Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Allan Joseph Kiula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. ALLAN J. KIULA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itachukua hatua za makusudi kutenga mitaji kwa wakulima wadogo wadogo wa mazao ya vitunguu na alizeti katika Wilaya mpya ya Mkalama kupitia benki za mikopo au ruzuku toka Serikalini?

Supplementary Question 1

MHE. ALLAN J. KIULA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri. Ninayo maswali madogo mawili ya nyongeza mafupi sana.
Kwa kuwa Serikali imetoa takwimu za mikopo inavyotolewa, lakini uhalisia wenyewe mikopo imekuwa haiwafikii wananchi wa vijijini ikiwemo Mkalama na Wilaya ya Dodoma ambako wanalima sana alizeti.
Je, Serikali iko tayari kuzielekeza benki hizo kwenda kwenye maeneo hayo mahsusi ili kununua zao la alizeti na vitunguu.
Swali la pili, swali la pili, je, Waziri yuko tayari kufuatana na mimi kwenda kuona wakulima wa vitunguu ambao sasa wanavuna ili aweze kutoa maelekezo ya upatikanaji wa mbegu bora na pembejeo kwa haraka? (Makofi)

Name

Dr. Mary Machuche Mwanjelwa

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Mbeya Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nikianza na lile swali lake la nyongeza la (b) kwanza niko tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda katika Jimbo lake la Iramba Mashariki ili kujionea hilo.
Vilevile ni kwamba Serikali sasa hivi tunaimarisha tafiti zetu kuhakikisha kwamba tunapata mbegu ambazo zitakuwa bora na za uhakika na za bei nafuu tukishirikiana na wakala wetu wa mbolea.
Mheshimiwa Spika, pia tuko katika awamu ya mwisho ya kufanya tafiti ya mbegu tatu za alizeti na zenyewe hizo tafiti hatua ya mwisho tunategemea mwakani tutaanza kutumia.
Mheshimiwa Spika, nikija kwenye swali lake la (a) ni kwamba lengo la Benki ya Kilimo ni kuhakikisha kabisa kwamba Wilaya zote za Tanzania wanapata mikopo kupitia Benki hii ya Kilimo na kama nilivyosema kwa kujibu katika swali langu la msingi Benki ya Kilimo riba yake ni asilimia nane mpaka 14 kitu ambacho ni masharti nafuu. Vilevile unalipa kwa muda mrefu.
Mheshimiwa Spika, pia Benki ya Kilimo tumeigawa au imegawa kwa Kanda Nane na Mkalama iko katika Mkoa wa Singida na Mkoa wa Singida uko katika Kanda ya Kati kwa maana hiyo na yenyewe iko katika huo mpangilio.
Mheshimiwa Spika na vile vile Benki ya Kilimo ni kwamba inawafuata wakulima kule waliko. Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nakushukuru. (Makofi)