Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Elias Masala

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nachingwea

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Ngongo - Ng’apa - Milola ambayo ipo chini ya TANROADS?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN E. MASALA: Mheshimiwa Spika, naomba nishukuru sana kwa majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini pamoja na hayo naomba nitumie nafasi hii kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, ni muda mrefu sasa toka fedha hii shilingi bilioni moja itengwe na barabara ambayo imetajwa imefanyiwa sehemu tu ya matengenezo naomba kupata kauli ya Serikali, hizi kilometa 12 zilizobaki ni wakati gani zitamaliziwa kwa fedha ambayo imetengwa?
Swali la pili, naomba kuuliza Serikali imekuwa na kipaumbele cha kuunganisha barabara za Mikoa kama ambavyo jibu la msingi linavyojieleza. Nini mpango wa Serikali wa kukamilisha au kuanza ujenzi wa barabara ya lami kutoka Masasi kwenda Nachingwea, Nachingwea kwenda Nanganga ikiwa ni ahadi ambayo imetolewa kwa muda mrefu?

Name

Eng. Atashasta Justus Nditiye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muhambwe

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO:
Mheshimiwa Spika, ni kweli kuna kiasi cha fedha kilitengwa kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii na ilikuwa ni mkakati wa Serikali kulipa madeni. Katika kipindi hiki hadi Desemba Serikali ime-clear madeni kwa makandarasi zaidi ya shilingi trilioni 1.385 kwa maana hiyo hii ni fursa inatosha sasa kuanza kuendelea kutoa sasa mikataba kwa ajili ya ujenzi wa barabara. Nimhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge hizi kilometa 12 zitatangazwa na kuanza kutengenezwa wakati wowote.
Mheshimiwa Spika, pia niseme tu ni mpango wa Serikali kuunganisha Mikoa kama nilivyojibu katika jibu la msingi na Mheshimiwa Mwalimu Masala unakumbuka kwamba katika mpango ambao unaendelea kwa ajili ya ujenzi wa barabara kile kipande cha Nachingwea kwenda Nanganga kilometa 46 kitatangazwa wakati wowote, kipo kipande kingine cha Nachingwea - Ruangwa kilometa 45, lakini kuna kipande cha Ruangwa - Nanganga kilometa 58. Pia unatambua kwamba kuna ujenzi wa daraja kule kwenye Mto Lukuledi hii ni dhamira ya Serikali kuweza kuunganisha maeneo haya.
Mheshimiwa Spika, baada ya eneo hili kuwa limekamilishwa itakuwa ni sehemu ya kuunganisha Mkoa wa Lindi na Mkoa wa Ruvuma kwa maana kuwa unatambua kwamba ukitokea Nachingwea kwenda Kilimarondo utakuwa unaelekea kule Mindu upande wa Tunduru tutakuwa tunaunganika na wenzetu wa upande wa Ruvuma. Upande wa Morogoro pia kilometa 129 ukitokea Nachingwea kuelekea Liwale naona Mheshimiwa Kuchauka ananitazama hapa ni kwamba barabara hii sasa tutakapokuja kuanza kutengeneza itakuwa ni sehemu ya barabara ya kuunganisha upande wa Lindi kuelekea Mahenge kule Morogoro.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge nikuombe tu uvute subira ni mpango mzuri wa Serikali kuhakikisha kwamba tunaweza kutengeneza barabara hizi kuunganisha Mikoa na hii itatupa fursa sasa ya kuunganisha barabara ambazo zinakwenda kwenye Wilaya. Kwa hiyo tuvute subira na wananchi wajue Serikali inafanya kazi kubwa kulipa madeni na kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami. (Makofi)

