Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Halima Abdallah Bulembo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. JAMAL KASSIM ALI) aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kulifanyia Shirika la Umeme (TANESCO) lijiendeshe kwa faida?

Supplementary Question 1

MHE. HALIMA A. BULEMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Kwanza kabisa naomba nichukue fursa hii kuipongeza Serikali kwa uwekezaji mkubwa unaoendelea kwa TANESCO hasa eneo la uzalishaji, lakini hasara ya Shirika la TANESCO imekuwa inaongezeka kwa kasi zaidi. Kati ya mwaka 2015 mpaka 2017 ambapo TANESCO wameongeza hasara ya shilingi bilioni 124 mpaka shilingi bilioni 346.
Swali langu, Serikali ina mkakati gani unaotekelezeka kuhakikisha inapunguza hasara hizi na hatimaye kupata faida? (Makofi)
Swali langu la pili, TANESCO itagawanywa lini ili kutofautisha uzalishaji na usambazaji wa umeme? (Makofi)

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

WAZIRI WA NISHATI:
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri katika swali hilo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kabisa kwamba kwa muda mrefu Shirika letu limekuwa likijiendesha kwa hasara. Napenda kutoa taarifa tu katika Bunge lako kwamba hivi sasa Shirika la TANESCO limeanza kuongeza uzalishaji kuliko miaka iliyopita. Kipindi cha Julai mwaka 2017 hadi Machi mwaka huu, revenue ya TANESCO kwa wiki imeongezeka kutoka shilingi bilioni 29.1 mpaka shilingi bilioni 32.5. Kwa hiyo, ni maendelea mazuri ya Shirika letu katika hilo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sababu zilizochangia ni pamoja na kwanza kuzuia kuingiza vifaa kutoka nje, kitu kilichokuwa kinaligharimu shirika kwa kiwango kikubwa sana. Kitu cha pili ni kuwaunganisha wateja na LUKU kwa nchi nzima ambao ni mpango unaendelea na ni matumaini yetu Shirika litaendelea kuwaunganisha wateja na kupata mapato makubwa, na lingine ni kuondo kana na mafuta kama Mheshimiwa Naibu Waziri alivyojibu.
Mheshimiwa mwenyekiti, swali la pili kwamba ni lini Shirika litagawanywa? Mantiki kubwa ya Shirika hili ni kulionyesha kwamba linafanya kazi kwa manufaa. Suala la kuligawa ni suala ambalo ni endelevu, ni suala ambalo tunatakiwa kulitafakari kwa kina sana kwa sababu kufanya hivyo ni lazima pia tuangalie madhara yake. Mantiki kubwa vile vile ni kwamba lazima Shirika lijiendeshe kifaida na liweze kumudu majukumu yake na kazi hizo zinaendelea.