Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Machano Othman Said

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua dhidi ya wauzaji wakubwa wa dawa za kulevya wanaoingiza na kuuza badala ya kuakamata waathirika ambao wanahitaji misaada na ushauri nasaha wa kuachana na matumizi ya dawa hizo?

Supplementary Question 1

MHE. MACHANO OTHMAN SAID: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kwanza nimpongeze Mheshimiwa Waziri kwa jibu lake. Lakini pamoja na jibu hilo naomba kuuliza maswala mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Mwenyekiti, biashara hii ya dawa za kulevya ina mtandao mrefu, na katika mtandao huo wapo baadhi ya raia ya wa kigeni ambao wanaishi Tanzania wanajishirikisha na dawa hizi. Miaka miwili, mitatu, minne nyuma kuna mwanamke mmoja kutoka nchi jirani alikamatwa maeneo ya Mbezi beach na alikuwa akitumia passport nyingi na majina tofauti.
Je, Serikali ina mpango gani wa kukabiliana na wageni ambao wanaitumia Tanzania kwa uuzaji wa madawa ya kulevya?
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili, miongoni mwa waathirika wakubwa watumiaji wa dawa za kulevya ni wasanii wetu. Serikali ina mpango gani wa kuwasaidia wasanii hawa kuondokana na tatizo hili la utumiaji wa dawa za kulevya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la kwanza, sheria yetu haibagui wenyeji na ugeni. Inapotokea mtu yeyote anajihusisha na dawa za kulevya sheria yetu imekuwa ikitumika kwa kuhakikisha kwamba hatua stahiki zinachukuliwa na kufanya kitu ambacho kinaitwa deterrence ili kuwazuia watu wengine wasifanye biashara hii ya dawa za kulevya. Adhabu kali kali hutolewa na hatua stahiki huchukuliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuhusu kuwasaidia wasanii; katika mpango tulionao wa kuhakikisha kwamba tunatatua changamo hii ya dawa za kulevya ambayo inawaathiri vijana wengi ikiwemo nguvu kazi ya taifa hili, moja kati ya kazi kubwa tunayofanya ni kuendelea kutoa elimu juu ya madhara ya matumizi ya dawa za kulevya. Vilevile katika mpango mmoja wapo ni kuhakikisha kwamba tunafanya kitu kinaitwa supply reduction kuhakikisha kwamba madawa hawa hayapatikani na hivyo kutokuwalazimu vijana wengi zaidi kuweza kuyatumia. Tume imefanya kazi kubwa mpaka hivi sasa na wameendelea kukamata na kuteketeza dawa nyingi na hivi sasa kuna upungufu mkubwa sana wa dawa za kulevya katika viunga vya miji yetu mingi ya Tanzania kutokana na kazi kubwa ambayo inafanywa na tume.

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. USSI SALUM PONDEZA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua dhidi ya wauzaji wakubwa wa dawa za kulevya wanaoingiza na kuuza badala ya kuakamata waathirika ambao wanahitaji misaada na ushauri nasaha wa kuachana na matumizi ya dawa hizo?

Supplementary Question 2

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushuku kwa kuniona. Kumekuwa na malalamiko mengi ya waathirika wa dawa za kulevya wanapokuwa rehab (rehabilitation) wanakaribia kupona wahusika wanawachoma tena dawa ya kulevya ili wasiweze kutoka na lengo limekuwa ili waendelee kujipatia fedha.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuanzisha rehab zao wenyewe ili kuweza kuwasaidia waathirka hawa dawa za kulevya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer


NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA VIJANA NA WENYE ULEMAVU (MHE. ANTONY P. MAVUNDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, asilimia kubwa ya sober house zinamilikiwa na watu binafsi na hilo lililolalamikiwa na Mheshimiwa Mbunge hatujapata malalamiko rasmi. Hata hivyo niseme tu kwamba kwa kuzingati hizi sober house nyingi ziko chini ya watu binafsi tumeamua sasa kutengeneza miongozo ambayo itasaidia namna bora ya management ya hizi sober house ili inapotokea mazingira ya namna hiyo tuwe tuna sehemu ya kuweza kukabiliana nao, kwa sababu miongozo ile itakuwa inaeleza mtu ambaye ni muathirika wa madawa ya kulevya awe treated vipi. Mpango wa Serikali, katika swali lake, ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na sober house nyingi za Serikali ili kuondokana na changamo hii ambayo wananchi wengi wanaipata hasa kutokana na gharama kubwa ya kulipia katika hiyo sober house.

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WENYE ULEMAVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri Mkuu kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Tumepokea hii taarifa sasa mara kadhaa na hata wakati wa bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Waheshimiwa Wabunge wametuarifu kwamba uko mchezo mbaya unaoendelea kwenye sober house; badala kuwasaidia vijana wetu wapone na waondoke ndani ya sober house, lakini taarifa ambazo tumekuwa tukizipokea ni kwamba wamiliki wa sober house wanataka kuendelea kuwaweka vijana wetu pale kwa faida binafsi. Naomba sasa nitoe tena agizo kwa wamiliki wa sober house wote ambao wana mchezo huo ambao umekuwa ukisemekana wauache haraka.
Mheshimiwa Mwenyekiti, na ninatumia muda huu pia kuiagiza mamlaka sasa kuanza kufanya uchunguzi wa kina na atakaye bainika ana tabia hiyo aweze kuchukuliwa hatua haraka sana na hiyo itatusai kuwaokoa vijana wetu kutokuendea kutumia dawa za kulevya katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)