Name

Dr. Dalaly Peter Kafumu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Ngongo - Ng’apa - Milola ambayo ipo chini ya TANROADS?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. DALALY P. KAFUMU: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, barabara ya kutoka Igunga kwenda Mwanzugi hadi Itumba ilikuwa na mkandarasi wa TARURA aliyewekwa na TARURA anaijenga, lakini uharibifu ulikuwa mdogo sana. Sasa hivi kutokana na mvua kama ulivyosema barabara hiyo imeharibika sana, naiomba Serikali itakuwa tayari kweli kuongezea bajeti kwa ajili ya kuijenga hiyo barabara ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Igunga? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Mheshimiwa Spika, kwanza niseme tu kwa ujumla ni kweli hali ya mvua zimekuwa excessive kwa maana ya kwamba kuna maeneo mengi yameharibika. Tunazo taarifa kule Koga hapapitiki, lakini tunazo taarifa kule Solwa hapapitiki na maeneo mbalimbali. Kama nilivyosema wakati nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Catherine kwamba tumejipanga kuhakikisha kwamba maeneo yanapitika.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Dalaly Kafumu sana muda mwingi tumezungumza juu ya barabara hii na kwa kweli swali lako nazungumza juu ya kuongeza bajeti. Tumejipanga kuitazama hii barabara, najua pia una hamu ya kwenda kuunganika na wenzetu kule upande wa Nyahua. Kwa hiyo, tunaitazama kwa umakini na tutakapopata fursa tutaendelea kuongeza bajeti ili hatimaye hii barabara iweze kutengenezwa vizuri na ipitike muda wote na pia ni huduma kwa wananchi wetu wa Igunga na maeneo ambayo yanazunguka Igunga. (Makofi)

Name

Daniel Nicodemus Nsanzugwako

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kasulu Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN E. MASALA (K.n.y. MHE. HASSAN S. KAUNJE) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itaanza kujenga kwa kiwango cha lami barabara ya Ngongo - Ng’apa - Milola ambayo ipo chini ya TANROADS?

Supplementary Question 3

MHE. DANIEL N. NSWANZUGWANKO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kuniona.
Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Naibu Waziri barabara ya Kidawe - Kasulu kilometa 63 tumezungumza na wewe na nikakujulisha kwamba mkandarasi hafanyi kazi sasa, anafanya kazi ndogon dogo tu kwa sababu hajalipwa fedha zake, barabara hiyo sasa ni miaka 12 inajengwa, ni kwa nini mkandarasi hapewi fedha zake akamaliza barabara hii?

Name

Elias John Kwandikwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO (MHE. ELIAS J. KWANDIKWA): Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge najua tumeongea mara nyingi sana kuhusu barabara za Kigoma, lakini niseme tu kwa wananchi wa Kigoma na Watanzania kwa ujumla, Serikali imejipanga vizuri sana kwa ajili ya kufanya matengenezo ya barabara kwa sababu kipaumbele chetu ni kuunganisha Mikoa yetu ya jirani na nchi za jirani. Kwa hiyo Mheshimiwa Nswanzugwanko unafahamu Kidahwe kwenda Kasulu kilometa 63 yuko mkandarasi pale, lakini kwa sasa kutokana na hali ya hewa kuna kazi ambazo zinafanyika wakati wa kipindi cha mvua, pamoja na kuwa tuna deni na mkandarasi yule upande wa Wizara tunafanya kila juhudi tuweze kuhakikisha kwamba tutapeleka fedha ili mvua zitakapopungua speed iwe kubwa.
Mheshimiwa Spika, niseme tu kwa barabara zote ukianzia Nyakanazi kuja Kakonko; kutoka Kankonko kuja Kibondo na kuja kuunganika Kigoma kuna juhudi nzuri na hatua nzuri tumefikia kwa ajili ya kutengeneza mikataba kwa ajili ya ujenzi wa barabara hii ili pamoja na viungo vyake kutoka Kasulu kwenda Manyovu pale border ziko kilometa 58 hivi lakini zipo tena kutoka Kakonko kwenda Mabamba na wewe unafahamu.
Kwa mkoa huu ambao ulikuwa umechelewa kufanya matengenezo ya barabara kiwango cha lami kwamba sasa ziko fedha ambazo harakati zinaendelea, kwa hiyo, Kigoma itafunguka na itaungana na mikoa mingine. Mheshimiwa Nswanzugwanko na wananchi wa Kigoma naomba wavute subira na tutaendelea kukupa feedback kujua hatua nzuri zinazoendelea kule Kigoma. Ahsante.