Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vicky Paschal Kamata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA aliuliza:- Kampuni kubwa za uchimbaji madini kama vile GGM, Buzwagi Gold Mine na North Mara Gold Mine licha ya kulipa kodi kwa Serikali kuu pia zinawajibika kuhudumia jamii inayozunguka migodi kwa utaratibu wa uwajibikaji kwa jamii kwa kutoa fedha au kufadhili miradi ya kijamii au maendeleo:- • Je, kwa mwaka 2017 Kampuni hizo kila moja ilitoa fedha kiasi gani? • Je, hadi kufikia Januari mwaka 2018, Kampuni hizo zimetoa kiasi gani.

Supplementary Question 1

MHE. VICKY P. KAMATA: Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri. Pamoja na majibu mazuri, nina swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa, GGM imekuwa ikitoa hili fungu la CSR kila mwezi kwa ajili ya kuhudumia hayo maeneo ambayo ameyataja katika maelezo yake ya msingi kwa maana ya elimu, afya, mazingira pamoja na wajasiriamali.
Mheshimiwa Spika, pia kwa kuwa, wamekuwa wakitoa kila mwezi hili fungu la CSR na kwa majibu haya inaonekana kwamba tangu Januari mpaka sasa GGM hawajatoa fungu hilo la CSR kwa maeneo hayo, nataka kujua kauli ya Serikali kwa wakati huu wa mpito kuhusiana na hawa waliokuwa wakisaidiwa na GGM kwa mfano, kituo cha Watoto Yatima cha Moyo wa Huruma wamekuwa wakisaidiwa pesa kila mwezi kwa ajili ya malazi ya wale watoto yatima, chakula, kuna mradi wa maji ambao kimsingi ni wa Serikali lakini GGM walikuwa bado wanaendelea kuutunza pamoja na ile hospitali inayotembea majini inayosaidia wanawake na watoto katika Visiwa kwa kuwa tangu Januari mpaka sasa pesa hazijatoka na imezoeleka kila mwezi huwa inatoka. Je, ni nini kauli ya Serikali katika kipindi hiki cha mpito?. Mheshimiwa Spika, ahsante.

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba baada ya marekebisho ya Sheria ya Madini ya mwaka 2010 na marekebisho yake ya mwaka 2017, tulisimamisha utoaji wa fedha hizi mpaka pale Baraza la Madiwani katika Halmashauri husika wakae, wakubaliane utekelezaji sawasawa wa miradi hiyo.
Mheshimiwa Spika, kwa hiyo GGM, pia nimeongea na RAS wa Mkoa wa Geita, ule mpango wa kupitia kwa Madiwani umeshakamilika na kuanzia leo wanaanza kuzitumia zile fedha kutokana na jinsi walivyokubaliana na Halmashauri husika. (Makofi)

Name

John Wegesa Heche

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA aliuliza:- Kampuni kubwa za uchimbaji madini kama vile GGM, Buzwagi Gold Mine na North Mara Gold Mine licha ya kulipa kodi kwa Serikali kuu pia zinawajibika kuhudumia jamii inayozunguka migodi kwa utaratibu wa uwajibikaji kwa jamii kwa kutoa fedha au kufadhili miradi ya kijamii au maendeleo:- • Je, kwa mwaka 2017 Kampuni hizo kila moja ilitoa fedha kiasi gani? • Je, hadi kufikia Januari mwaka 2018, Kampuni hizo zimetoa kiasi gani.

