Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saul Henry Amon

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rungwe

Primary Question

MHE. SAUL H. AMON aliuliza:- Barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu – Matwebe hadi mpakani ni barabara kubwa na inapita katika Kata nne ambazo ni Masoko, Bujela, Masukulu na Matwebe, barabara hii ilishapandishwa daraja na kuwa ya TANROADS:- Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili kuondoa adha kwa wananchi kwa kupoteza kipato kwa mazao kuharibika njiani?

Supplementary Question 1

MHE. SAUL H. AMON: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri. Naomba kama Naibu Waziri ana nafasi aone hali ilivyo mbaya, kile kipande cha kata nne hata kwenda kuwasalimia tunaogopa kwa sababu tunatoa ahadi lakini haitimizwi. Je, yuko tayari kuongozana na mimi akaangalie hali ilivyo mbaya ya hicho kipande cha kutoka Njiapanda mpaka Mpakani? (Makofi)
Mheshimiwa Spika, swali la pili, vilevile barabara hii iko sawa kabisa na barabara ya Igogwe – Mchangani - Mbeye One. Mazao ni mengi lakini wananchi wa eneo hilo wanauza mazao kwa bei ya chini sana kwa sababu hakuna usafiri. Naomba Waziri atakapokuja Rungwe aangalie vipande hivyo viwili na aone ukweli na hali halisi ilivyo kwa wananchi wa Rungwe. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, kubwa ambalo Mheshimiwa Mbunge analitaka kwangu mimi ni suala la kupata fursa ya kwenda kutembelea ili nijionee kwa macho hali halisi ikoje. Mimi niko tayari baada ya kwamba tumehitimisha shughuli za Bunge la Bajeti, nikiamini kwamba bajeti yetu itakuwa imepita salama ili nikajionee na tushauriane.
Mheshimiwa Spika, lakini pia naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, kwa kupitia chombo chetu cha TARURA ambacho tumekianzisha tutahakikisha tunawaelekeza maeneo yote ambayo ni korofi yaweze kutengenezwa ili yapitike vipindi vyote.

Name

Deo Kasenyenda Sanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Makambako

Primary Question

MHE. SAUL H. AMON aliuliza:- Barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu – Matwebe hadi mpakani ni barabara kubwa na inapita katika Kata nne ambazo ni Masoko, Bujela, Masukulu na Matwebe, barabara hii ilishapandishwa daraja na kuwa ya TANROADS:- Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili kuondoa adha kwa wananchi kwa kupoteza kipato kwa mazao kuharibika njiani?

Supplementary Question 2

MHE. DEO K. SANGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kuniona. Barabara ya kutoka Ilunda - Igongolo yenye kilometa tisa ni ya TANROADS na imetengenezwa lakini mbele inaendelea kwenda Kivitu – Kifumbe – Makambako urefu wa kilometa 19 na tuliomba ipandishwe hadhi. Ni lini Serikali itaipandisha hadhi barabara hii kuwa ya TANROADS ili itengenezwe iweze kuzunguka kama ambavyo imefanyika kwa zile kilometa 9?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, sisi sote ni mashuhuda tukiwa katika Bunge lako Tukufu Wabunge wengi walikuwa wakiomba barabara zao zipandishwe hadhi na zichukuliwe na TANROADS. Mawazo hayo Bunge lako Tukufu likachukua na kulifanyia kazi kwa nini Wabunge wengi tumekuwa tukiomba barabara zichukuliwe na TANROADS?
Mheshimiwa Spika, jibu ni jepesi kabisa kwamba kwa sababu barabara ambazo ziko chini ya TANROADS zimekuwa zikitengenezwa kwa kiwango kizuri. Ndiyo maana tukasema tuanzishe chombo ambacho kitakuwa kinafanya kazi nzuri kama TANROADS wanavyofanya na ndiyo essence ya kuanzishwa kwa TARURA.
Mheshimiwa Spika, naomba tutoe fursa kwa chombo hiki ambacho tumekianzisha ndani ya Bunge lako kifanye kazi. Naamini kinafanya kazi nzuri kwa sababu tumeanza kupata taarifa kutoka kwa baadhi ya Wabunge, wengi wana- appreciate jinsi ambavyo TARURA imeanza kufanya kazi. Naamini hata Mheshimiwa Mbunge kilio chake si barabara kuchukuliwa na TANROADS bali barabara itengenezwe ipitike kwa vipindi vyote.

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Primary Question

MHE. SAUL H. AMON aliuliza:- Barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu – Matwebe hadi mpakani ni barabara kubwa na inapita katika Kata nne ambazo ni Masoko, Bujela, Masukulu na Matwebe, barabara hii ilishapandishwa daraja na kuwa ya TANROADS:- Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili kuondoa adha kwa wananchi kwa kupoteza kipato kwa mazao kuharibika njiani?

