Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mashimba Mashauri Ndaki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Magharibi

Primary Question

MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mabonde ya mpunga katika Vijiji vya Masela, Bukangilija na Mwatigi katika Wilaya ya Maswa yanaweza kuzalisha mpunga mwingi kuliko ilivyo hivi sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji katika maeneo hayo ili kuwawezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji?

Supplementary Question 1

MHE. MASHIMBA M. NDAKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mwaka jana niliuliza swali kuhusiana na bwawa la Mwamihanza nikaambiwa Serikali inatafuta fedha; mwaka huu pia nimeuliza juu ya miradi hii ya umwagiliaji kwenye vijiji hivi vitatu majibu ya Serikali ni kwamba bado Serikali inatafuta fedha. Sasa nataka kuiuliza Serikali, pesa itapatikana lini? Kwa sababu kwenye Bwawa la Masela usanifu ulishafanyika na watu walishaondolewa kwenye eneo ambalo bwawa litachimbwa. Sasa Serikali inapata pesa lini ili kuanza ujenzi wa Bwawa la Masela?
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili, Tume ya Taifa ya Umwagiliaji inapata pesa kidogo sana, ndiyo maana miradi mingi ya umwagiliaji inakwama. Mradi wangu wa Bukangilija umekwama wa Mwatigi umekwama wa Kulimi umekwama sasa ni lini Serikali itatenga kiasi cha fedha cha kutosha ili kushughulikia miradi ya umwagiliaji hapa nchini? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda nimpongeze kwanza Mheshimiwa Mbunge kwa namna anavyofanya kazi. Pili, amezungumzia kuhusu suala la uchache wa fedha na lini Serikali itatoa fedha. Pamoja na Serikali kutoa fedha lakini kupitia ziara tulizokuwa tumezifanya tumeona katika miradi mingi ya umwagiliaji kumekuwa na changamoto.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, tuna miradi ya zaidi ya 889 ambayo imejengwa lakini miundombinu yake haijakamilika, lakini la pili ipo miradi 54 ambayo imejengwa lakini haifanyi kazi kabisa. Kutokana na changamoto hiyo Waziri wangu akaona haja ya kupitia mpango kabambe wa mwaka 2002 wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji ili kuangalia namna gani tutaweza kutumia fedha ingawa kwa uchache lakini miradi iwe yenye tija. Nataka nimhakikishie kupitita mapitio haya tuliyoyafanya miradi ile ambao tumeiorodhesha na tumeibainisha ipo haja ya kutengeneza maaboreshe na ili hata kama miradi inatekelezawa lazima iwe miradi ambayo imekamilika kwa wakati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kuhusu miradi yake ambayo ameelekeza, katika miradi ambayo tumeanisha na yeye tutamuweka katika utekelezaji ili miradi iende kwa wananchi kama zamani. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mabonde ya mpunga katika Vijiji vya Masela, Bukangilija na Mwatigi katika Wilaya ya Maswa yanaweza kuzalisha mpunga mwingi kuliko ilivyo hivi sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji katika maeneo hayo ili kuwawezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na swali moja la nyongeza. Mji wa Kibondo unakaabiliwa na tatizo kubwa la ukosefu wa maji, na mji huo uko kilimani. Pampu zinazosukuma maji kusambaza ndani ya mji wa Kibondo zimechakaa, ni lini Serikali itapeleka pesa kwa ajili ya mradi wa maji Wilayani Kibondo?

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali moja la Mheshimiwa Mbunge Genzabuke kuhusiana na matatizo ya maji ya Kibondo, kwanza Mheshimiwa Genzabuke pamoja na wananchi wa Jimbo la Kibondo nikufahamishe tu kwamba tayari tunasaini mkataba wa mkopo wa fedha nafuu kutoka Serikali ya India na katika ya fedha hizo sehemu ya fedha itashughulikia utoaji wa maji, huduma ya maji katika mji wa Kibondo, kwa hiyo sasa hivi vuta subira mambo baada ya muda mfupi yatakuwa mazuri. (Makofi)

Name

Joseph Roman Selasini

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Rombo

Primary Question

MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mabonde ya mpunga katika Vijiji vya Masela, Bukangilija na Mwatigi katika Wilaya ya Maswa yanaweza kuzalisha mpunga mwingi kuliko ilivyo hivi sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji katika maeneo hayo ili kuwawezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji?

