Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Juma Kombo Hamad

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:- Je, Zanzibar ina nafasi gani katika Jumuiya za Kimataifa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. JUMA KOMBO HAMAD: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba sasa nimuulize Mheshimiwa Waziri maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, ni miaka 20 sasa toka pale ambapo Zanzibar ilitakiwa ijiondoe kwenye Jumuiya hii ya OIC. Zanzibar ilijiunga na Jumuiya ya OIC kwa maslahi ya kiuchumi na si siasa wala siyo dini kama vile wengine walitafsiri katika kipindi hicho. Naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri, je, sasa kwa sababu Tanzania kwa miaka 20 imeshindwa kujiunga kama ilivyoahidi ipo tayari kutoa ruhusa kwamba Zanzibar ina haki ya kujiunga na taasisi hii? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, Mheshimiwa Waziri ametaja miradi mingi na ameenda mbali lakini nataka kuona tu kwamba kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Tanzania, anionyeshe kwa Ibara kwamba Zanzibar ina nafasi hii ndani ya Jumuiya za Kimataifa lakini yeye kazungumza masuala mengine ambapo na mimi nitaelekeza nguvu zangu huko huko.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kataja miradi hapa, miradi hii kwa bahati mbaya au nzuri yote imetekelezwa upande mmoja wa Kisiwa cha Unguja, si vibaya yote ni Zanzibar, lakini katika ahadi ambayo imekuwa ikiwekwa kila bajeti ni upanuzi wa uwanja wa ndege wa Pemba pamoja na bandari ya Mkoani Pemba. Naomba Mheshimiwa Waziri anieleze ni lini sasa bandari hii na huu uwanja wa ndege kupitia Jumuiya hizi za Kimataifa utakelezwa na itapanuliwa kama walivyoahidi? Mheshimiwa Spika, nashukuru. (Makofi)

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, anasema kwamba kwa miaka 20 Zanzibar imejiondoa katika kujiunga na ile Jumuiya ya Kiislam na kwamba sisi kama Tanzania iko tayari kuiruhusu Zanzibara kujiunga na taasisi hiyo? Jibu langu nasema bado liko vilevile kama lilivyojadiliwa katika Bunge hili katika siku za nyuma na maamuzi yaliyofanyika siku za nyuma kwamba kama ni faida bado Tanzania ikiwemo Zanzibar inaweza ikafaidika tu kwa mahusiano yaliko baina yetu na nchi ambazo ni wanachama katika Jumuiya hiyo hiyo ya Kiislam.
Mheshimiwa Spika, kama anavyojua kwenye Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania suala la dini tumesema kwamba si suala ambalo tunataka tulijadili au kujihusisha na kuweza kuweka utenganishi kati ya sehemu ya nchi na nchi nyingine. Kwa hiyo, bado msimamo uko pale pale kwamba sisi kama Tanzania hatujakubaliana kwamba Zanzibar ijiunge na taasisi hiyo. Hata hivyo, faida za taasisi hiyo bado tunaweza kufaidika nazo kwa kufanya mikataba baina sisi kama Tanzania au upande wa Zanzibar kushirikiana na nchi hiyo kwa kufanya bilaterals. (Makofi)

Name

Maryam Salum Msabaha

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:- Je, Zanzibar ina nafasi gani katika Jumuiya za Kimataifa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Supplementary Question 2

MHE. MARYAM SALUM MSABAHA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ili nami niulize swali la nyongeza. Mheshimiwa Waziri kumekuwa na malalamiko nafasi nyingi za Balozi Wazanzibari wengi wanapelekwa nchi za Kiarabu. Je, kama malalamiko haya ni kweli hamuoni kama sasa kuna umuhimu wa kufanya uwiano sawa ili Wazanzibari wengi wasipelekwe nchi za Kiarabu nao wapelekwe nchi hizi nyingine kama Marekani, Ulaya na kwingineko?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Maryam Msabaha, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, anasema kwa siku nyingi sana wamekuwa wakilalamika kwamba Watanzania ambao wanatoka Zanzibar wanapoteuliwa kuwa Mabalozi wanapelekwa kwenye nchi za Kiarabu zaidi. Naomba niweke taarifa hii sawa kwamba tunapowateua Mabalozi tunawateua kwa kigezo cha weledi, ufahamu wao na uwezo wao wa kushika nafasi hiyo ya kiubalozi. Tunapowateua kuwapeleka mahali popote iwe ni kwenye nchi za Kiarabu, Afrika, Ulaya au Latin America wako sawa kabisa kwa status.
Mheshimiwa Spika, nimwambie tu siyo tu kwamba katika hizi nchi za Kiarabu wako Watanzania ambao wanatoka Zanzibar yaani Mabolozi ambao wanatoka Zanzibar tu wapo pia wameteuliwa na wamekwenda huko wanatoka pia Tanzania Bara. Naomba hisia hizo za kusema kwamba tunawapeleka Mabalozi kwenye nchi za Kiarabu wale tu ambao wanaotoka Zanzibar zitolewe.
Mheshimiwa Spika, vilevile niseme tu kwamba sisi tunapowapeleka Mabalozi mahali popote iwe nchi za Kiarabu, tunaangalia pia additional value ambayo anaweza akaifanya. Sisi tunapowapima wale ambao pengine wanatoka Zanzibar au Bara tunajua kabisa kwamba kwa kufanya kazi kule watasimamia maslahi ya Taifa na maslahi wa nchi hii kwa ujumla wake.
Mheshimiwa Spika, wako Watanzania Mabalozi ambao wanatoka Tanzania Bara wameteuliwa hivi karibuni na wamekwenda kule. Nafasi hiyo itaendelea kufanywa hivyo na wale wanaotoka Zanzibar na wao ikifika wakati tunaweza tukawachukua tukawapeleka sehemu nyingine.
Mheshimiwa Spika, niseme tu kwamba hakuna upendeleo wala dharau kwamba wanapopelekwa kwenye nchi za Kiarabu maana yake kwamba tumewaonea na wanafanya kazi nzuri. (Makofi)

Name

Jaku Hashim Ayoub

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

House of Representatives

Primary Question

MHE. JUMA KOMBO HAMAD aliuliza:- Je, Zanzibar ina nafasi gani katika Jumuiya za Kimataifa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania?

Supplementary Question 3


MHE. JAKU HASHIM AYOUB: Mheshimiwa Spika, nami nikushukuru kwa kuniona. Mheshimiwa Naibu Waziri alipokuwa akijibu swali la msingi hapa alitaja Balozi, sasa nataka kujua Balozi zote za Tanzania duniani ziko ngapi na Zanzibar wamegaiwa ngapi?

Name

Dr. Susan Alphonce Kolimba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Spika, Balozi za Tanzania ziko 40 na Mabalozi wanaotoka Zanzibar wako tisa na hiyo ni asilimia 22.5 ya Mabalozi wote waliopo. (Makofi)