Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Mpaka sasa inadaiwa kuwa hakuna dawa sahihi za kutibu ugonjwa wa kisukari. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti kuhusu dawa za kisukari?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Licha ya majibu mazuri, nina maswali mawili mafupi ya kumuuliza.
Kwa kuwa mpaka sasa hivi tafiti zinaendelea hapa duniani kuhusu ugonjwa wa kisukari, lakini mpaka sasa hivi azijazaa matunda, napenda kujua; je, tafiti hizi zimehusishaje tiba mbadala au tiba asilia kuhusu kutibu ugonjwa huu? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa kuwa ugonwja huu umeenea sana na unaleta vifo na inaonekana kuwa inawashambulia pia watoto wadogo na wajawazito na njia mojawapo inahusisha mambo ya lishe; je, kuna mkakati gani wa kutoa elimu kwa watu wote na hasa tukianza na Waheshimiwa Wabunge humu ndani kuhusu ugonjwa huu wa kisukari na hasa na mambo ya lishe? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli sisi kama Serikali, tunatambua kwamba sasa hivi hatuna tiba dhidi ya ugonjwa wa kisukari, lakini Serikali vilevile inatambua umuhimu wa tiba asili na tiba mbadala, ndiyo maana ndani ya Wizara ya Afya tuna Kitengo Maalum ambacho kinasimamia tiba asili na tiba mbadala.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kupitia taasisi zetu za Utafiti za Magonjwa ya Binadamu (National Institute of Medical Research) na Taasisi ya Tiba Asili ambayo iko Muhimbili, tumekuwa tunaendelea kufanya utafiti wa tiba mbalimbali ambazo zinapunguza kiwango cha sukari mwilini.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema, hatujapata tiba mbadala, lakini mtu yeyote ambaye amekuja na dawa ambayo anadhani inaweza kusaidia kupunguza makali ya ugonjwa wa kisukari, tumekuwa tunazifanyia utafiti na kuziangalia ili ziweze kutumika kwa binadamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, ameuliza kuhusiana na masuala ya lishe. Serikali mwezi Julai, 2017 imezindua mkakati wa Kitaifa wa masuala ya lishe na uzinduliwa na Mheshimiwa Waziri Mkuu na lengo ni kuhakikisha sasa tunaongeza nguvu na kuongeza juhudi kuhusiana na magonjwa ya kuambukiza. Magonjwa ya kuambukiza yanazidi kuongezeka. Tunakadiria kwamba wastani wa asilimia 13 za Watanzania wana ugonjwa wa kisukari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nasi tunaendelea kuhamasisha wananchi pamoja na Waheshimiwa Wabunge.
Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi tunavyoongea hapa Bungeni, wenzetu wa Bima ya Afya tumeleta Madaktari Bingwa wa magonjwa yote pamoja na kisukari na mimi nitoe rai kwa Waheshimiwa Wabunge, twende pale kliniki tupime afya zetu; siyo suala tu la Kisukari lakini magonwja yote pamoja na Saratani huduma hizi zinapatikana Bungeni.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishie kwa kutoa rai kwa wananchi wa Tanzania, magonjwa yasiyoambukizwa ikiwa ni pamoja na kisukari na shinikizo la damu, yanatokana kwa kutozingatia masuala ya lishe, kutofanya mazoezi na matumizi yaliyopindukia ya vilevi na sigara.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kuwasisitiza Watanzania kuzingatia msingi ya afya bora. (Makofi)

