Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Wananchi wengi wa Tarafa ya Eyasi katika Wilaya ya Karatu wanajishughulisha na kilimo cha vitunguu maji, hata hivyo mavuno yanayotokana na kilimo hicho hupimwa kwa debe yanapouzwa badala ya kilo. Je, ni kwa nini Serikali isihakikishe na kusimamia uuzwaji wa mazao haya kwa kutumia kilo badala ya vipimo vya debe?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.
Swali la kwanza, vifungashio vya mazao haya ya vitunguu katika Tarafa ya Eyasi hufanyika kwa aina mbili. Kuna kifungashio cha Mkenya maarufu wanaita net ambapo net hii ikijazwa net tatu inakuwa sawa na debe kumi; na kuna kifungashio kingine kinaitwa kifungashio cha Mganda ambapo kifungashio hiki cha Mganda kinachukua kati ya debe nane mpaka tisa jambo ambalo kwa kweli linawaumiza wakulima.
Je, ni kwanini Serikali isihakikishe kunakuwa kuna standard ya vifungashio kwa wakulima hawa ili tusiweze kuwaumiza?
Swali la pili, tatizo la ujazo kupita kiasi maarufu kama lumbesa bado ni changamoto kwa wakulima hawa katika maeneo mbalimbali na zao hili linapofika sokoni wanunuzi wanachukua yale ambayo yamejazwa kwa maana ya lumbesa kuliko yale ambayo yana ujazo wa kawaida. Mfano, labda ujazo huu unatokea Singida, unatokea Kilimanjaro, unatokea Mang’ola wale ambao wana ujazo zaidi ndiyo itanunuliwa zaidi na wale ambao wana ujazo wa kawaida ambao ni standard inakuwa hainunuliwi.
Je, ni kwa nini sasa Serikali isiendelee kutia msisitizo ili jambo hili lisimamiwe katika maeneo yote kwa ukamilifu wake ili kuwepo na ujazo ambao unafanana?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana.
Kwanza, nisisitize tu kama ambavyo swali limejibiwa kwamba kipimo sahihi cha uzito wa aina ya bidhaa kama vitunguu ni kilogram, kwa hiyo tunachosema ni kwamba whether hicho kifurishi kitawekwa kwenye net, kitawekwa kwenye debe, kitawekwa kwenye kitu chochote kile ilimradi baada ya kuwekwa humo basi kipimwe kwenye uzito sahihi ambao ni kilogram ndivyo inavyostahili.
Pili, ulivyouliza kuhusu suala la lumbesa ni hivyo hivyo kwamba kwa mfano, unavyofungasha kwenye gunia likaitwa hili ni gunia la kilo 50 wakati ndani yake kumbe kuna kilogramu zaidi ya 50 inasababisha kwamba kwanza mkulima mwenyewe ananyonywa, lakini vilevile hata Halmashauri inaweza ikakosa mapato kutokana na kuwa na uzito ambao haustahili kutokana na kwenye kile kitu ambacho kimefungashiwa. Ijulikane kwamba siyo kwamba bidhaa zote zinakuwa na ujazo unaofanana. Kwa mfano, ujazo wa pamba kwenye kiroba ni tofauti na ujazo huo huo ukiwa ni wa viazi na ndiyo maana tunasisitiza kilogramu ambayo ndiyo kipimo sahihi ambacho kinastahili katika kupimia.
Mheshimiwa Spika, hivyo ninawaomba sana wananchi wote pamoja na wafanyabiashara kuhakikisha kwamba tunakuwa na mizani katika maeneo yetu ya kibiashara na hilo ndiyo linalosisitizwa sasa kuwa na masoko ya pamoja ili kuweza kuwafanya hawa wananchi wanaolima mazao kama hayo, kuweza kuwa na ushirikiano katika kudhibiti hali kama hiyo ya kuwa na vipimo ambavyo haviruhusiwi kisheria.

Name

Nape Moses Nnauye

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtama

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Wananchi wengi wa Tarafa ya Eyasi katika Wilaya ya Karatu wanajishughulisha na kilimo cha vitunguu maji, hata hivyo mavuno yanayotokana na kilimo hicho hupimwa kwa debe yanapouzwa badala ya kilo. Je, ni kwa nini Serikali isihakikishe na kusimamia uuzwaji wa mazao haya kwa kutumia kilo badala ya vipimo vya debe?

Supplementary Question 2

MHE. NAPE M. NNAUYE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru ka kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:
Mheshimiwa Spika, itakumbukwa msimu uliopita soko la mbaazi lilisababisha kuanguka kwa bei ya mbaazi kutoka shilingi 2,000 kwenda mpaka shilingi 150, Serikali ilihaidi hapa Bungeni kwamba itahakikisha inahangaika kupata soko la kuaminika la zao hili. Sasa ni msimu wa kilimo hicho, Serikali imefikia wapi kupata soko hili na kama hali bado haileweki tuwashauri wananchi wetu waachane na mbaazi badala yake wajikite kwenye mazao mengine ambayo yana soko la uhakika?

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA, BIASHARA NA UWEKEZAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, ni kweli kabisa katika msimu huu ulioisha kulikuwa na hali isiyopendeza katika soko la mbaazi, hiyo ni kutokana na kwamba wadau ambao tulikuwa tunawategemea sana katika biashara hiyo ilikuwa ni wenzetu kutoka India. Niseme tu kwamba mbaazi ni chakula kizuri, mbaazi ni chakula ambacho kina protini na hata sisi wenyewe tunaweza tukala siyo kuwategemea tu watu wa maeneo mengine. Kama tunaavyosema kwamba biashara ni ushindani na kila watu wanajitahidi kuhakikisha kwamba wanakidhi soko lao la ndani, upande wa Tanzania tunaendelea kutafuta soko wakati huo tunaendelea kusisitiza kwamba hata wenyewe tupende kutumia mbaazi.
Mheshimiwa Spika, nimepita hapa katika masoko yetu kwa mfano soko la hapa Dodoma, nilipofuatilia nilikuta kwamba mbaazi zinauzwa mpaka shilingi 1,800 kwa kilo. Soko la pale Dar es Salaam kwenye supermarket mbaazi inauzwa mpaka shilingi 2,400 kwa kilo. Kwa hiyo, tusitegemee tu soko kutoka nje hata ndani ya nchi bado kuna watu ambao wananweza kula mbaazi na mimi mwenyewe ni mtumiaji wa mbaazi, vilevile tunategemea kwamba hata kupitia shule zetu tutaweza pia kuhamasisha na kuweza kupeleka chakula cha aina hiyo wakati masoko mengine ya nje yakiendelea kutafutwa.