Supplementary Question 3

MHE. PAULINE P. GEKUL: Mheshimiwa Spika, nikushukuru sana kwa kunipa nafasi niulize swali moja la nyongeza. Mheshimiwa Naibu Waziri mapema mwaka huu alifanya ziara katika Halmashauri yetu ya Mji wa Babati nasi tukakueleza juu ya ahadi ya Mheshimiwa Rais kuhusu ujenzi wa barabara za lami kilometa 20 alizoahidi wakati wa kampeni. Wananchi wa Babati wanauliza ni lini ahadi ya Mheshimiwa Rais ya kilometa 20 za lami katika Mji wao wa Babati utaanza?

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli nilipata fursa ya kutembelea Babati, lakini pia katika ziara yangu sikumbuki kama Mheshimiwa Gekul alisema hilo. Hata hivyo, kwa sababu ni ahadi ya Mheshimiwa Rais na ahadi zake ni mkataba baina yake yeye na wapiga kura na mkataba huu ni ndani ya miaka mitano, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, yale yote ambayo yameahidiwa na Mheshimiwa Rais yanaratibiwa na ndani ya miaka mitano yataweza kutekelezwa.

Name

Magdalena Hamis Sakaya

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Kaliua

Primary Question

MHE. SAUL H. AMON aliuliza:- Barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu – Matwebe hadi mpakani ni barabara kubwa na inapita katika Kata nne ambazo ni Masoko, Bujela, Masukulu na Matwebe, barabara hii ilishapandishwa daraja na kuwa ya TANROADS:- Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili kuondoa adha kwa wananchi kwa kupoteza kipato kwa mazao kuharibika njiani?

Supplementary Question 4

MHE. MAGDALENA H. SAKAYA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kunipa nafasi hii muhimu sana. Kutokana na mvua ambazo zinaendelea kunyesha barabara nyingi za Jimbo la Kaliuwa zimekatika na hazipitiki kabisa, zikiwemo barabara ambazo zinatoa magari Kahama kwenda Kaliuwa na kwenda vijiji mbalimbali. Barabara ya Kahama kwenda Ugaza imekatika, Kahama kwenda Usinge imekatika, Usinge kwenda Lugange Mtoni imekatika na Kahama kwenda Mpanda Mloka imekatika.
Mheshimiwa Spika, TARURA waliomba bajeti ya dharura ili waweze kufungua barabara hizi ambazo sasa hivi hazipitiki kabisa, wananchi wametengeneza mitumbwi ya kupita. Naomba Serikali ituambie mpango wa haraka wa kuweza kuwapa fedha kwa TARURA, Wilaya ya Kaliuwa ili waweze kutengeneza barabara hizi ziweze kupitika kwa sababu ni barabara kubwa za uchumi? Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kuhusu suala la barabara nyingi kukatika kwa sababu ya mvua zinazonyesha, naomba nimhakikishie na itakuwa vizuri mimi nikishatoka baada ya hapa tukafanya mawasiliano ili tuhakikishe haraka kabisa barabara hizo zinatengenezwa ili ziweze kupitika. Kwa sababu ni lengo la Serikali kuhakikisha kwamba barabara zote zinapitika kwa vipindi vyote.
Mheshimiwa Spika, ametaja barabara nyingi, itapendeza kama tutawasiliana halafu tuone jambo gani la haraka linaweza likafanyika ili wananchi wasije wakakwama katika shughuli zao.

Name

Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Primary Question

MHE. SAUL H. AMON aliuliza:- Barabara ya Pakati – Njugilo – Masukulu – Matwebe hadi mpakani ni barabara kubwa na inapita katika Kata nne ambazo ni Masoko, Bujela, Masukulu na Matwebe, barabara hii ilishapandishwa daraja na kuwa ya TANROADS:- Je, ni lini barabara hii itaanza kujengwa ili kuondoa adha kwa wananchi kwa kupoteza kipato kwa mazao kuharibika njiani?

Supplementary Question 5

MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Tatizo la barabara katika Jimbo la Songea Mjini hususan barabara itokayo Songea Mjini kupita Kata ya Ruvuma na Kata ya Subira ni kubwa sana kiasi kwamba haipitiki na hata mimi Februari hii nilikwama wakati natumia barabara hiyo. Je, Mheshimiwa Waziri ni lini barabara hiyo itaweza kutengenezwa kwa kiwango cha lami ili kuwahudumia wananchi wa Jimbo la Songea Mjini? (Makofi)

Name

Josephat Sinkamba Kandege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalambo

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. JOSEPHAT S. KANDEGE): Mheshimiwa Spika, ni lini barabara hiyo itaweza kutengenezwa kwa kiwango cha lami, najua kiu yake kubwa angetamani hata kesho barabara ikakamilika, lakini ni ukweli usiopingika kwamba kutengeneza barabara kwa kiwango cha lami inahitaji pesa za kutosha.
Mheshimiwa Spika, hivyo, ni vizuri katika vipaumbele vya halmashauri yake na katika vyanzo vya mapato walivyonavyo wakaweka kama ni kipaumbele. Pia ni vizuri nikipata fursa wakati nikiwa katika ziara kwenda Ruvuma nitapita ili tushauriane na Mheshimiwa Mbunge tukiwa site ili tuone umuhimu wa barabara hii.