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Mpaka sasa inadaiwa kuwa hakuna dawa sahihi za kutibu ugonjwa wa kisukari. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti kuhusu dawa za kisukari?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza.
Kama alivyokiri Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba mgonjwa wa kisukari ili aweze kuishi ni lazima apate dawa za kisukari kila siku. Sasa kule Jimboni Bagamoyo kwenye Hospitali ya Wilaya kuna tatizo kubwa sana la upatikanaji wa dawa hizi kwa wagonjwa wa kisukari. Pia hata vipimia vya kiwango cha sukari navyo havipatikani hospitali.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kwamba dawa hizi na vipimo vinapatikana kwa urahisi ili wananchi wetu wa Tanzania waweze kuendelea kuishi?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi na vilevile majibu ya nyongeza ni kwamba tunatambua sasa hivi ongezeko kubwa sana la wagonwja wa kisukari, na sisi kama Serikali tumeelekeza nguvu zetu katika bajeti ambayo tumeitenga ya fedha kwa ajili ya dawa, vifaa tiba na vitendanishi, bajeti ya ugonjwa wa kisukari nayo imo ndani yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imeendelea kuongeza wigo wa utoaji wa huduma hii kwa kushirikiana na wadau, kusambaza vifaa vya upimaji, vilevile kusambaza dawa za insulin pamoja na vidonge vyake na katika mwaka huu wa fedha tumetenga shilingi bilioni 1.7 kwa ajili ya kununua matumizi ya insulin.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie kwamba hili suala la Bagamoyo tutajaribu kulifuatilia kuhakikisha kwamba sasa huduma hizo za dawa pamoja na vipimo vinapatikana.

Name

Rukia Ahmed Kassim

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza:- Mpaka sasa inadaiwa kuwa hakuna dawa sahihi za kutibu ugonjwa wa kisukari. Je, Serikali ina mpango gani wa kufanya utafiti kuhusu dawa za kisukari?

Supplementary Question 3

MHE. RUKIA AHMED KASSIM: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo la nyongeza.
Kwa kuwa kuna ongezeko kubwa la maradhi ya kisukari mpaka kuna baadhi ya watoto wachanga wanazaliwa wakiwa na maradhi haya; je, Serikali inaweza kutuambia nini chanzo kinachosababisha watoto wadogo kuzaliwa wakiwa na kisukari?

Name

Dr. Faustine Engelbert Ndugulile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigamboni

Answer

NAIBU WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika majibu yangu ya msingi nilisema kuna aina tatu za kisukari. Aina ya kwanza ni kisukari ambacho kinawapata watu katika umri mdogo na changamoto ya aina hii ni kwamba mtoto anazaliwa zile cell zake za kongosho ambazo kwa lugha ya kitaalam tunaita pancreas mwili wake wenyewe unaanza kuishambulia ikiona kwamba kile ni kitu ambacho ni kigeni ndani ya mwili. Kwa hiyo, hiyo ni aina moja ya kisukari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aina ya pili ya ni kisukari ambacho kinawapata watu katika umri mkubwa; na hiyo ndiyo hali ambayo ilikuwepo kutokana na jinsi tunavyokula, masuala ya uzito, matumizi ya vilevi na kutofanya mazoezi. Sasa hivi hali imeendelea kubadilika, hata watoto wadogo kwa sababu ya lishe. Mara nyingi ukiona mtoto anakuwa na uzito mkubwa na sisi kama wazazi tunaona kwamba ni faraja. Uzito uliopitiliza wa aina yoyote hauna tija na ni moja ya kitu ambacho kinapelekea sasa hivi watoto wetu kuanza kupata kisukari wakiwa na umri mdogo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, aina ya tatu ni kisukari ambacho kinatokana na ujauzito. Mama anapokuwa mjamzito kuna baadhi wanapata kisukari na mara nyingi kinaisha baada ya yule mtoto kuzaliwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ombi langu na kwa kujibu swali la Mheshimiwa Rukia Kassim, ni kwamba ni lazima sisi kama wazazi tuzingatie misingi ya lishe kwa watoto wetu, tusiwalishe chakula kilichopitiliza na watoto wetu wakawa wazito na uzito mkubwa kwa sababu nayo ina mchango mkubwa sana katika kupata kisukari.
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kuna kikundi kidogo ambacho miili yao tangu wamezaliwa zile cells zao za kongosho sinashindwa kufanya vizuri, hazizalishi insulin ama kwa kuwa na deformity ama kwa kuwa haikuumbwa vizuri zaidi au zikawa zimeshambuliwa; hawa wako wachache na wao watakuwa wanahitaji insulin tangu wakiwa na umri mdogo. Kubwa la msingi ni kuzingatia suala la lishe hususan kwa watoto hawa wasiwe na uzito mkubwa.