Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Kemirembe Rose Julius Lwota

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka x-ray na CT-Scan kwenye Hospitali ya Sekou Toure Mkoani Mwanza?

Supplementary Question 1

MHE. KEMIREMBE J. LWOTA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Nashukuru kwa maelezo mazuri ya Mheshimiwa Waziri, lakini nasikitika kusema hajajibu swali langu. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, wananchi wa Mkoa wa Mwanza wanapata taabu kwa vipimo vya x-ray na CT-Scan na inawabidi waende kwenye Hospitali za Private ambazo ni gharama kubwa sana kufanya vipimo hivi. Swali langu: Je, ni lini Serikali itanunua machine ya CT-Scan na x-ray kwa hospitali yetu ya Mwanza ya Sekou Toure?

Name

Ummy Ally Mwalimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tanga Mjini

Answer

WAZIRI WA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kemirembe, Mbunge wa Viti Maalum, Mwanza kama fuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, alichojibu Mheshimiwa Naibu Waziri kinabaki kuwa ni sahihi. Tuna mradi wa Orion kwa ajili ya kununua vifaa tiba na kuvisimika katika hospitali zote za Rufaa nchini ikiwemo Hospitali ya Rufaa ya Sekou Toure, Mwanza. Tumepata fedha, juzi Mheshimiwa Rais katika ile fedha ya kufanya Semina Elekezi kwa Mawaziri shilingi bilioni 2.8 itatumika kwa ajili ya kununua vifaa hivi. Tulikwama muda mrefu kwa sababu hiyo fedha haijapatikana. Fedha imeshatolewa. Kwa hiyo, lini? Tayari, anytime, soon, tutaweza kusimika hivi vifaa katika Hospitali za Rufaa zote za Mikoa Tanzania.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Kemirembe tunakuomba sana, tunajua wananchi wanatumia gharama kubwa kufanya hivi vipimo katika hospitali binafsi na lengo letu ni kuwapunguzia mzigo Watanzania. Hili tunalifanya kabla ya mwaka huu wa fedha wa 2015/2016 haujaisha.