Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA B. MWAIFUNGA (k.n.y. MHE. TUNZA I. MALAPO) aliuliza:- Je, ni eneo gani limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha Kubangua Korosho katika Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 1

MHE. HAWA B. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru pamoja na majibu ya Serikali ya utengaji wa maeneo, lakini je, mpaka sasa ni waombaji wangapi ambao tayari wameshapewa maeneo hayo kwa ajili uwekezaji wa viwanda vya kuchakata korosho? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Mkoa wa Tabora ni moja kati ya Mikoa ambayo inalima tumbaku kwa wingi; je, ni lini Serikali itatenga maeneo ya uwekezaji wa viwanda vya korosho/ulimaji wa tumbaku ili wakulima wetu waweze kunufaika na tumbaku yao? Nakushukuru.

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, anauliza ni wangapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, utaungana na mimi kwamba suala la kitakwimu linahitaji kupata data mapema. Namwomba Mheshimiwa ili apate jibu la uhakika, angeleta kama swali la msingi ili tuweze kumtafutia takwimu ili tumpe majibu ambayo yanastahili.
Mheshimiwa Mwenyekiti, juu ya Mkoa wa Tabota kutenga eneo kwa ajili ya wakulima wa korosho; kasema korosho na wakati mwingine kasema tumbaku, sasa I am not so sure ni kwa ajili ya nini? Kwa sababu hata ukienda Tabora pia korosho zinastawi.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kama msingi ni kwa ajili ya wakulima wa tumbaku, namwomba Mheshimiwa Mbunge na bahati nzuri yeye ni Diwani katika eneo lake, mchakato ni vizuri ukaanzia kwenye Halmashauri, maana yeye analifahamu vizuri eneo la Mkoa wa Tabora ili wahakikishe kwamba maeneo kwa ajili ya wajasiriamali yanawekwa na yanatunzwa ili watu wetu waweze kupata maeneo hayo.

Name

Sikudhani Yasini Chikambo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAWA B. MWAIFUNGA (k.n.y. MHE. TUNZA I. MALAPO) aliuliza:- Je, ni eneo gani limetengwa kwa ajili ya ujenzi wa Kiwanda cha Kubangua Korosho katika Manispaa ya Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 2

MHE. SIKUDHANI Y. CHIKAMBO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa inayolima zao la korosho na yapo maeneo mengi ambayo ni rafiki kwa ujenzi wa viwanda vya korosho ikiwemo Wilaya ya Tunduru na Namtumbo ambapo zao la korosho linalimwa katika Wilaya hizo.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha tunajenga viwanda katika maeneo hayo ili wakulima sasa waweze kubangua korosho zao katika Wilaya hizo? Ahsante.

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Na mimi kwanza nampongeza Mheshimiwa Chikambo, lakini pia nawapongeza wote wanaofuatilia suala hili la korosho.
Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kutoa rai kwa sisi sote ambao tuko hapa na Watanzania wengine ambao watafanikiwa kuwafahamu wanaohitaji kuwekeza katika viwanda vya korosho; tafadhalini Tanzania ni katika nchi ambayo inatoa korosho bora sana. Hali kadhalika kupitia SIDO tunatengeneza viwanda vidogo vidogo vya kuweza kuendeleza ubanguaji au viwanda vya korosho. (Makofi)