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH R. SELASINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Maji mengi sana ya mvua yanapotea katika nchi hii kiasi kwamba tungekuwa na utaratibu wa kuyavuna yangeweza kusaidia katika shughuli za umwagiliaji na shughuli za wanyama. Kwa mfano katika Jimbo langu la Rombo kuna mito ya msimu kama Ungwasi, Marwe, Tarakea, Uashi pamoja na Nana ambapo maji ya mvua ambayo yanakwenda nchini Kenya wale wameyazuia wanafanya nayo umwagiliaji halafu wanatuletea tena bidhaa huku kwetu.
Je, Mheshimiwa Waziri uko tayari utakapopata nafasi twende wote Rombo ukayaone haya mabonde ya mito hii ya msimu ili tuweze kuangalia uwezekano wa kuyazuia ili tuweze baadae kuyatumia kwa ajili ya umwagiliaji?

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge Selasini Mzee wangu, mimi kama Naibu wa Waziri wa maji nipo tayari baada ya Bunge twende pamoja Rombo ahsante sana. (Makofi)

Name

Catherine Valentine Magige

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mabonde ya mpunga katika Vijiji vya Masela, Bukangilija na Mwatigi katika Wilaya ya Maswa yanaweza kuzalisha mpunga mwingi kuliko ilivyo hivi sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji katika maeneo hayo ili kuwawezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji?

Supplementary Question 4

MHE. CATHERINE V. MAGIGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza; katika Wilaya ya Karatu mkoa wa Arusha kijiji cha Mang’ola kuna biashara kubwa ya kimataifa ya vitunguu ambapo robo ya mapato ya Halmashauri ya Karatu yanatokana na kilimo hiki cha vitunguu.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea mabwawa na mifereji ya umwagiliaji wananchi hawa wa Mang’ola ili kuongeza tija kuwainua kimaisha wananchi wa Karatu hasa akina mama waliowekeza katika kilimo hiki cha vitunguu? (Makofi)

Name

Jumaa Hamidu Aweso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Pangani

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu asilimia kubwa zaidi ya 70 wanaishi vijijini na wanategemea kilimo cha kudra za Mwenyezi Mungu kwa maana ya mvua. Kwa hiyo sisi kama Wizara ya Maji tukaona haja sasa ya kuwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji katika kuhakikisha kilimo chetu kinakuwa bora na tija katika suala zima la uzalishaji, kwa maana ya kupata malighafi za viwandani na hata katika suala zima la biashara. Nataka nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge sisi kama Wizara ya Maji hatutokuwa kikwazo katika kuhakikisha tunatengeneza miundombinu ya umwagiliaji eneo hilo ili wananchi wale waweze kunufaika na kilimo cha kisasa.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mabonde ya mpunga katika Vijiji vya Masela, Bukangilija na Mwatigi katika Wilaya ya Maswa yanaweza kuzalisha mpunga mwingi kuliko ilivyo hivi sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji katika maeneo hayo ili kuwawezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji?

Supplementary Question 5

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi na mimi naomba niulize swali dogo la nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tatizo lililopo Maswa Magharibi linafanana na la Mvomero, na kwa kuwa Mvomero kuna maji mengi, kuna mabonde mazuri sana na kwa kuwa wananchi wa Mvomero wamejipanga katika kilimo cha umwagiliaji, na kwa kuwa kuna ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Maji injinia Isack kwa kusaidia mabonde mawili, Bonde la Kigugu na Bonde la Mbogo, je, ni lini fedha zile zitatoka ili kuleta tija kwa wananchi wa Mvomero na Taifa kwa ujumla? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli katika bajeti ya mwaka huu wa fedha tumetenga fedha kwa ajili ya kuendelea na usanifu wa miradi ya Kigugu na usanifu umekamilika, wakati wowote Mheshimiwa Murad nikuhakikishie hatutaingia kwenye kutangaza tender kuhakikisha kwamba hiyo miradi imetekelezwa.

Name

Abdallah Majurah Bulembo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Primary Question

MASHIMBA M. NDAKI aliuliza:- Mabonde ya mpunga katika Vijiji vya Masela, Bukangilija na Mwatigi katika Wilaya ya Maswa yanaweza kuzalisha mpunga mwingi kuliko ilivyo hivi sasa. Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga mabwawa na mifereji ya umwagiliaji katika maeneo hayo ili kuwawezesha wakulima kuongeza tija katika uzalishaji?

Supplementary Question 6

MHE. ABDALLAH M. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu Dar es Salaam pale kwenye kulaza bomba la kutoka Bagamoyo kuja Chuo Kikuu kuna watu walivunjiwa na watu wengine wakakataa wakapelekwa mahakamani, walipopelekwa mahakani wameshindwa mpaka leo wanasema wanalindwa na wakubwa hawataki kuvunja nataka Wizara iniambie wanavunjiwa lini ili Dar es Salaam tupatae maji Chuo Kikuu? (Makofi)

Name

Eng. Isack Aloyce Kamwelwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Katavi

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wanayo taarifa kwa sababu wameshapewa notice kwamba wanavunjiwa, kwa hiyo ni wakati wowote hatua za kuvunja zile nyumba zitafanyika.