe 30 Aprili, Jumatatu ijayo tunakwenda kutia saini mkataba ili sasa utekelezaji uanze wananchi wa Kilolo wapate maji. (Makofi)

Name

Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 6

MHE. HUSSEIN M. BASHE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nimshukuru Waziri kwa utekelezaji wa mradi wa visima katika Jimbo la Nzega. Naomba kujua mwaka 2015 moja ya hadi kubwa ya Mheshimiwa Rais ilikuwa ni kufufua skimu ya umwagiliaji katika Kijiji cha Idudumo katika Halmashauri ya Mji wa Nzega. Je, ni lini ahadi hii Serikali itaanza utekelezaji wake kwa ajili ya kulipitia na kulirekebisha bwawa hilo na kutekeleza ahadi hiyo?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru na napenda nijibu swali la Mheshimiwa Mbunge juu ni lini utekelezaji. Miradi ya utekelezaji wa umwagiliaji inategemeana na fedha. Fedha zitakapopatikana ka wakati na sisi tutatekeleza kwa wakati katika kuhakikisha mradi huu unakamilika. Ahsante.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MAHMOUD H. MGIMWA aliuliza:- Mheshimiwa Mizengo Pinda akiwa Waziri Mkuu mwaka 2013 aliahidi kuchangia shilingi 295,000,000 katika mradi wa umwagiliaji uliopo kijiji cha Nundwe, kata ya Ihalimba. Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo ili wananchi wa eneo hilo waweze kujikwamua kiuchumi?

Supplementary Question 7

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, wakulima wa vitunguu katika Tarafa ya Eyasi wanayo miundombinu ya umwagiliaji ambayo imejengwa na World Vision na fedha za DADPs na Shirika na Maendeleo la Jimbo Katoliki la Mbulu na Waziri Mkuu alikuja kuzindua. Tatizo kubwa si miundombinu kama ambavyo imeelezwa na Mbunge mmoja hapa, suala ni uhifadhi wa chanzo ambao wakulima wale wanatumia kumwagilia vitunguu vyao. Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhifadhi chanzo kile ili wananchi waweze kulima zao hilo? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Bonde la Eyasi linatumia chanzo cha maji ya mbubujiko kutoka chini ya ardhi eneo la Mang’ola. Nilikwenda kule na tayari tumeshaweka mipaka ili kuzuia wananchi wasifanye shughuli za kibinadamu karibu na vile vyanzo. Mipaka hiyo inaendelea kuwekwa na Mheshimwa Mbunge tuendelee kushirikiana, na kama utaona kwamba kuna kitu ambacho hakiendi vizuri, tuwasiliane. Lengo ni kuboresha ili yale maji yaendelee kutoka kila wakati.