Supplementary Question 2

MHE. JOHN W. HECHE: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kuniona. CSR ipo kwa mujibu wa sheria, lakini hii migodi wamekuwa wakionyesha kama ni hisani fulani wanawapatia wananchi. Kwa nini sasa Serikali isiwaagize hizi pesa zipelekwe moja kwa moja kwenye Halmashauri na zisimamiwe na Madiwani wetu katika kutekeleza miradi hii, kwa sababu unaona gharama zinazoandikwa ni kubwa kweli ukilinganisha na kazi halisi ambazo zinakuwa zinafanyika, yaani ziende kama vile kodi zingine zinavyoenda lakini zikiwa specific kama CSR ili zisimamiwe na Baraza la Madiwani? (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO): Mheshimiwa Spika, ni kweli kabisa kwamba hesabu zinazoonekana ni hesabu kubwa sana zilizotumika kuliko miradi yenyewe ilivyo, hilo tunakubaliana kabisa. Nimepita baadhi ya maeneo kwa mfano, GGM na North Mara tumewaagiza kwanza watupe taarifa ya utekelezaji wa zile fedha zilizotengwa kwa miaka miwili iliyopita ili tujiridhishe tuone zile fedha zilizotengwa na wamepeleka wapi na nini kimefanyika. Hilo la kwanza.
Mheshimiwa Spika, jambo la pili, kwa sababu hizi fedha za corporate social responsibility huwa zinatolewa kutokana na jinsi wao wanavyotengeneza faida na kwa sasa hivi ni sheria lazima watoe zile fedha. Kwa hiyo, namwomba Mheshimiwa Mbunge kwa kushirikiana na Madiwani husika wakakae na zile Kampuni waamue kwamba watekeleze miradi ile kwa jinsi wao walivyoweka kipaumbele chao.
Mheshimiwa Spika, vilevile kuna fedha ambayo inakwenda moja kwa moja kwenye Halmashauri, fedha hiyo ni service levy ambayo ni asilimia 0.3 ya mauzo ya madini wanayoyapata. Kwa hiyo, nadhani tu kwamba tuendelee kutoa ushirikiano na sisi kama Wizara ambayo tunasimamia Sheria ya Madini tutahakikisha kwamba zile fedha zinazotengwa zinakwenda zinavyostahili na Madiwani wasimamie utekelezaji wa miradi ambayo wamejipangia. Mheshimiwa Spika, ahsante sana.

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Napenda kuongezea majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri wa Madini. Napenda kusema kwamba sheria ya sasa na kanuni kuhusiana na uwajibikaji kwa jamii ziko wazi.
Mheshimiwa Spika, niombe tu ushirikiano Waheshimiwa Wabunge pamoja na Halmashauri zetu za Wilaya na Miji waweze kutoa ushirikiano na kutupatia taarifa endapo wanaona kuna miradi imetekelezwa ipo chini ya viwango, lakini kiwango ambacho kimekuwa-declared ni kidogo kuliko fedha halisi ambayo inatamkwa kwamba imetumika.
Mheshimiwa Spika, pili; pamoja na maelezo aliyotoa Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba tumewataka GGM waweze kutoa maelezo na taarifa zao za miaka miwili, tutaenda kwa migodi yote ambayo imekuwa ikifanya uwajibikaji kwa jamii na tutapitia na kukagua na yeyote ambaye ataonekana alifanya udanganyifu, hatua kazi za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. VICKY P. KAMATA aliuliza:- Kampuni kubwa za uchimbaji madini kama vile GGM, Buzwagi Gold Mine na North Mara Gold Mine licha ya kulipa kodi kwa Serikali kuu pia zinawajibika kuhudumia jamii inayozunguka migodi kwa utaratibu wa uwajibikaji kwa jamii kwa kutoa fedha au kufadhili miradi ya kijamii au maendeleo:- • Je, kwa mwaka 2017 Kampuni hizo kila moja ilitoa fedha kiasi gani? • Je, hadi kufikia Januari mwaka 2018, Kampuni hizo zimetoa kiasi gani.

Supplementary Question 3

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Ni hivi juzi tu siku mbili, tatu zilizopita Wabunge wa Geita tumeletewa barua inayoonesha CSR iliyotolewa na GGM 2017/2018 dola 9,600,000 lakini katika majibu ya Waziri amesema ni dola milioni 6.5 na hizi barua ambazo tumeletewa tayari ziko kwa Mkuu wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya na baadhi ya wananchi wameshazipata, lakini kwa majibu ya Wizara ina maana tunachanganyikiwa tujue ipi ni sahihi na ipi siyo sahihi.
Mheshimiwa Spika, sasa ni nini kauli ya Wizara kuweza kuisaidia Halmashauri angalau kufanya auditing kujua uongo uko Wizarani au uongo uko mgodini. (Makofi)

Name

Stanslaus Haroon Nyongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Maswa Mashariki

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI (MHE. STANSLAUS H. NYONGO: Mheshimiwa Spika, ni kwamba GGM tuliwaeleza tarehe 27 Februari, 2018 watuandikie breakdown ya kuonesha ni jinsi gani wametumia fedha za CSR na majibu waliyonipa ni kwamba kwa mwaka 2017 wametumia kama nilivyosema katika jibu la msingi dola 6,358,000. Mheshimiwa Musukuma anachosema dola milioni 9.7 ni jumla ya miaka miwili yaani mwaka 2016 na 2017 kajumlisha kapata 9.7 lakini swali la msingi limeuliza mwaka 2017 jibu ni milioni 6.358. Mheshimiwa Spika, ahsante.
Waheshimiwa Wabunge, tunaendelea na Wizara ya Maliasili na Utalii. Swali linaulizwa na Mheshimiwa Hawa Mchafu.